Kubaki Tukiwa Tumejipanga Kitengenezo Ili Tuokoke Kuingia Katika Mileani
“Kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.”—YOHANA 10:16.
1. Kwa Mungu aliye hai sikuzote, miaka elfu ni kama nini?
YEHOVA ndiye Muumba wa wakati kwa aina ya binadamu. Na kwake, Mungu asiyeweza kufa wa kutoka milele mpaka milele, miaka elfu ni kama siku yenye kupita upesi au hata zamu moja tu ya ulinzi katika vipindi vyetu vya usiku.—Zaburi 90:4; 2 Petro 3:8.
2. Ni kipindi gani ambacho Yehova ameweka kando kwa ajili ya kubariki aina yote ya binadamu?
2 Mungu ameweka siku ya mfano ya miaka elfu ambayo katika hiyo atabariki jamii zote za dunia. (Mwanzo 12:3; 22:17, 18; Matendo 17:31) Hii inatia ndani wale ambao ni wafu sasa na wale ambao wangali hai. Mungu atafanyaje hivyo? Basi, kupitia Ufalme Wake katika Yesu Kristo, ile “mbegu” ya mke Wake wa mfano!—Mwanzo 3:15.
3. (a) Kisigino cha Mbegu ya mwanamke wa Mungu kilichubuliwaje, na kidonda hicho kiliponaje? (b) Mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu ya Yesu Kristo, yeye atafanya nini kwa nyoka wa mfano?
3 Kisigino cha mfano cha Mbegu ya mwanamke wa Mungu (au tengenezo la kimbingu) kilichubuliwa wakati Yesu Kristo alipopatwa na kifo cha mfia imani na akabaki akiwa mfu kwa sehemu za siku tatu katika mwaka wa 33 wa Wakati wa Kawaida wetu. Lakini siku ya tatu, Mungu Mweza Yote, Mpaji-Uhai Mkubwa, aliponya kidonda hicho kwa kumfufua Mwana wake mshikamanifu kwa uhai wa kutokufa katika makao ya kimbingu. (1 Petro 3:18) Kwa kuwa Yesu hatakufa tena, yeye yumo katika hali ya kutawala akiwa Mfalme juu ya aina ya binadamu kwa miaka elfu na ‘kuchubua’ kichwa cha nyoka wa mfano, akimponda-ponda na kumwondolea mbali baada ya mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu. Hiyo itakuwa baraka iliyoje kwa aina ya binadamu waliorudishwa wenye uaminifu!
4. Ni programu ya aina gani ambayo Mungu amekuwa akitekeleza pamoja na watu wake?
4 Kadiri kubwa ya kupanga mambo kitengenezo kumekuwa kukiendelea miongoni mwa watu wa Yehova duniani pote wakati wa huu “umalizio wa mfumo wa mambo” tangu Nyakati za Mataifa zilipomalizika katika 1914. (Mathayo 24:3; Luka 21:24, King James Version) Programu hii ya kitengenezo inayotangulia Mileani inaendelezwa kupatana na penzi la Mtengeneza Mambo Mkubwa, Yehova Mungu, na chini ya mwongozo Wake. Kupitia mwanamke wake, tengenezo lake la kimbingu lililo kama mke, uzawa wa Ufalme wake ulioahidiwa kupitia Yesu Kristo ulitukia katika 1914, kama inavyothibitishwa na utimizo wa unabii wa Biblia.
5. Ni uzawa wa nini uliotabiriwa kwenye Ufunuo 12:5, na huo ulielezwa mara ya kwanza wakati gani katika Mnara wa Mlinzi?
5 Hivyo maneno ya Ufunuo 12:5, NW yametimizwa kwa utukufu: “Na yeye akazaa mwana, wa kiume, ambaye apaswa kuchunga mataifa yote kwa ufito wa chuma. Na mtoto wake akadakwa mbali hadi kwa Mungu na kwenye kiti cha ufalme chake.” Uzawa wa Ufalme wa Yehova, ulielezwa kwanza katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Machi 1, 1925. Uzawa wa Ufalme huu wa Kimesiya katika mbingu katika 1914 unatofautiana na uzawa wa “taifa” la ‘watoto’ wa Sayuni duniani katika 1919.—Isaya 66:7, 8.
