Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • br78 kur. 14-17
  • Habari Njema Wanazotaka Wewe Usikie

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Habari Njema Wanazotaka Wewe Usikie
  • Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • BARAKA ZA KIDUNIA CHINI YA UFALME
  • Habari Njema Wanazotaka Usikie
    Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini?
  • Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Maswali Manne Kuhusu Mwisho Yajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Maisha Anayotuwezesha Kupata
    Amkeni!—2006
Pata Habari Zaidi
Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya 20
br78 kur. 14-17

Habari Njema Wanazotaka Wewe Usikie

Yesu alipokuwa duniani, wanafunzi wake walimjia wakamwuliza: “Ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?” Alijibu kwamba kungekuwako vita vyenye kuhusu mataifa mengi, njaa, magonjwa ya kipuku, matetemeko ya dunia, kuongezeka kwa uasi, walimu wa uwongo wa kidini wakipoteza wengi, wafuasi wake wa kweli wangechukiwa na kunyanyaswa, na upendo wa kutaka uadilifu ungepoa katika watu wengi. Wakati mambo hayo yangeanza kutukia, ingeonyesha kuwapo kwa Kristo bila kuonekana, na kwamba Ufalme wa kimbingu ungekuwa karibu. Hizo zingekuwa habari​—habari njema! Hivyo Yesu aliongeza maneno haya kuwa sehemu ya ile ishara: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa kwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mathayo 24:3-14, New World Translation.

Matukio yenyewe ya ulimwengu ya juzijuzi ni mabaya, lakini kile ambacho yanamaanisha, yaani, kuwapo kwa Kristo, ni chema. Kwa hiyo, Yesu alisema: “Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.” (Luka 21:28) Mambo hayo yalianza kutukia mwaka ule uliotangazwa kotekote wa 1914! Ulionyesha mwisho wa Nyakati za Mataifa na mwanzo wa kipindi cha badiliko kutoka utawala wa kibinadamu kuja kwenye Utawala wa Kristo wa Miaka 1,000 (Mileani).

Kwamba kungekuwapo kipindi cha badiliko yaonyeshwa na Zaburi ya 110, mistari 1 na 2, na Ufunuo 12:7-12. Inaonyeshwa humo kwamba Kristo angeketi kwenye mkono wa kulia wa Mungu mbinguni mpaka wakati wa kuja kwake mara ya pili. Ndipo vita mbinguni ingetokeza kufukuzwa kwa Shetani kuja kwenye dunia, kukileta ole duniani, na Kristo angetawala katikati ya maadui wake kwa kipindi kisichozidi kizazi kimoja. Mwisho kamili wa uovu ungekuja kupitia “dhiki kubwa,” ikifikia upeo katika vita ya Har–Magedoni na kufuatwa na Utawala wa amani wa Kristo wa Miaka 1,000.​—Mathayo 24:21, 33, 34; Ufunuo 16:14-16.

“Kumbuka kwamba,” Biblia yasema, “katika siku za mwisho, kutakuwa na nyakati za taabu. Watu watakuwa na ubinafsi, wenye tamaa ya fedha, wenye majivuno, wenye kujiona, wenye kumtukana Mungu, wasiowatii wazazi wao, wasio na shukrani na waovu; watatokea watu wasio na upendo moyoni, wasio na huruma, wachongezi, walafi na wakali; watachukia cho chote kilicho chema; watakuwa wahaini, wakaidi na waliojaa kiburi; watapenda anasa kuliko kumpenda Mungu. Kwa nje wataonekana kama watu wenye kumcha Mungu, lakini wataikana nguvu yake. Jiepushe kabisa na watu wa namna hiyo.” (2 Timoteo 3:1-5, Habari Njema kwa Watu Wote) Sasa, huenda watu fulani wakabisha wakisema kwamba mambo hayo yametukia zamani katika historia ya kibinadamu.

Lakini, kama wanahistoria na wafafanuzi wanavyosema, haujapata kuwako wakati duniani kama ule ambao umekuwapo tangu 1914 na kuendelea. Taabu zimeenea zaidi ya zile zilizotangulia. Isitoshe, kwa habari ya sehemu nyingine za ishara ya Kristo ya siku za mwisho, mambo haya ya hakika yapasa kufikiriwa: Kutangazwa duniani pote kwa kuwapo kwa Kristo na Ufalme kumefanywa kwa kiasi kikubwa sana ambacho hakina kifani katika historia. Kunyanyaswa kwa sababu ya kuhubiri hakujapata kuwa na kifani kamwe kama kule ambako Mashahidi wa Yehova wamepata. Mamia mengi kati yao waliuawa katika kambi za mateso za Hitler. Mpaka leo hii Mashahidi wa Yehova wamepigwa marufuku katika nchi nyingi, na katika nyingine wanakamatwa, wanafungwa gerezani, wanateswa, na kuuawa. Yote hayo ni sehemu ya ile ishara ambayo Yesu alitoa.

Kama ilivyotabiriwa katika Ufunuo 11:18, ‘Mataifa wamekasirikia’ Mashahidi waaminifu wa Yehova, na hiyo inaonyesha kwamba “hasira” ya Yehova mwenyewe italetwa juu ya mataifa hayo. Andiko ilo hilo lasema kwamba Mungu ‘atawaharibu hao wanaoiharibu dunia.’ Haujapata kamwe kuwako wakati zamani katika historia ya kibinadamu ambapo uwezo wa dunia kuendeleza uhai umekaribia kuharibiwa. Lakini, sasa ni tofauti! Wanasayansi wengi wameonya kwamba iwapo mwanadamu ataendelea kuichafua dunia, itakuwa isiyokalika. Lakini Yehova “aliiumba ili ikaliwe na watu,” naye atawaondoa wachafuzi hao kabla hawajamaliza kuiharibu dunia.​—Isaya 45:18.

BARAKA ZA KIDUNIA CHINI YA UFALME

Huenda wazo la kwamba watu wataishi duniani wakiwa raia za Ufalme wa Mungu likaonekana kuwa ajabu kwa waamini wengi wa Biblia wanaodhani kwamba watu wote waliookolewa wako mbinguni. Biblia yaonyesha kwamba ni hesabu ndogo tu inayoenda mbinguni na kwamba wale watakaoishi milele duniani watakuwa umati mkubwa usio na hesabu. (Ufunuo 14:1-5; 7:9; Zaburi 37:11, 29) Kwamba Ufalme wa Mungu mikononi mwa Kristo utaijaa dunia na kuitawala yaonyeshwa na unabii katika kitabu cha Biblia cha Danieli.

Humo Ufalme wa Kristo unafananishwa na jiwe lenye kuchongwa kutoka enzi kuu ya Yehova iliyo kama mlima. Linapiga na kuharibu sanamu inayofananisha mataifa ya dunia yenye nguvu, “na lile jiwe lililoipiga hiyo sanamu likawa mlima mkubwa, likaijaza dunia yote.” Unabii huo waendelea hivi: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”​—Danieli 2:34, 35, 44.

Ufalme huo na lile tumaini linalotegemezwa na Maandiko la uhai wa milele katika dunia iliyosafishwa na kurembwa ndio Mashahidi wa Yehova wanataka kukuambia juu yake. Mamia ya maelfu wanaoishi sasa na mamilioni mengine mengi waliomo sasa katika makaburi yao watapata nafasi ya kukaa humo milele. Ndipo kusudi la awali la Yehova la kuiumba dunia na kuweka ndani yake watu wawili wa kwanza litakapotimizwa, chini ya Utawala wa Kristo Yesu wa Miaka 1,000. Paradiso hiyo ya kidunia haitakuwa yenye kuchosha kamwe. Kama vile Adamu alivyopewa kazi katika bustani ya Edeni, vivyo hivyo jamii ya binadamu itakuwa na mipango itakayohitaji kufikiri kwingi katika kuitunza dunia na mimea na wanyama watakaokuwa juu yayo. “Wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.”​—Isaya 65:22; Mwanzo 2:15.

Maandiko mengi yangeweza kutolewa kuonyesha hali zitakazokuwako wakati itakapojibiwa ile sala ambayo Yesu alifundisha: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.” (Mathayo 6:9, 10) Lakini, acheni hili litoshe kwa sasa: “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, ‘Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao. Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!’ Kisha Yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi akasema, ‘Tazama, nafanya yote mapya.’ Tena akaniambia, ‘Andika hili, maana maneno haya ni ya kuaminika na ya kweli.’”​—Ufunuo 21:3-5, Habari Njema kwa Watu Wote.

[Blabu katika ukurasa wa 15]

“Nyakati za taabu,” LAKINI “ukombozi wenu umekaribia”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki