Sura ya 4
Mungu—Yeye Ni Nani?
1. (a) Ni miungu gani imeabudiwa na watu? (b) Biblia inatoa tofauti gani kati ya “miungu” na “Mungu”?
ULIMWENGUNI pote kuna miungu mingi inayoabudiwa. Katika dini za Shinto, Buddha, Hindu na za kikabila kuna mamilioni ya miungu. Miungu kama vile Zeu na Herme iliabudiwa katika siku za mitume wa Yesu. (Matendo 14:11, 12) Basi inakubali kwamba ‘kuna miungu mingi,’ lakini inasema vilevile kwamba “kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake.” (1 Wakorintho 8:5, 6) Ikiwa ungeulizwa, ‘Mungu huyo ni nani?’ ungesema nini?
2. Ni maoni gani yanayotofautiana ambayo watu wanayo juu ya Mungu?
2 ‘Yeye ndiye Bwana,’ wengi wanajibu hivyo. Au labda watasema: ‘Yeye ni Roho katika mbingu.’ Kamusi (ya Kiingereza) inamwita Mungu: “Yule Mtu Mkuu Kupita Wote.” Wanapoulizwa: ‘Jina la Mungu ni nani?’ watu fulani wanajibu, ‘Yesu.’ Wengine hawamfikirii Mungu kuwa mtu, lakini kama kani (msukumo) yenye nguvu kila mahali. Na hata watu fulani wanatia shaka kama kuna Mungu. Je! tunaweza kuwa na hakika kwamba yeye yuko?
Kweli Mungu Yuko
3. Nyumba inatokeaje?
3 Unapotazama nyumba nzuri, je! umepata kuwazia nani aliijenga? Ikiwa mtu fulani angekuambia hakuna aliyejenga nyumba hiyo, lakini ilijitokeza yenyewe, ungeamini hivyo? Hapana! Ni kama mwandikaji wa Biblia alivyosema: “Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani.” Kila mtu anajua hivyo. Basi, je! hatuwezi kuukubali uamuzi wa busara wa mwandikaji huyo wa Biblia: “Na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote”?—Waebrania 3:4, HNWW.
4. Mabilioni yale mengi ya nyota yalitokeaje?
4 Ufikirie ulimwengu mzima na mabilioni ya mabilioni ya nyota zilizomo. Hata hivyo zote zinaenda katika mbingu kulingana na sheria zinazofanya kila moja iwe na uhusiano mzuri kabisa na ile nyingine. “Ni nani aliyeziumba hizi . . .”? ni ulizo lililoulizwa zamani za kale. Jibu lili-lotolewa linafaa: Ni Yeye “aletaye nje jeshi lao kwa hesabu; aziita zote kwa majina.” (Isaya 40:26) Bila shaka ungekuwa upumbavu kufikiri kwamba mabilioni ya nyota yalijifanya yenyewe, na, pasipo mwongozo wo wote, yakafanyiza mifumo mikubwa ya nyota zinazokwenda kwa utaratibu mzuri ajabu! —Zaburi 14:1.
5. (a) Kuna uwezekano gani kwamba, vipande mbalimbali vingeweza kujikusanya vyenyewe viwe mashine ya kukatia nyama? (b) Hilo linaonyesha nini juu ya ulimwengu mzima wetu?
