Sura 8
Kuishiriki “Furaha” ya “Mwana-Mfalme wa Amani”
1. (a) Ni kwa sababu gani mtu fulani alisafiri kwenda ng’ambo? (b) Ni jambo gani linalodokezwa katika mfano wa Yesu, ijapokuwa halikutajwa waziwazi?
KATIKA mfano wa Yesu wa zile talanta, yule mtu aliyekuwa na zile talanta nane za fedha hakusafiri kwenda ng’ambo kwa ajili ya anasa tu kama vile kusafiri akajionee mambo. Yeye alikuwa na sababu nzito ya kusafiri kwenda ng’ambo; alitamani kujipatia kitu chenye thamani. Kama vile mfano huo unavyoonyesha, yeye alisafiri kwenda ng’ambo akajipatie “furaha,” pamoja na mambo “mengi.” (Mathayo 25:21) Hivyo, yeye alilazimika kusafiri mwendo mrefu, ukihitaji wakati mrefu, ili akafanye ombi kwa yule ambaye angeweza kumpatia furaha iyo hiyo.
2. (a) Kwa habari ya Yesu, safari ya kwenda ng’ambo ya yule mtu tajiri ilifananisha nini, na alikwenda kwa nani? (b) Bwana-Mkubwa alirudi akiwa na nini?
2 Kwa kuwa yule mtu tajiri katika huo mfano anafananisha Yesu Kristo, kusafiri kwa mtu huyo kwenda ng’ambo kwa safari ndefu kunafananisha Yesu akienda kwenye Chanzo cha ile furaha ya pekee aliyokuwa akitazamia. Kwa hiyo, yeye alienda kwa nani? Waebrania 12:2 hutuambia: “Tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili [mti wa mateso] na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.” Ndiyo, kweli kweli, Yehova Mungu ndiye Chanzo cha furaha hiyo. Ni kwake alikokwenda Yesu, akaacha wanafunzi wake waaminifu hapa duniani wakiwa wamekabidhiwa “talanta” zake. Yule Bwana-Mkubwa alirudi akiwa na mambo “mengi” ambayo hakuwa nayo wakati alipokabidhi watumwa wake watatu zile talanta nane za fedha. Mfano wa mapema uliotolewa na Yesu, ule mfano wa “mafungu kumi ya fedha,” unaonyesha waziwazi kwamba kile alichorudi nacho kilikuwa ni “ufalme.”—Luka 19:12-15.
3. Ulikuwa wakati wa namna gani unabii wa Zekaria 9:9 ulipoanza kutimizwa katika karne ya kwanza W.K.?
3 Akiwa ametawazwa tu, mfalme ana sababu ya kufurahi, na ndivyo na raia zake washikamanifu. Tunakumbuka pindi ile Mwana wa Mungu alipopanda kwenda Yerusalemu kutimiza unabii wa Zekaria 9:9. Kwa habari ya utimizo wa unabii huo imeandikwa hivi: “Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani. Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la [Yehova]; Hosana juu mbinguni. Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?”—Mathayo 21:4-10; ona pia Luka 19:36-38.
4. Baada ya kutawazwa akiwa Mfalme, ni kwa sababu gani Yesu Kristo alikuwa na msingi wa pekee wa kualika “watumwa” wake waaminifu kwenye hali yenye furaha?
4 Basi, ikiwa, ilikuwa pindi yenye furaha alipojitoa tu mwenyewe kwa wakazi wa Yerusalemu, akiwa ndiye mpakwa-mafuta kwa roho ya Yehova kwa ajili ya umaliki, ilikuwa hivyo kwa kadiri kubwa jinsi gani zaidi alipotawazwa kweli kweli awe Mfalme mwishoni mwa Nyakati za Mataifa mwaka wa 1914? Ilikuwa pindi yenye furaha sana kwake. Ndipo, kweli kweli, alipoingia katika furaha asiyopata kuwa nayo kamwe wakati uliotangulia. Kwa hiyo wakati wa kufanya hesabu, angeweza kuwaambia wale wanafunzi ambao aliwahukumu kuwa ‘wema na waaminifu’ hivi: “Ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” (Mathayo 25:21) Sasa kukawa na furaha mpya ambayo katika hiyo “watumwa” wake waliokubaliwa wangeweza kushiriki. Ni thawabu iliyoje!
