Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w74 4/1 kur. 159-163
  • Uchawi Waenea Pote—Je! Ni Hatari?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uchawi Waenea Pote—Je! Ni Hatari?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAKANISA, SAYANSI VYASHINDWA KUTOA UHITAJI
  • HATARI
  • MWANZO WA MASHETANI
  • MUNGU ANAMLINDA MKRISTO WA KWELI
  • Unajua Nini Kuhusu Uchawi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Unachopaswa Kujua Kuhusu Uchawi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Ni Nini Husababisha Uchawi?
    Amkeni!—1999
  • Ukweli Kuhusu Uchawi na Ulozi
    Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
w74 4/1 kur. 159-163

Uchawi Waenea Pote​—Je! Ni Hatari?

KATIKA nyakati za karibuni mazoea ya uchawi yamepenya katika jamii isiyo na tabia ya asili. Bila shaka, uchawi au ulozi si jambo jipya.

Biblia inataja walozi na vile vile makuhani wenye kuzoea uchawi katika Misri nyuma huko katika karne ya kumi na sita B.C.E. (Kut. 7:11) Mnamo miaka ya 500 C.E. mpaka 1500 C.E. katika Ulaya, wale walioshukiwa kuwa wenye uchawi waliuawa. Lakini, kwa karne nyingi uchawi na ulozi vimekuwa vyenye kuzoewa kwa uhuru zaidi katika Afrika, Asia, Amerika ya Kusini na visiwa vya bahari kama dini zilizo kubwa.

Lakini nini sababu ya umaarufu wake na kukubaliwa kwake kunakoendelea katika nchi za Magharibi, kama vile United States, ambapo, kulingana na habari fulani, kuna “makumi ya maelfu . . . wanaochezacheza katika uovu kwa kukusudia, uchawi, ulozi na namna nyingine za uchawi au uganga”?

Imani ya mafumbo na uchawi vimewavuta vijana sana. Vinaonekana sana katika viwanja vya vyuo vikuu leo. Mchunguzi mmoja anadai kwamba kuna “walau mchawi mmoja na nyakati nyingine kusanyiko la wachawi,” katika kila uwanja. Ingawa ni wachache tu wa wanafunzi wanaojitia kabisa katika matendo ya uchawi, wengi wanauona kwa kuupendelea. Wao wanasema wanatafuta kitu cha kushikamana nacho, kwamba wamepaswa wajulikane, kutakiwa na kupendwa. Kama wasemavyo, wanajisikia imewapasa ‘wayarudie matakatifu.’

MAKANISA, SAYANSI VYASHINDWA KUTOA UHITAJI

Basi, kwa sababu gani vijana hawa hawakuzirudia dini za Kristendomu zilizotengenezwa? Kama ilivyosemwa na Dr. Andrew M. Greeley, padre wa Kikatoliki aliyemo katika National Opinion Research Center, Chuo Kikuu cha Chicago, mwanafunzi mmoja alitoa sababu wakati aliposema:

“Nani ulimwenguni aweza kutazamia kupata cho chote kitakatifu makanisani?”

Lakini je! sayansi na njia ya kufikiri ya kibinadamu na ya kimwili havikutoa jibu? Sivyo. Kwa kweli, kushindwa kwavyo kunatajwa kama mojawapo ya sababu zenye nguvu zaidi za ‘kuyarudia matakatifu.’ Kama vile mwanafunzi mwingine alivyotoa maoni yake:

“Ebu na tuwe thabiti, sayansi imekufa. Ingawa magazeti yalikuwa yakikazia fikira kwenye kifo cha Mungu, kwa kweli sayansi ndiyo iliyokuwa ikifa.”

Mwingine aliongezea:

“Sayansi haikukomesha vita, haikukomesha udhalimu, nayo haitendi kwa kuyaitikia mahitaji yaliyo mengi zaidi ya mwanadamu.”