6. (a) Uzawa wa Ufalme ulitaka kazi gani iliyotabiriwa na Yesu? (b) Kufanya kazi hii kulitaka nini kwa upande wa watu wa Yehova, na ni kabiliano la namna gani wanalotokeza sasa?
6 Uzawa wa Ufalme wa Yehova ambao kupitia kwao atatetea uhaki wake wa enzi kuu juu ya ulimwengu wote mzima—aha, hapa kukawa na jambo fulani lililostahili kutangazwa duniani pote! Na hapa kukawa na wakati wa kutimiza maneno haya ya Yesu kuhusu uthibitisho wa “kuwapo” kwake kusikoonekana: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:3, 14, NW) Kuhubiri kwa umoja na upatani duniani pote hakika kungetaka kupanga kitengenezo sehemu ionekanayo ya tengenezo la Yehova la ulimwengu wote mzima. Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti, kama ilivyowakilishwa na msimamizi wayo wa wakati huo, J. F. Rutherford, ilipendelea kufanya hivyo. Kwa hiyo kuanzia mwaka wa 1919 baada ya vita, kupangwa kitengenezo kwa waunga mkono washikamanifu wa Sosaiti wakiwa taifa lililorudishwa kuliendelea mbele kwa kupiga moyo konde, pamoja na sala ya mwongozo na baraka ya Mtengeneza Mambo Mkuu Zaidi, Yehova Mungu. Wajapopatwa na upinzani mkali wa Wafashisti, harakati ya Nazi ya Hitler, Aksio ya Wakatoliki na kukabiliwa na Vita ya Ulimwengu 2, Mashahidi wa Yehova duniani pote walielekeana na ulimwengu wenye uadui wakiwa na umoja.
7. (a) Ni kwa kubaki tu katika uhusiano gani mmoja na mwenzake ndipo watu wa Yehova wanaweza kutazamia kuokoka dhiki kubwa? (b) Waokokaji wa Gharika walipitaje Gharika ya tufe lote, nao walitangulia kufananisha nani?
7 Mashahidi wa Yehova peke yao, wale wa mabaki wapakwa-mafuta na “umati mkubwa,” wakiwa tengenezo lenye umoja chini ya ulinzi wa Mtengeneza Mambo Mkuu Zaidi, ndio wenye tumaini lolote la Kimaandiko la kuokoka mwisho unaokaribia wa mfumo huu unaotawalwa na Shetani Ibilisi ambao umehukumiwa maangamizi. (Ufunuo 7:9-17; 2 Wakorintho 4:4, NW) Wao watafanyiza “mnofu” ambao Yesu Kristo alisema ungeokolewa kupita dhiki mbaya sana katika historia ya binadamu. Kama ilivyokuwa katika siku za Noa, akasema Yesu, ndivyo itakavyokuwa katika siku ile ambayo Yeye angefunuliwa. Nafsi nane tu za kibinadamu ndizo zilizookoka Gharika ya tufe lote zikiwa ndani ya safina iliyochukua miaka mingi ya jitihada iliyopangwa kitengenezo ili kuimaliza. Waliokoka wakiwa kikundi cha jamaa chenye umoja. (Mathayo 24:22, 37-39; Luka 17:26-30) Mke wa Noa analingana na bibi-arusi wa Kristo, na wana wake na binti wakweze wanalingana na “kondoo wengine” wa Yesu wa kisasa, ambao wamekua wakawa umati mkubwa unaoongezeka, ambao sasa hatujui utakuwa na ukubwa gani mwishowe. (Yohana 10:16) Ili kuokoka kuingia Mileani chini ya Noa Mkubwa Zaidi, Yesu Kristo, wanahitaji kubaki wakiwa wamepangwa kitengenezo pamoja na mabaki wapakwa-mafuta, “wateule” ambao kwa habari yao zile siku za “dhiki kubwa” zitapunguzwa.—Mathayo 24:21, 22.
Kuokoka Kuingia Katika Mileani
8. Kwa kufunga unabii wake kuhusu kuwapo kwake, Yesu alitoa kielezi gani, nayo tarehe ya Juni 1, 1935, ilikuwaje ya maana kwa habari ya kukielewa?
