Fedha za Kuendesha Kazi Yao Zinatokana na Michango ya Kujitolea
Utendaji wote uliotangulia kusimuliwa unategemezwa na wafanyi kazi wa kujitolea, kwa njia hiyo gharama zinapunguzwa. Huduma ya nyumba kwa nyumba na ugawaji wa vitabu unafanywa na Mashahidi wa Yehova kwa kujitolea. Wanajilipia gharama zao wenyewe. Wazee wanaosimamia makundi, wakisaidiwa na watumishi wa huduma, hawapokei mshahara kwa utumishi wao. Wanajilipia wenyewe gharama.
Hata washiriki wa Baraza Linaloongoza na wengine wote wanaofanya kazi wakati wote katika kutayarisha na kufanyiza Biblia na vitabu vya Biblia wanapokea tu chumba chao na chakula na rudishio kidogo la gharama. Vivyo hivyo na waangalizi wasafirio wa wakati wote.
Michango midogo inayopokewa kwa vitabu kwa sehemu kubwa inalipia tu gharama za msingi za vifaa, uchapaji, na usafirishaji. Gharama nyingine zote zinalipiwa kwa michango ya kujitolea ya fedha inayofanywa na Mashahidi wa Yehova wenyewe, kupitia upaji au usia halali.
Kwenye mikutano yote ya Mashahidi wa Yehova, iwe ni mahali walipo au kwenye makusanyiko, kuna visanduku vya michango vinavyopatikana kwa wale wanaotaka kutoa michango. Hakuna sadaka zinazochukuliwa. Hakuna kodi wala zaka zinazolipwa. Kama ilivyoandikwa katika Maandiko, kila mmoja aweza kuchanga kama alivyoazimu katika moyo wake.—2 Wakorintho 8:12; 9:7.
• Utendaji wote wa Mashahidi wa Yehova unategemezwaje kifedha?