5. (a) Mtume Paulo alikuwa ‘balozi’ kwa ajili ya Kristo wakati hali ya mambo ilikuwaje? (b) Lakini leo mabaki ya wapakwa mafuta ni “mabalozi” kwa ajili ya Kristo baada ya matukio gani?
5 Mwaka wa 1919 wanafunzi waliopakwa mafuta wa Mfalme anayetawala, Yesu Kristo, waliingia katika hali inayokubaliwa, nayo ilifuatana na furaha kuu kwa upande wao. Karne kumi na tisa mapema mtume Paulo aliwaandikia waamini wenzake kuwaambia juu ya cheo chao kilichotukuka: “Kwa hiyo sisi tu mabalozi badala ya Kristo.” (2 Wakorintho 5:20, NW) Hilo liliandikwa wakati Yesu alikuwa angali mrithi tu akionekana kuwa na tazamio la kuupokea ule “ufalme wa mbinguni.” (Mathayo 25:1) Kwa hiyo, basi, yeye alihitaji kuketi katika mkono wa kuume wa Mungu angojee hapo ile siku ya kuanza kutawala. Lakini sasa, tangu 1919, wale mabaki waliokubaliwa wamekuwa “mabalozi” waliopelekwa na Yule Mfalme ambaye kwa kweli anatawala. (Waebrania 10:12, 13) Fikira za Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa sana sana zilivutwa kwenye uhakika huo wakati wa mkusanyiko huko Seda Pointi, Ohaiyo, mwaka wa 1922.
6. Jitihada za baada ya vita za wale waliokuwa wamepokea zile “talanta” zilielekezwa kwanza kwa kazi ya namna gani?
6 Mwaka wa 1919 walikuwa wamekwisha kabidhiwa kile kilicholingana na zile “talanta” za Mfalme anayetawala Yesu Kristo. Hilo lilikuwa limezidisha kule kutozwa hesabu na Mfalme anayetawala. Tangu mwanzo, jitihada zao za baada ya vita zilielekezwa kwenye kazi ya “mavuno,” kule kukusanywa kwa ile iliyokuwa jamii ya “ngano.” (Mathayo 13:24-30, NW) Kwa kuwa, kama vile Yesu alivyosema, mavuno ni “umalizio wa mfumo wa mambo,” ule mwaka wa baada ya vita wa 1919 ndio uliokuwa wakati wa kuanza kuvuna wale “wana wa ufalme” wenye mfano wa ngano, wale mabaki waliopakwa mafuta waaminifu.—Mathayo 13:37-39.
7. (a) Wale wavunaji waliingia katika wakati wa namna gani pamoja na Bwana-Mkubwa wao? (b) Yehova amewaleta wavunaji kwenye hali gani, na ni maneno gani ya kiunabii wanayochukua?
7 Wakati wa mavuno ni wakati wa furaha kwa wavunaji, kwa kuwa Bwana-Mkubwa wa mavuno anafurahia pindi hiyo pamoja nao. (Zaburi 126:6) Wakati huu wa mavuno umetajirishwa sana na ushuhuda unaoongezeka kwamba Ufalme wa Mungu mikononi mwa Yesu Kristo ulisimamishwa mbinguni mwaka wa 1914 na kwamba Yehova amewarudishia watu wake walio wakfu hapa duniani msimamo wa uadilifu. Kama jamii, wanayachukua maneno ya Isaya 61:10: “Nitafurahi sana katika [Yehova], nafsi yangu itashangilia katika Mungu wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la [uadilifu].”
Kukusanya “Mkutano Mkubwa” wa Washiriki wa Ile “Furaha”
8. Ni furaha gani ambayo haikutazamiwa na mabaki ya wapakwa mafuta ambayo ingekuwa fungu lao wakiisha kumaliza kukusanya warithi wa Ufalme?