Hatuwezi kuukana uhakika wa kwamba mahitaji ya mwanadamu na magumu hayawezi kuondolewa na filosofia ya mambo ya kimwili. Kwa vyo vyote vitu vyote anavyovihitaji mwanadamu havitolewi na sayansi ya kisasa iliyokadiriwa. Mwanadamu anao upande wa kiroho katika maisha yake, akijua kwamba kuna nguvu zilizo kuu kumpita yeye. Lazima awe na sababu ya kuishi, na tumaini. Lazima awe na upendo vile vile, usiopatikana katika filosofia ya mambo ya kimwili. Na kwa kuwa dini za Kristendomu zimekuwa sehemu kamili ya huu ulimwengu wa mambo ya kimwili, zimeshindwa vile vile kuleta majibu yo yote ya kweli. Hazikukutana na uhakika. Alisema mwanafunzi mmoja:

“Tunachohangaikia kwa kweli ni kama kitu cho chote ni hakika, yaani, kama ni hakika kabisa. Je! kuna cho chote chenye nguvu sana kwamba kinaweza hata kutufanya sisi hakika?”

HATARI

Katika uchunguzi huu, je! wale wanaogeukia uchawi au mafumbo wamelipata jibu? Au kuna hatari ya kweli katika kujitia katika mambo haya, hata kuyajaribu? Onyo kwa wote wanaochezacheza katika uchawi limo katika maneno ya Dr. Greeley, anayesema: “Uovu wa kukusudia waweza kuwa hatari, kama vile kisa cha Manson na uuaji wa kawaida unavyopaswa kuonyesha wazi.”

Wengine wa wale wanaojidai kufanya uchawi wanasema wanazoea “uganga,” lakini wanaepuka “ulozi.” (Ulozi unatia ndani na kutoa maneno ya kuunuizia yenye kudhuru, kufanya kawaida za dini au kutengeneza dawa za kunywa uwaumize wengine.) Hata hivyo, kawaida yao inafanana sana na ile ya ‘wachawi,’ wengi wao ambao ni “wafanya uovu wa kukusudia.” Hatari ya uchawi yenye kuaibisha ilionyeshwa wazi na mmojawapo wa “wachawi” mwenyewe, aliyekubali kwamba uchawi “waweza kuwa hatari sana hata ikiwa huuamini. . . . Unaweza kukupumbaza kwa maana unamkana Mungu na udugu na kila wazo jema lililo la asili katika mtu.”

Kuna hatari kutoka pande zote kwa wale wanaojitia katika namna yo yote ya uchawi. Mara nyingi viongozi wao wanataka kuwatumia wao kwa faida yao tu. Mchawi hapendezwi kweli kweli na wale ambao anafanyia uchawi wake. Mmoja alieleza namna ya kweli ya mazoea haya aliposema: “Nimeona nina uwezo mwingi zaidi juu ya watu kutokana nao. Waweza kuwachunguza sana na kucheza michezo pamoja nao. Ni matembezi ya ajabu ya nafsi.”

Zaidi ya haya, kuna uwezekano mkubwa kwamba wale wanaochezacheza katika uchawi watavutwa kwenye matumizi ya dawa za kulevya na mazoea ya ufisadi, yenye aibu na yenye kuchukiza. Juu ya yote, wamo katika hatari iliyo kubwa zaidi ya kuja kabisa chini ya uongozi wa mashetani, ambamo wanaweza kufanya karibu uhalifu wa namna yo yote, kutia na kujiua wenyewe au kuua wengine, au huenda wakawa wenda wazimu.

Je! “mashetani” hawa ni watu hakika? Au ni nguvu tu za uovu katika mwanadamu, kama wengine wasemavyo? Ye yote asidanganyike kufikiri wao si watu hakika. Biblia inayahakikisha yaliyosemwa juu ya hatari zilizomo katika uchawi nayo inatupa wonyesho hakika wa mashetani. Inaonyesha kwamba mashetani ni watu wa kiroho, ambao mkubwa wao ni Shetani Ibilisi. Huenda wengine wakane kuwako kwake, jambo linalowafanya waelekee zaidi kupatwa na madanganyo yake. Imani katika Neno la Mungu ni ulinzi, “Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana [sisi tuaminio yasemwayo na Neno hilo] hatukosi kuzijua fikira zake.”​—2 Kor. 2:11.