8 Kulingana na Gospeli ya Mathayo, Yesu alifunga unabii wake kuhusu ishara ya kuwapo kwake kwa kielezi. Kielezi hicho ambacho kwa kawaida huitwa mfano wa kondoo na mbuzi, kinahusika sasa, wakati wa umalizio wa mfumo huu wa mambo, ulioanza mwishoni mwa Nyakati za Wasio Wayahudi katika 1914. (Mathayo 25:31-46) Tarehe ya Jumamosi, Juni 1, 1935, ilikuwa ya maana kwa habari ya kuelewa utambulishi wa kondoo kuwa washiriki wa umati mkubwa. Siku hiyo, kwenye mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C., watu mmoja mmoja 840 walibatizwa kuonyesha wakfu wao [ ] kwa Yehova Mungu kupitia Yesu Kristo. Walio wengi wa hao walichukua hatua hii kwa kuuitikia haraka mhadhara uliotolewa na J. F. Rutherford juu ya Ufunuo 7:9-17. Ilikuwa tamaa yao kuwa sehemu ya umati mkubwa wa kondoo wengine wa Mchungaji Mwema, wakiwa na fursa ya kuokoka dhiki kubwa inayokuja na kuwa hai kuupita mwisho wa mfumo huu wa mambo na kuingia katika Utawala wa Mileani wa Mchungaji-Mfalme, Yesu Kristo. Hatimaye, wanafikia uhai wa milele katika dunia paradiso.—Mathayo 25:46; Luka 23:43.
9. Kwa nini kondoo wanaalikwa warithi ‘ufalme waliowekewa tayari,’ na ni kwa njia gani wamo katika hali nzuri zaidi kuwatendea mema ndugu za Mfalme?
9 Kwa nini watu hawa wa aina ya kondoo waalikwa ‘waurithi ufalme waliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu’? Mfalme awaambia kwamba ni kwa sababu wamewatendea “ndugu” zake mema, na kwa sababu hiyo walimtendea yeye. Kwa usemi “ndugu,” Mfalme anamaanisha mabaki wa ndugu zake wa kiroho ambao wangali duniani katika umalizio huu wa mfumo wa mambo. Wakiisha kuwa kundi moja na akina ndugu wa Mchungaji-Mfalme, Yesu Kristo, wangeshirikiana kwa ukaribu sana iwezekanavyo pamoja na mabaki wa hao na kwa hiyo wangekuwa katika hali nzuri kabisa ya kuwatendea mema. Hata katika njia za kimwili, wangewasaidia ndugu za Yesu kuhubiri ulimwenguni pote ujumbe wa Ufalme uliosimamishwa kabla mwisho haujaja. Kwa sababu hii, kondoo wangehazini pendeleo lao la kuwa wamepangwa kitengenezo pamoja na mabaki wakiwa kundi moja la Mchungaji mmoja.
10. Inamaanisha nini kwa kondoo ‘kurithi ufalme waliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu’?
10 Kurithi ‘ufalme waliowekewa tayari’ hakumaanishi kwamba kondoo hawa watatawala pamoja na Yesu Kristo na ndugu zake mbinguni kwa miaka elfu. Bali, tangu mwanzo wa Mileani, kondoo watarithi milki ya kidunia ya Ufalme. Kwa kuwa wao ni wazao wa Adamu na Hawa, milki hii ya kidunia ambayo Ufalme wa Mungu kupitia Kristo utatawala ilitayarishwa kwa ajili yao “tangu kuumbwa ulimwengu” kwa aina ya binadamu waliokombolewa. Zaidi ya hilo, kwa kuwa kondoo wanakuja kuwa watoto wa kidunia wa Mfalme, ambaye anakuwa “Baba wa milele” wao, wanarithi milki ya kidunia, au makao, chini ya Ufalme wa Mungu.—Isaya 9:6, 7.
11. Kondoo wanaonyeshaje kwamba wao wanatetea Ufalme, na kwa sababu ya hilo, ni baraka gani ambayo ni yao?
11 Kwa kutofautiana na mbuzi wa mfano, watu wa aina ya kondoo wanaonyesha kwamba wanatetea Ufalme waziwazi. Jinsi gani? Kwa vitendo, si maneno matupu tu. Kwa sababu ya kutoonekana kwa Mfalme katika mbingu, hawawezi kumtendea mema moja kwa moja kwa kuunga mkono Ufalme wake. Kwa hiyo wanawatendea mema ndugu zake wa kiroho ambao bado wako duniani. Ijapokuwa hilo linatokeza chuki, upinzani, na mnyanyaso kutoka kwa mbuzi, kwa sababu ya huko kutenda mema, kondoo wanaambiwa na Mfalme kwamba ndio ‘waliobarikiwa na Baba yake.’
12. Kondoo watakaookoka watakuwa na pendeleo la kukaribisha nani, na kwa habari hii, ni wazo gani ambalo washiriki wa mabaki wamekuwa nalo?
12 Umati mkubwa wa watenda mema wa aina ya kondoo wa ndugu za kiroho wa Mfalme watabarikiwa kwa pendeleo lenye shangwe la kuokoka kuingia katika Mileani. Hatimaye, watashiriki kuwakaribisha wanadamu wafu walio katika makaburi ya ukumbusho. (Yohana 5:28, 29; 11:23-25) Hawa watakuwa ni kutia ndani wazee waaminifu wa ukoo na wanabii ambao waliteseka na kuvumilia mengi kwa ajili ya kutetea enzi kuu ya Yehova ili waweze ‘kupata ufufuo ulio bora,’ ikiwezekana wa mapema. (Waebrania 11:35) Wanaume na wanawake hao wa imani watakaofufuliwa, ambao wameorodheshwa kwa sehemu katika sura ya 11, watakuwa ni kutia ndani Yohana Mbatizaji. (Mathayo 11:11) Baadhi ya mabaki wapakwa-mafuta fulani wamefikiria juu ya kuokoka na kuendelea kuwa hai mpaka wakati wa kukaribisha waaminifu hao watakaofufuliwa ambao walikufa kabla ya Pentekoste 33 W.K. Je! wapakwa-mafuta watapendelewa hivyo?
13. Kwa nini haingehitajiwa mabaki wawepo ili wawakaribishe na kuwatunza wale watakaofufuliwa duniani?
13 Hiyo haingehitajiwa. Umati mkubwa wa waokokaji wa dhiki watakuwako tayari kwa hesabu ya kutosha ili washughulikie hali hiyo na kuwafanya wafufuliwa hao wafahamiane na “dunia mpya” iliyo chini ya “mbingu mpya.” (2 Petro 3:13, NW) Hata sasa, umati mkubwa unapangwa kitengenezo kwa ajili ya jambo hilo. Leo, wakati hesabu ya ndugu wa kiroho wa Yesu walio duniani inaporipotiwa kuwa chini ya 9,000, waokokaji miongoni mwao wangekuwa wachache sana kwa vyovyote kuweza kushughulikia kazi yote ya kujitayarisha inayoongoza kwenye ule ufufuo wa jumla. (Ezekieli 39:8-16) Hapa basi, ndipo umati mkubwa, ambao hesabu yao inaingia katika mamilioni, watatumika vizuri sana. Na bila shaka pendeleo hilo limewekwa kwa ajili yao.
14. (a) Wengi wa umati mkubwa wanazoezwa kwa ajili ya nini, na kwa nini ni lazima hesabu kubwa yao wachukue madaraka sasa? (b) Ni matukio gani ambayo lazima yatukie karibuni, na ni kazi gani inayowangojea kondoo wengine?