8 Yale mabaki ya wapakwa mafuta yaliyoingia katika “furaha” ya Bwana-Mkubwa wao hayakujua hata kidogo kwamba karibu na mwisho wa kukusanywa kwa washiriki wale wa mwisho wa warithi wa Ufalme wa kimbingu kungekuwako na furaha nyingine, jambo lisilotazamiwa. Hiyo ingekuwa ni kule kukusanywa kwa jamii ya kidunia ambayo ingeishi katika dunia-Paradiso chini ya Utawala wa Mileani wa Yesu Kristo. Ni nani wengine isipokuwa watu kutoka jamii hii ya kidunia wangefaa kualikwa kwenye ile ambayo ingekuwa ndiyo habari ya kwanza kufunuliwa kuhusu wao?
9. Ni nani hasa walioalikwa wahudhurie mkusanyiko wa mwaka 1935 huko Washington, D.C., na ni habari gani ya wakati unaofaa waliyofunuliwa huko?
9 Basi ikawa kwamba, katika kuitikia mwaliko uliochapishwa katika Mnara wa Mlinzi,a mamia waliokuwa wakitafuta uhusiano na Yehova, pamoja na watu wa jina lake, walihudhuria mkusanyiko wa watu wote wa Mashahidi wa Yehova huko Washington, D.C., Mei 30 mpaka Juni 2, 1935. Kwenye mkusanyiko huo, walichochewa mpaka kwenye vina vya mioyo yao kupata kujua kwamba kumbe “ule mkutano mkubwa” uliotangulia kuonwa katika Ufunuo 7:9-17 ulikuwa uwe jamii ya kidunia.
10, 11. Huu ulipaswa uwe wakati wa furaha ya pekee kwa nani huko mbinguni?
10 Ni lazima iwe ilikuwa furaha kubwa kama nini kwa Yehova Mungu Aliye Juu Zaidi mkusanyiko huo kufanyika katika Washington, D.C.! Ni lazima iwe ilikuwa furaha kuu kama nini pia kwa Mwanaye akiwa ndiye Mchungaji Mwema ambaye sasa angeanza kukusanya hawa “kondoo wengine” katika lile “kundi moja”!—Yohana 10:16.
11 Wanapokuwa wakiongozwa na kulishwa, kwa njia ya mfano, wale washiriki wa mabaki na ule “mkutano mkubwa” unaoendelea kuongezeka wa “kondoo wengine” wanachangamana pamoja kwa amani na kwa upendo. Moyo wa “mchungaji mmoja” wao ni lazima sasa ufurike furaha ya kuwa na “kundi” kubwa namna hiyo karibu na mwisho wa huu “umalizio wa mfumo wa mambo.”
Wajumbe wa “Mwana-Mfalme wa Amani”
12, 13. (a) Ni nani wamealikwa kushiriki pamoja na mabaki ya wapakwa mafuta furaha ya Bwana-Mkubwa aliyerudi, na ni nini sababu ya hilo? (b) Ule “mkutano mkubwa” wa “kondoo wengine” wanatumikia faida za “Mwana-Mfalme wa Amani” katika cheo gani?
12 Hawa wenye mfano wa kondoo wanaokuwa ule “mkutano mkubwa” sasa wanashiriki sehemu kubwa katika furaha ya Bwana-Mkubwa, Yesu Kristo. Sana sana hii ni kwa sababu ya kuwa washiriki watendaji katika kuwaleta wale wanaohitajiwa ili kukamilisha ule “mkutano mkubwa” ambao hakuna hesabu iliyotolewa katika Ufunuo 7:9.
13 Ile kazi ya kukusanya ambayo katika hiyo “kondoo wengine” wanashiriki imepanuka kadiri ya kuenea ulimwenguni pote, kupita sana ambavyo hesabu ya mabaki wapakwa mafuta inayoendelea kupunguka iwezavyo kushughulikia. Kwa hiyo, hesabu inayoendelea kuongezeka ya “kondoo wengine” imeendelea kulazimika kushiriki sehemu kubwa hata zaidi katika kuwaleta wengi zaidi wa wale “kondoo wengine” wenye tumaini la kidunia. Kwa njia hiyo “kondoo wengine” wanatumika wakiwa wajumbe waaminifu wa “Mwana-Mfalme wa Amani.” Mithali 25:13 inaongeza hivi: “Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno; ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwao wamtumao; kwa maana huwaburudisha bwana zake nafsi zao.”
14. (a) Wale kondoo wa mfano wa ule mfano wa Yesu kwenye Mathayo 25:31-46 wanarithi nini? (b) Ufalme umewekwaje tayari kwa ajili yao “tangu [kuwekwa msingi wa] ulimwengu”?
14 Katika ule mfano wa kondoo na mbuzi, kondoo wa mfano ndio wanaoambiwa na Mfalme Yesu Kristo hivi: “Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme mliowekewa tayari tangu [kuwekwa msingi wa] ulimwengu.” (Mathayo 25:31-46) Wanarithi eneo la kidunia ambalo juu yalo Ufalme wa mbinguni utatawala wakati wa utawala wa Kristo wa Mileani. Tangu wakati wa Abeli mwaminifu, Yehova amekuwa akitayarisha eneo hili kwa ajili ya ulimwengu wa wanadamu wenye kukomboleka.—Luka 11:50, 51.
15, 16. (a) Ni “pambo” gani la mfalme, kama linavyotajwa na Sulemani, alilo nalo Bwana-Mkubwa leo ijapokuwa utawala wake katikati ya maadui wake? (b) Mfalme anayetawala ana “pambo” hilo leo likiwa la namna gani? (c) Wale wanaokuwa ndio “pambo” hilo wamefanya nini?
15 Mfalme Sulemani mwenye hekima wa Israeli wa kale aliandika: “Katika halaiki ya watu mna pambo la mfalme.” (Mithali 14:28, NW) Yule Bwana-Mkubwa wa kifalme wa leo, Kristo Yesu, ambaye ni afisa aliye juu zaidi ya Mfalme Sulemani wa kidunia, ana “pambo” kama hilo kwa habari ya “halaiki ya watu.” Ndivyo ilivyo hata sasa kabla ya kuanza kwa utawala wake wa miaka elfu, ndiyo, wakati yeye anapotawala katikati ya maadui wake wa kidunia, ambao juu yao Shetani Ibilisi ndiye mfalme asiyeonekana mwenye uwezo upitao wa kibinadamu.—Mathayo 4:8, 9; Luka 4:5, 6.
16 “Pambo la” leo linalomfaa afisa aliye na cheo cha mfalme lapatikana sasa katika hesabu inayoongezeka ya “kondoo wengine” wake ambao ndio “mkutano mkubwa.” Kwa shangwe, wanalia kwa sauti yenye umoja hivi: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.” (Ufunuo 7:9, 10) Tayari wao wamepata wokovu kutokana na mfumo huu wa mambo uliohukumiwa maangamizi ambao Shetani Ibilisi ndiye “mungu” wao. (2 Wakorintho 4:4) Tayari wao, kwa njia ya mfano, “wamefua mavazi yao . . . katika damu ya Mwana-Kondoo” na kuyafanya meupe ili waonekane bila doa mbele za Yehova Mungu, aliye Hakimu.—Ufunuo 7:14.
17. (a) Wale wa “mkutano mkubwa” wangali wanatazama mbele kwenye wokovu gani? (b) Watafurahia pendeleo gani wakati wa Utawala wa Mileani wa “Mwana-Mfalme wa Amani”?
17 Hata hivyo wanatazama mbele kwenye wokovu ulioandaliwa kimungu ambao watapata wakati wa upeo wa ushindi wa Yehova katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har–Magedoni. Ushindi wake wenye utukufu wakati huo utakuwa na matokeo ya kuondolea malawama enzi yake kuu ya ulimwengu wote, nao watakuwa ndio mashahidi wa kidunia wenye kujionea kwa macho yao wenyewe kwa sababu watahifadhiwa hai waupite mwisho huo mbaya sana wa huu ulimwengu mbovu. (Ufunuo 16:14; 2 Petro 3:12) Ni pendeleo lenye thamani kama nini! Ni furaha kuu kama nini ambayo “Mwana-Mfalme wa Amani” atashiriki wakati huo pamoja na “mkutano mkubwa” utakaookolewa wa “kondoo wengine” wake wenye ushikamanifu!
[Maelezo ya Chini]
a Ukurasa 2 wa Mnara wa Mlinzi wa matoleo ya Kiingereza ya Aprili 1 na 15, Mei 1 na 15, 1935.
[Picha katika ukurasa wa 71]
Ni lazima sasa moyo wa Mchungaji Mwema uwe unajaa furaha kwa kuwa na “kondoo wengine” wengi sana