Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 5 uku. 18-uku. 19 fu. 5
  • Safina ya Noa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Safina ya Noa
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Nuhu Anajenga Safina
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Gharika Kubwa​—Nani Alimsikiliza Mungu? Nani Hakumsikiliza?
    Msikilize Mungu Uishi Milele
  • Maji Yachukua Ulimwengu
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 5 uku. 18-uku. 19 fu. 5
Noa na familia yake wakijenga safina

SOMO LA 5

Safina ya Noa

Watu walizidi kuongezeka duniani na wengi walikuwa wakifanya mambo mabaya. Hata baadhi ya malaika wa mbinguni wakawa wabaya. Waliacha makao yao huko mbinguni na kuja duniani. Je, unajua ni kwa nini walifanya hivyo? Ili wavae miili ya wanadamu na kujichukulia wanawake.

Malaika walijichukulia wanawake na kuzaa watoto. Watoto hao walikuwa watu wenye nguvu sana na wajeuri. Waliwapiga watu. Yehova hangeruhusu hali hiyo iendelee. Hivyo, aliamua kuwaharibu watu wabaya kupitia gharika.

Noa na familia yake wakijenga safina na kuandaa chakula

Lakini kulikuwa na mtu mmoja aliyekuwa tofauti na watu hao. Alimpenda Yehova. Jina lake ni Noa. Alikuwa na mke na watoto watatu, yaani, Shemu, Hamu, na Yafethi, na kila mtoto alikuwa na mke. Yehova alimwambia Noa wajenge safina, ili yeye na familia yake waokoke Gharika. Safina ilikuwa sanduku kubwa lililoelea majini. Pia, Yehova alimwambia Noa awaingize wanyama ndani ya safina ili wao pia waokoke.

Mara moja, Noa alianza kujenga safina. Noa na familia yake walijenga safina kwa karibu miaka 50. Walijenga safina kulingana na maagizo ya Yehova. Katika kipindi hicho, Noa aliwaonya watu kuhusu Gharika. Lakini hakuna mtu aliyemsikiliza.

Hatimaye, muda wa kuingia ndani ya safina ukafika. Acha tuone kile kilichotokea baadaye.

“Kama siku za Noa zilivyokuwa, ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.”​—Mathayo 24:37

Maswali: Kwa nini Yehova alileta Gharika? Yehova alimpa Noa maagizo gani?

Mwanzo 6:1-22; Mathayo 24:37-41; 2 Petro 2:5; Yuda 6

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki