Wimbo 35
Njia ya Upendo Ipitayo Zote
1. Mungu upendo, kwa hiyo
Hutaka tuwe hivyo,
Kwa Mungu, jirani, pendo
Litutie bidii.
Kuwe imani, ujuzi,
Lugha na unabii,
Pendo likikosekana
Tu bure, hatufai.
2. Tujapohubiri sana,
Na kuteswa vibaya;
Ingetufaidi nini
Ikiwa nia mbaya?
Pendo lafadhili sana,
Si la adabu mbaya,
Si la kiburi na wivu,
Busara latumia.
3. Pendo si kali, si chungu,
Mabaya lachukia.
Linavumilia sana,
Haki lafurahia.
Imani, pendo, vyadumu
Tukihudumu Mungu;
Njia ipitayo zote
Ni pendo la kimungu.