14 Wengi wa umati mkubwa tayari wanazoezwa katika madaraka ya kundi na kupitia programu za kujenga ambazo tengenezo la Mungu linaongoza duniani pote. Na ni jambo lenye kutia moyo kuona wanaume zaidi waliokomaa kiroho wa umati mkubwa wakipewa mgawo wa kuchukua madaraka makubwa zaidi katika tengenezo ambalo sasa Yehova anatendesha kazi duniani. Wapakwa-mafuta wanaobaki wanaendelea kuzidi umri na hawawezi sana kubeba mzigo huo. Ndugu hawa wa Mfalme wanaukaribisha msaada wa kitengenezo wenye upendo ambao wazee wanaostahili kiroho na watumishi wa huduma wa kondoo wengine wanaweza kutoa. Karibuni sana, Babuloni Mkubwa ataondolewa kutoka mandhari ya kidunia. Kisha kama Ufunuo 19:1-8 inavyoonyesha, ndoa ya Mwana-Kondoo na bibi-arusi wake wa wote 144,000 itakamilishwa katika mbingu, wale kondoo wengine, wakiwa dunia mpya chini ya mbingu mpya, watamwakilisha Mfalme katika kuendeleza ile kazi tukufu ya kurudisha hali zinazofaa mpaka dunia yote iwe paradiso inayokaliwa kwa sifa ya Yehova.—Isaya 65:17; linganisha Isaya 61:4-6.
15. Ni mataraja gani ambayo umati mkubwa unatazamia kwa ajili ya Mileani?
15 Wakati wa Utawala wa Kristo wa Mileani, wakati aina ya binadamu wafu walioko mbolewa watakapofufuliwa, umati mkubw, wenye kuokoka utaona shangwe ya kupata mapendeleo makubwa mno na yenye kuhe shimika. Ndipo watakapokuwa wana na ma binti wa Mfalme. Itawezekana kwa wana hao miongoni mwao kuwa na cheo kama cha wana-wafalme, sawa na wana wa Mfalme Daudi walivyokuwa wana-wafalme wakiwa na madaraka mbalimbali.a Hili linatukumbu sha Zaburi 45, iliyotungwa kwa habari ya “mfalme” mpakwa-mafuta wa Yehova.
16. Zaburi 45 imeandikwa kwa nani hasa, na jambo hilo linaweza kuthibitiswaje?
16 Zaburi 45 imeandikwa hasa kwa mfalim gani? Basi, ni kwa Yesu Kristo! Waebranie 1:9 inatumia andiko hilo katika kunukuu Zaburi 45:7, ambayo inasomwa hivi: “Umependa haki, umechukia maasi; kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, mafuta ya shangwe kupita wenzio.” Kwa hiyo ni kwa Yesu Kristo aliyetukuzwa hasa kwamba Zaburi 45:16 inasema: “Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako, utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.”
17. Mfalme, Yesu Kristo, anapendezwa na nini na nani hasa?
17 Kwa haki, Yesu anapendezwa zaidi na wakati wake ujao akiwa Mfalme anayetawala kuliko na wakati wake uliopita. Bila shaka, yeye hasahau kwamba wakati uliopita na hasa mababu wake wa kibinadamu walihusika katika ahadi ya Yehova ya kubariki jamaa zote kupitia Mbegu ya Abrahamu. Lakini sasa anapendezwa sana na wakati ujao ulio karibu kama ulivyokusudiwa na Mfalmemfanyi, Yehova Mungu. Kwa hiyo watoto wa kidunia wa Yesu, hasa wana walio miongoni mwao ambao wanastahili kutumika wakiwa chini yake katika ofisi za wana-wafalme, watachukua mahali penye kupendeza sana —kuliko babu zake wa kidunia.
18. Tafsiri fulani fulani za Zaburi 45:16 zinakaziaje upendezi mkubwa wa Yesu katika wana-wafalme kuliko katika babu zake wa kidunia?
18 Tafsiri mbalimbali za Biblia zinakazia kwamba Yesu ana upendezi mkubwa katika wana-wafalme kuliko katika babu zake. Hivi ndivyo nyingine zinavyotafsiri Zaburi 45:16: “Wana wako watajiingiza mahali pa baba zako, nao watainuka wawe wana-wafalme juu ya bara lote.” (Moffatt) “Mahali pa baba zako wana wako watapachukua; wewe utawafanya wawe wana-wafalme katika bara lote.” (Mstari 17, The New American Bible) “Badala ya baba zako watoto wazaliwa kwako: wewe utawafanya wawe wana-wafalme juu ya dunia yote.”—The Septuagint Version, iliyochapishwa na Samuel Bagster and Sons.
19. Watu fulani wa umati mkubwa sasa wana madaraka gani ya kundi, na huenda Mfalme, Yesu Kristo, akawaweka rasmi kwenye cheo gani wakati wa Utawala wa Miaka Elfu?
19 Kwa furaha yetu kubwa, wanaotazamiwa kuwa wana-wafalme wamo miongoni mwetu. Wanapatikana miongoni mwa kondoo wengine ambao wanasikiliza sauti ya Mchungaji Mwema, Yesu Kristo. Wamekuwa wakisikiliza hasa tangu 1935, wakati Ufunuo 7:9-17 ilipoelezwa kwenye mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika Washington, D.C. Leo, maelfu ya umati mkubwa huu wa kondoo wengine wanatumikia wakiwa wazee, au waangalizi, katika makundi zaidi ya 57,670 ya Mashahidi wa Yehova katika mabara 212 kuzunguka ulimwengu. Kwa kubaki wakiwa wamepangwa kitengenezo pamoja na mabaki wa ndugu za kiroho wa Yesu ambao wangali duniani, wanaume hawa wanakuwa katika mstari wa kuchukuliwa kikamili wawe wana wa kimalezi duniani wa Mfalme, Yesu Kristo, wakati wa Utawala wake wa Miaka Elfu juu ya dunia mpya iliyoahidiwa. (2 Petro 3:13) Wakiwa hivyo, wanaweza kuwekwa rasmi kuwa wana-wafalme watumikie katika dunia mpya.
20. (a) Mfalme atakuwa na mtazamo gani kuelekea watu atakaowaweka rasmi duniani? (b) Umati mkubwa utakaribisha nani wenye kurudi, na ni fursa gani ambayo imewekwa mbele ya wale wanaorudi?
20 Mfalme, Yesu Kristo, atafurahia kuwatambua wana-wafalme hawa waliowekwa rasmi karibuni, sawa na vile anavyotambua uangalizi wa kondoo wengine waaminifu katika makundi ya ki-siku-hizi ya Mashahidi wa Yehova. Washiriki wote wa umati mkubwa wa kondoo wengine—wanawake na vilevile wanaume—watakuwa na pendeleo lenye kusisimua la kuwakaribisha kutoka kwa wafu wote ambao watasikia sauti ya Yesu na kuinuka ili wawe na fursa ya kupata uhai wa milele katika ukamilifu wa kibinadamu juu ya dunia iliyosafishwa ambayo itageuzwa iwe paradiso ya tufe lote. (Yohana 5:28, 29) Wapendelewa hao watakaofufuliwa watatia ndani babu za Yesu waliofidiwa, watu wa imani waliokuwa na nia ya kuthibitisha ujitoaji wao kwa Yehova Mungu hata mpaka kufa wakiwa na tumaini la kupata “ufufuo ulio bora.” (Waebrania 11:35) Lakini kuinuliwa kufikia uhai mkamilifu wa kibinadamu wakati wa Utawala wa Mileani wa Mfalme-Mfidia wao, Yesu Kristo, ni mwanzo tu. Kwa kubaki chini ya Yehova Mungu wakiwa katika mpango wa kitengenezo usiovunjika wakati wa mtihani wa mwisho juu ya aina ya binadamu waliorudishwa mwishoni mwa Mileani, watajithibitisha wenyewe kuwa wanastahili kuhesabiwa kuwa haki wapate uhai usio na kikomo katika Paradiso wakiwa sehemu ya kidunia ya tengenezo la Yehova la ulimwengu wote mzima.—Mathayo 25:31-46; Ufunuo 20:1–21:1.
[Maelezo ya Chini]
a Linganisha 2 Samweli 8:18, New World Translation Reference Bible, maelezo ya chini.
Wewe Ungejibuje?
◻ Yehova ameweka kando kipindi gani kwa kubariki aina yote ya binadamu?
◻ Ni kwa kubaki tu katika uhusiano gani mmoja na mwenzake ndipo tunaweza kuokokadhiki kubwa?
◻ Inamaanisha nini kwa kondoo ‘kurithi ufalme waliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu’?
◻ Wakati wa Mileani, huenda umati mkubwa ukashiriki mapendeleo gani?