5 Ulimwengu mzima huo uliopangwa kwa utaratibu mkubwa sana haungeweza kujitokeza wenyewe. Muumba mwenye akili na uwezo mkubwa alihitajiwa. (Zaburi 19:1, 2) Mwanabiashara mmoja aliyeulizwa sababu gani alimwamini Mungu alieleza kwamba, katika kiwanda chake inamchukua msichana siku mbili kujifunza kuunganisha vipande 17 vya mashine ya kukatia nyama. “Mimi ni mtengenezaji wa visu, vijiko na nyuma za kulia tu,” akasema. “Lakini najua jambo hili, kwamba unaweza kuvitikisa vipande 17 vya mashine ya kukatia nyama na kuvichanganya-changanya katika bakuli la kuoshea vyombo kwa muda wa mabilioni 17 ya miaka inayokuja na hutaona vikiungana viwe mashine ya kukatia nyama.” Ulimwengu mzima huu, pamoja na namna nyingi za uhai duniani, ni mgumu sana sana kufahamika kuliko mashine ya kukatia nyama. Ikiwa mashine hiyo inahitaji mtengenezaji mwenye ujuzi, tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu Mweza Yote alihitajiwa ili kuumba vitu vyote. Basi, inafaa kumsifu kwa vitu ambavyo amefanya, sivyo?—Ufunuo 4:11; Matendo 14:15-17; 17:24-26.
Je! Mungu Ni Mtu Halisi?
6. Sababu gani tunaweza kuwa na hakika kwamba Mungu ni mtu halisi?
6 Ijapokuwa watu wengi wanasema wanamwamini Mungu, wengi hawamfikirii kuwa mtu halisi. Je! yeye ni mtu halisi? Ni wazi kwamba, palipo uwezo wa kufikiri pana akili. Kwa mfano, labda tutasema, ‘Ninatatizwa akili, siwezi kuamua.’ Nasi tunajua kwamba palipo akili pana ubongo katika mwili ulio na umbo halisi. Hivyo, basi, ile akili kubwa iliyofanya viumbe vyote ni mali ya Mtu mkubwa, Mungu Mweza Yote. Ingawa yeye hana mwili wenye nyama, ana mwili wa kiroho. Je! mtu wa kiroho ana mwili? Ndiyo, Biblia inasema: “Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko.”—1 Wakorintho 15:44; Yohana 4:24.
7. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba Mungu ana mahali anapoishi? (b) Ni nini kinachoonyesha kwamba anao mwili?
7 Kwa kuwa Mungu ni mtu mwenye mwili wa kiroho, bila shaka ana mahali pa kuishi. Biblia inatuambia kwamba mbingu ni “makao” ya Mungu yaliyoimarishwa. (1 Wafalme 8:43) Vilevile, tunaambiwa kwamba “Kristo . . . aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu.” (Waebrania 9:24) Wanadamu fulani watapewa thawabu ya kuishi mbinguni pamoja na Mungu, na wakati huo watapokea milli ya kiroho. Biblia inasema hapo ndipo watamwona Mungu, wawe pia kama yeye. (1 Yohana 3:2) Hilo, pia, linaonyesha kwamba Mungu ni mtu, na kwamba ana mwili.
8, 9. (a) Mfano wa mtambo wa umeme unaweza kuonyeshaje kwamba uwezo wa Mungu ni wenye kufika mbali? (b) Roho takatifu ya Mungu ni nini, nayo inaweza kufanya nini?
8 Lakini labda mtu fulani atauliza hivi: ‘Ikiwa Mungu ni mtu halisi anayeishi mahali fulani mbinguni, anaweza kuonaje kila kitu kinachotendeka kila mahali? Na uwezo wake unawezaje kuhisiwa katika kila sehemu ya ulimwengu mzima?’ (2 Mambo ya Nyakati 16:9) Uwezo wala ukuu wa Mungu haupungui kwa sababu ya kwamba yeye ni mtu. Wala haitupasi kuacha kumheshimu sana kwa sababu hiyo. (1 Mambo ya Nyakati 29:11-13) Ili kutusaidia tufahamu hilo, fikiria matokeo yenye kufika mbali ya mtambo wa umeme.
9 Mtambo wa umeme una mahali fulani katika mji au karibu yake. Lakini umeme unaenezwa katika sehemu yote hiyo, ukitoa mwangaza na nguvu za kufanyia kazi. Ndivyo alivyo Mungu. Yeye yuko mbinguni. (Isaya 57:15; Zaburi 123:1) Hata hivyo roho takatifu yake, ambayo ni kani (nguvu) ya utendaji isiyoonekana, inaweza kuhisiwa kila mahali, katika ulimwengu mzima wote. Kwa kutumia roho takatifu yake, Mungu aliumba mbingu, dunia na vitu vyote vyenye uhai. (Zaburi 33:6; Mwanzo 1:2; Za-buri 104:30) Ili aumbe vitu hivyo, Mungu hakuhitaji kuwapo katika mwili. Yeye anaweza kuipeleka roho yake, kani ya utendaji wake, ifanye lo lote analotaka ijapokuwa yuko mbali. Mungu wa ajabu kama nini!—Yeremia 10:12; Daniell 4:35.
Mungu Ni Mtu wa Aina Gani?
10. Ni katika njia gani moja tunavyoweza kumjua Mungu?
10 Je! Mungu ni aina ya mtu ambaye tungezidi kumpenda ikiwa tungepata kumjua vizuri? ‘Labda ndivyo,’ huenda ukajibu hivyo, ‘lakini kwa kuwa hatuwezi kumwona Mungu, tunaweza kumjuaje?’ (Yohana 1:18) Biblia inaonyesha njia moja inapose-ma hivi: “Kwa maana sifa zake zisizoonekana zinaonekana wazi tangu kuumbwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zina-fahamika kwa vitu vile vilivyofanywa, hata uweza wake wa milele na Uungu.” (Waroma 1:20, NW) Basi vitu ambavyo Mungu ameumba, tukivichunguza kweli kweli na kuvifikiria, vinaweza kutusaidia tufahamu Mungu alivyo.
11. Tunaweza kujifunza nini juu ya Mungu kwa vitu alivyovifanya?
11 Kama tulivyokwisha kuona, kuzitazama mbingu zenye nyota kunaweza bila shaka kutuambia habari za ukuu wa Mungu na uweza wake mkubwa! (Zaburi 8:3, 4; Isaya 40:26) Halafu ifikirie dunia. Mungu aliiweka katika mbingu mahali panapoiwezesha kupata kiasi kinachofaa tu cha joto na nuru kutokana na jua. Tena fikiria kawaida ambayo maji yanafuata. Mvua inaanguka imwagilie dunia maji. Maji hayo yanaingia katika mito, nayo inatiririka kuingia katika bahari. Jua linainua maji hayo baharini yakiwa mvuke, nao unaanguka kuwa mvua ya kumwagilia dunia maji tena. (Mhubiri 1:7) Kuna kawaida nyingi na za ajabu alizoweka Mungu katika utendaji ili kutoa chakula, makao na vitu vyote ambavyo wanadamu na wanyama wanahitaji! Na vitu vyote hivyo vya ajabu vinatuambia Mungu ni mtu wa namna gani? Kwamba yeye ni Mungu wa hekima kuu na ni mkarimu sana sana na anaangalia viumbe vyake.—Mithali 3:19, 20; Zaburi 104:13-15, 24, 25.
12. Mwili wako mwenyewe unakufundisha nini juu ya Mungu?
12 Ufikirie mwili wako mwenyewe. Ni wazi kwamba ulifanywa utende mengi kuliko kuishi tu. Ulibuniwa kiajabu ili kufurahia maisha kweli kweli. (Zaburi 139:14) Macho yetu yanaweza kuona si weusi na weupe tu bali rangi za namna nyingi. Nao ulimwengu umejaa rangi nyingi za kufurahia. Tunaweza kunusa na kuonja. Hivyo kula si utendaji wa lazima tu; kunaweza kupendeza. Ijapokuwa si lazima tuwe na hisi hizo ili tuishi, ni zawadi kutoka kwa Mungu mwenye upendo, ukarimu na busara.—Mwanzo 2:9; 1 Yohana 4:8.
13. Unajifunza nini juu ya Mungu kutokana na njia yake ya kushughulika na wanadamu?
13 Vilevile kuchunguza shughuli za Mungu pamoja na wanadamu kunaonyesha Mungu ni wa namna gani. Yeye anafuata sana kaki ya hukumu. Hapendelei jamii fulani za watu. (Matendo 10:34, 35) Vilevile ni mwenye rehema na fadhili. Biblia inasema yafuatayo juu ya kushughulika kwake na taifa la Israeli, ambao aliokoa utumwani Misri: “Yeye alikuwa mwenye rehema; . . . aliendelea kukumbuka kwamba wao walikuwa mwili.” Hata hi-vyo mara nyingi Waisraeli hao walikataa kutii, na hilo lilimhuzunisha Mungu. Kama Biblia inavyosema: “Walikuwa wakimfanya audhike . . . nao wakamtia uchungu hata Yule Mtakatifu wa Israeli.” (Zaburi 78:38-41; 103:8, 13, 14, NW) Kwa upande mwingine, Mungu anafurahi watumishi wake wanapotii sheria zake. (Mithali 27:11) Vilevile, Mungu anaeleza namna anavyohisi wakati watumishi wake wanapoteswa na adui: “Yeye anayegusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.” (Zekaria 2:8, NW) Je! wewe huvutwi umpende Mungu anayeonea wanyonge shauku hiyo, wanadamu wa hali ya chini sana wa jamii na kabila zote?—Isaya 40:22; Yohana 3:16.
JE! MUNGU NI YESU AU NI UTATU?
14. Fundisho la Utatu ni nini? mapenzi ya Mungu, wala si yake, yatimizwe,
14 Ni nani Mungu huyo wa ajabu? Watu fulani wanasema jina lake ni Yesu. Wengine wanasema yeye ni Utatu, ijapokuwa neno hili “utatu” halionekani katika Biblia. Kulingana na mafundisho ya Utatu, kuna watu watatu katika Mungu mmoja, yaani, kuna “Mungu mmoja, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.” Matengene-zo mengi ya kidini yanafundisha hivyo, ijapokuwa wao wana-kubali kwamba hilo ni “fumbo.” Je! maoni hayo juu ya Mungu ni sawa?
15. Biblia inaonyesha namna gani kwamba hasa wawili hawawezi kuwa ni nafsi moja Mungu na Yesu ni watu wawili walio mbali mbali, wasiolingana?
15 Basi, je! Yesu alisema wakati wo wote kwamba yeye ni Mungu? Hakusema hivyo hata kidogo. Badala yake, katika Biblia yeye anaitwa “Mwana wa Mungu.” Naye alisema: “Baba ni mkuu kuliko mimi.” (Yohana 10:34-36; 14:28) Vilevile, Yesu alieleza kwamba yalikuwako mambo ambayo wala yeye wala malaika hawakuyajua ila Mungu peke yake. (Marko 13:32) Zaidi ya hayo. pindi moja Yesu alisali kwa Mungu akisema: “Si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.” (Luka 22:42) Ikiwa Yesu angekuwa Mungu Mweza Yote, angekuwa akijiomba mwenyewe, sivyo? Kwa kweli, baada ya kufa kwa Yesu, Andiko linasema hivi: “Yesu huyo Mungu alimfufua.” (Matendo 2:32) Basi ni wazi kwamba Mungu Mweza Yote na Yesu ni watu wawili walio tofauti. Hata baada ya kufa kwake na kufufuliwa na kupanda mbinguni, Yesu bado alikuwa mdogo kwa Baba yake.—1 Wakorintho 11:3; 15:28.