MWANZO WA MASHETANI

Biblia inaonyesha wazi kwamba Shetani ndiye adui mkubwa wa Mungu na mwanadamu. Mwana wa Mungu, aliyekuwa kando ya Baba yake mbinguni mbele ya kuja duniani, alikuwa amekwisha kumwona Ibilisi na kukutana naye mwenyewe. Yeye alimwita Shetani “baba wa uongo.” (Yohana 8:44, NW; 17:5; Ayubu 1:6; Yuda 9) Huyu alimwasi Mungu, akiipinga enzi ya Mungu na kuwashawishi wanadamu wa kwanza wawili kutenda dhambi. (Mwa. 3:1-5) Katika siku za Nuhu, mbele ya gharika ya dunia, hesabu isiyotajwa ya malaika wengine vile vile ilifuata mwendo wa uasi, wakiacha cheo chao katika utumishi wa Mungu na mahali pao pafaapo katika makao ya kiroho yasiyoonekana. Walijivika miili ya kibinadamu kusudi watimize tamaa iliyopotoshwa, kuoa wanadamu wajapokuwa wenyewe walikuwa wametoka katika makao ya kiroho. (Mwa. 6:4, 5) Hii yaeleza kwa sababu gani kawaida za uchawi mara nyingi zinafuatwa na uchi, mifano ya uzaaji na dansi, hata karamu za uasherati.

Mtume Petro aliandika: “Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu.” Petro anaendelea kuzungumza juu ya uharibifu wa Mungu wa ulimwengu huo uliopotoshwa na mashetani na ulioitangulia Gharika. (2 Pet. 2:4, 5) Yuda ndugu mzazi mmoja wa Yesu vile vile alizungumza juu ya hukumu waliyopasishwa malaika hawa, akisema: “Malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, [Mungu] amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.” (Yuda 6) Hawakuruhusiwa na Mungu kuwa na mwangaza mwingine zaidi wa kimungu wala mgawo wa utumishi, nao wamefungiwa. Kuna ushuhuda kwamba, tangu Gharika, hawajaweza kujivika miili ya kibinadamu, bali, ili watimize tamaa yao iliyopotoshwa, wamekaa ndani ya wanadamu na kuwaongoza. Mwana wa Mungu Yesu Kristo alipokuwa duniani, alikutana na watu kama hao waliopagawa na mashetani wakiwa katika hali ya kusikitikiwa naye aliwaponya, akiyafukuza mashetani.​—Mt. 12:22; Marko 5:1-6.

Kufufuka kwa uchawi, ulozi na namna nyingine za ushetani katika nyakati hizi ni utimizo kweli kweli wa masimulizi ya Maandiko ya “siku za mwisho” za hii taratibu ya mambo. Mashetani wanajua karibuni wataharibiwa, na kwa hiyo wanatokeza jeuri na upotovu duniani kusudi wamchukue kila mtu kwenye uharibifu pamoja nao, ikiwezekana.​—2 Tim. 3:1-5; Ufu. 12:9, 12; Mt. 8:29-32; Marko 1:23, 24.

MUNGU ANAMLINDA MKRISTO WA KWELI

Je! Mkristo wa kweli anayeishi katika mtaa ambapo uchawi au ulozi vinazoewa amwogope mungu au shetani anayeabudiwa, au mchawi mwenyewe? Hapana, kwa maana “jina la [Yehova] ni ngome imara; mwenye haki huikimbilia, akawa salama.” (Mit. 18:10) Yehova Mungu Mwenye Nguvu Zote Ndiye aliyehukumia mashetani uharibifu. Mkristo wa kweli, kwa hiyo, kwa sala kwa Yehova katika jina la Kristo aweza kuutegemea uwezo huo umlinde na shetani ye yote au maneno yo yote yaliyonuizwa na mchawi. Neno la Mungu Biblia kwa kufariji linatuambia: “Malaika wa [Yehova] hufanya kituo, akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.”​—Zab. 34:7.

Kwa hiyo, anayeweka tumaini katika Mungu ataufuata mwendo ambao mashahidi wa Yehova wanafuata katika sehemu zote za dunia. Wao hawajikunji kwa woga wala kuzifuata desturi za wenye woga wanaowazunguka. Wao wanaifuata amri ya Biblia: “[Yehova] asema hivi, Msijifunze njia ya mataifa, wala msishangae . . . Maana desturi za watu hao ni ubatili.”​—Yer. 10:2, 3.

Kwa mfano, katika Afrika watoto wa mashahidi wa Yehova hawaonekani wakiwa na nyuzi nyeusi na nyeupe shingoni pao wala katika vifundo vyao vya mikono za kuwalinda na mungu “Sambio.” Wao hawawaungi wanavijiji katika kuvunja matawi ya miti, kutupa mawe au kulaani, ili kuwazuia ndege fulani wa usiku wanaoitwa “ndege wa wachawi” wasitue mitini, ili kuzuia kifo kisitokee kijijini. Wakristo wanajua kwamba ndege hawa ni uumbaji wa Mungu, wanaokuja usiku kutafuta wadudu au wanyama kama panya. Wala wao hawajizuii wasiwashike wanaoitwa samaki “watakatifu” wawale. Wao wameipuza desturi ya mahali pao nao wakaifahamu miungu ya mahali pao kuwa si miungu hata kidogo, na ibada kama hiyo kuwa ibada ya mashetani. (Gal. 4:8; 1 Kor. 10:20; Yer. 16:20; Zab. 96:5) Watu wa vijijini wamengoja wakiwatazamia Mashahidi wafe. Lakini wasipokufa, wengi wa watu hao walianza kuisikiliza kweli ya Biblia kutoka kwa Mashahidi nao wamejitenga na utumwa wao wa ushirikina.

Mfano wa uhuru ambao kwa huo kweli imewaweka maelfu ya watu huru na uchawi na ushirikina ni mwanamume anayeitwa Fallah John, aliyekuwa kuhani wa hirizi aliyeongoza jamii ya siri ya mwituni ya Kiafrika. Yeye anasimulia:

“Mimi nilitumia maongozi ya ajabu kati ya wazee wangu na kati ya watu katika vijiji vingi katika eneo kubwa katika jamii yetu. Nilikuwa na uwezo usio wa kawaida wa kupigana na watu hata 25 wakati mmoja. ‘Dawa’ yangu kwa njia fulani ilitengenezwa na sehemu ya mwili wa kibinadamu uliochomwa. Kwa sababu ya uwezo huu wa pekee niliopewa na mashetani nilipenda sana kupigana nami niliheshimiwa, hata hivyo kuogopwa, na wenzangu wa kabila langu. Mashahidi wa Yehova walipokuja na ujumbe wa Biblia na kueleza Yehova ni nani nalo kusudi lake ni nini, niliukubali ukaribishaji wao niwe na funzo la Biblia nyumbani mwangu. Nikaja kujua kwamba uwezo wa Yehova ni mkuu zaidi kuupita ule wa Shetani na mashetani zake. Haukupita muda mwingi mbele ya mimi kukata maneno kwamba mahali pa kuwa kuhani wa ibilisi, nilitaka kumtumikia Yehova na kupata nguvu zake.”

Fallah John sasa anatumikia kama mhudumu painia wa wakati wote wa mashahidi wa Yehova. Sasa yeye ni mfanya amani.

Leo watu wengi wanaona kushindwa kwa dini za ulimwengu huu na filosofia. Wao wanatafuta kwa bidii jambo fulani linalowapa tumaini imara. Mashahidi wa Yehova wamefanya utafutaji huo, nao wamepata jambo hakika la kuamini. Wao wanafurahia mashirika ambamo wanatakiwa na kupendwa. Watu wa nje, wanaoyatazama makusanyiko yao ya mahali pao na ya mataifa yote, wamesifu amani, umoja na udugu wa Mashahidi kwa maana, wao wanakusanyika na kufanya kazi pamoja wakiwa wametoka katika mataifa yote na hali za maisha. Mmoja aliyetembelea kusanyiko katika North Carolina, kwa kuona “kadiri ya juu zaidi ya mchanganyiko wa mataifa kuliko vikundi vilivyo vingi zaidi vya kidini,” aliandika: “Shughuli ya ‘ndugu na dada’ siyo ya kusingizia.” “Wao wanamshuhudia mungu mwenye furaha,” alisema mwandikaji wa Journal, la Shreveport, Louisiana. Naye msimamizi wa habari wa Atlanta, Georgia, kituo cha radio alimalizia: “Si kwamba tu vijana wenu wanayo majibu juu ya Biblia, lakini vile vile wanayo majibu juu ya ugumu wa dawa za kulevya.”

Mashahidi wa Yehova wamekipata kile ambacho maelfu ya vijana waliofumbuliwa macho wanatafuta kweli. Kwa sababu gani usilitembelee Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova katika mtaa wako, ukajionee mwenyewe? Utakaribishwa kwa uchangamfu, na haitakulazimu kufanya lo lote isipokuwa kuyasikiliza mazungumzo yenye kuelimisha na yenye kujenga ya mambo yanayoongoza kwenye uzima na amani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki