Wimbo 150
Mkate Kutoka Mbinguni
1. Baba wa mbingu juu,
U yule yule daima,
Twaimba sifa zako
Twatakasa jina lako.
Kale ulitumia
Pendo kuongoza,
Watu kama kondoo,
Ukawapa mana.
Na kiu wakazima
Kwa maji kutoka mwamba.
’Kawaleta Kana’ni
Ni kundi lenye furaha.
2. Mana uliwalisha
Ni mufano wa Mwanako.
Kaacha utukufu
Watu wakaokolewe.
Ndiye ule mukate;
Mwili akatoa,
Kwa wale watu wote,
Wokovu wapate.
Mukate tu ambao
Mungu aweza kutoa;
Na tule kila siku,
Na kuishi kwa usafi.
3. Watu wasizuiwe
Mukate hata kidogo,
Bali, na tuwalishe
“Kondoo” za Kristo Yesu.
Saidia wengine
Watafute haki,
Waje waokolewe,
A’bariki Mungu.
Na baada ya vita
Kuu ya Har–Magedoni,
Tutamusifu Mungu,
Shangwe kwa matendo yake.