16. Ijapokuwa Yesu anatajwa kuwa “Mungu,” ni nini kinachoonyesha kwamba yeye 51 Mungu Mweza Yote?
16 ‘Lakini je! Yesu haitwi mungu katika Biblia?’ labda mtu fulani atauliza. Hiyo ni kweli. Hata hivyo Shetani pia anaitwa mungu. (2 Wakorintho 4:4) Katika Yohana 1:1, andiko linalomtaja Yesu kuwa “Neno,” tafsiri fulani za Biblia zinasema: “Hapo mwanzo kulikuwako yule Neno, na yule Neno alikuwako pamoja na Mungu, na yule Neno alikuwa Mungu.” Lakini angalia, mstari wa 2 unasema kwamba Neno huyo alikuwa “mwanzoni pamoja na Mungu.” Ijapokuwa wanadamu wamemwona Yesu, mstari wa 18 unasema kwamba “hakuna mwanadamu ambaye ameona Mungu wakati wo wote.” (Authorized au King James Version) Hivyo tunaona kwamba tafsiri fulani za mstari 1 zinatoa maana sahihi ya lugha ile ya kwanza kabisa zinaposomwa hivi: “Huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, na huyo Neno alikuwa wa kimungu,” au alikuwa “mungu mdogo,” yaani, huyo Neno alikuwa mtu mwenye nguvu za kimungu. (An American Translation) Kwa wazi, Yesu si Mungu Mweza Yote. Kwa kweli, Yesu alimtaja Baba yake kuwa “Mungu wangu” na “Mungu wa pekee wa kweli.”—Yohana 20:17; 17:3.
17. Kule kumwagwa kwa roho takatifu juu ya wafuasi wa Yesu kunahakikishaje kwa-mba roho hiyo si mtu?
17 Kwa habari ya “Roho Mtakatifu,” yule anayeitwa Mtu (Nafsi) wa tatu wa ule Utatu, tumekwisha kuona kwamba si mtu bali ni kani (nguvu) ya utendaji ya Mungu. Yohana Mbatizaji alisema kwamba Yesu angebatiza kwa roho takatifu, Imam Yohana alivyokuwa amekuwa akibatiza kwa maji. Basi, kama vile maji si mtu, roho takatifu si mtu. (Mathayo 3:11) Matabiri ya Yohana yalitimizwa baada ya kufa na kufufuliwa kwa Yesu, wakati roho takatifu ilipomwagwa juu ya wafuasi wake waliokusanyika Yerusalemu. Biblia inasema: “Wote wakajazwa roho takatifu.” (Matendo 2:4, NW) Je! ‘walijazwa’ mutu? Sivyo, bali walijazwa kani ya utendaji ya Mungu. Hivyo mambo ya hakika yanaonyesha wazi kwamba Utatu si fundisho la Biblia. Kwa hakika, zamani kabla Yesu hajatembea hapa duniani miungu iliabudiwa katika vikundi vya utatu-utatu, au vikundi vingi vya watatu-watatu, kama huko Misri na Babiloni ya kale.
Jina la Mungu
18. (a) Je! “Mungu” ndilo jina la kibinafsi la Mungu Mweza Yote? (b) Jina lake binafsi ni jina gani?
18 Bila shaka kila mtu unayejua ana jina. Mungu vilevile ana jina lake mwenyewe la kujitofautisha na wengine wote. ‘Jina lake si “Mungu”?’ labda watu fulani watauliza hivyo. Sivyo, maana “Mungu” ni mtajo tu wa cheo, kama vile “Rais,” “Mfalme” na “Hakimu” ilivyo mitajo ya cheo. Tunajifunza jina la Mungu katika Biblia, linamoonekana karibu mara 7,000. Kwa mfano, katika tafsiri ya Kiswahili Union Version, Zaburi 83:18 inasomwa hivi: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.” Vilevile, jina la Mungu linapatikana katika Biblia nyingi katika Ufunuo 19:1-6, likiwa sehemu ya usemi “Haleluya.” Maana yake ni “msifu-ni Yah,” kifupi cha Yehova.
19. (a) Sababu gani watu fulani wanashangaa kuona jina la Mungu katika Biblia yao? (b) Ni wapi katika Biblia Union Version ya Kiswahili ambapo jina hilo linaonekana?
19 Watu fulani wanashangaa kuona jina la Mungu katika Biblia yao. Ni kwa sababu Biblia yao inatumia mara chache jina la Mungu. Kwa mfano, Biblia ya Kiswahili Union Version inatumia jina hilo “Yehova” likiwa peke yalo katika Kutoka 6:2, 3, 6-8; Zaburi 68:20; 83:18; Isaya 12:2; 26:4; 49:14; Yeremia 16:21 na Habakuki 3:19. Walakini, wakati Biblia hiyo inapotafsiri jina la Mungu kwa mtajo wa “Bwana” au “Mungu,” nyakati zote mtajo huo unakuwa katika herufi kubwa, “BWANA” na “MUNGU,” unaolitofautisha na maneno “Bwana” na “Mungu,” yanayotumiwa kuhusu mtu ye yote tu. Angalia hilo katika Zaburi 110:1.
20. (a) Sababu gani mara nyingi jina la Mungu halikutumiwa? (b) Je! litumiwe?
20 ‘Lakini sababu gani,’ labda utauliza, ‘jina la Mungu halitumiwi kila mahali linapoonekana katika maandishi ya kwanza kabisa ya Biblia? Sababu gani mitajo BWANA na MUNGU inatumiwa kwa kawaida mahali palo?’ Katika dibaji yake, Biblia American Standard Version inaeleza sababu gani inatumia jina la Mungu Yehova, na sababu gani kwa muda mrefu jina hilo halikutumiwa: “Baada ya kufikiri kwa uangalifu, Wasahihishaji Waamerika walisadiki kwa umoja kwamba ushirikina wa Kiyahudi, ulioliona Jina la Kimungu kuwa takatifu mno lisiweze kutamkwa, haupasi tena utawale katika Kiingereza wala katika tafsiri nyingineyo . . . Jina hilo la kibinafsi, lenye mahusiano mengi matakatifu, sasa linarudishwa mahali linapopasa kuwa bila kupingwa katika maandishi matakatifu.” Ndiyo, watu waliotafsiri Biblia hiyo katika Kiingereza waliona kwamba zile sababu zilizofanya jina la Mungu liondolewe mahali palo hazikuwa nzuri. Basi wakalirudisha mahali linapofaa kuwa katika Biblia.
21. Biblia Douay Version ya Kikatoliki inaserna nini juu ya jina Yehova?
21 Walakini, kuna wale wanaopinga wakisema neno “Yehova” halipasi kutumiwa kwa sababu si jina lenyewe la Mungu. Kwa mfano, Biblia ya Kikatoliki Douay Version, isiyotumia jina la Mungu katika maandishi yake makuu, inasema hivi katika maelezo ya chini juu ya Kutoka 6:3: “Watu fulani wa kisasa wametunga jina Yehova . . . matamshi ya kweli ya jina hilo, ambalo liko katika maandishi ya Kiebrania, hayajulikani sasa, kwa maana kwa muda mrefu limekuwa halitumiwi.”
22. (a) Jina la Mungu linawakilishwaje katika lugha ya Kiebrania? (b) Sababu gani kuna tatizo la kujua narnna jina la Mungu lilivyotamkwa hapo kwanza?
22 Ndiyo, kama vile Biblia ya Kikatoliki inavyosema hapa, jina la Mungu linaonekana katika maandishi ya Kiebrania, Kiebrania kikiwa ndiyo lugha iliyotumiwa kuandika vitabu vya kwanza 39 vya Biblia. Jina, hilo linawakilishwa humo na herufi nne za Kiebrania, YHWH. Katika nyakati za kale lugha ya Waebrania iliandikwa bila herufi a, e, i, o na u, herufi zinazotusaidia kutamka maneno inavyofaa. Kwa hiyo, tatizo leo ni kwamba hatuna njia ya kujua sawasawa ni herufi gani za a, e, i, o, u, ambazo Waebrania walitumia pamoja na konsonanti YHWH.
23. Maendelezo ya herufi “jng” badala ya “jengo” yanawezaje kutusaidia tufahamu lile tatizo la kutamka jina la Mungu?
23 Ili kutusaidia tufahamu tatizo hilo, fikiria neno hili “jengo.” Tuseme kwamba nyakati zote lingeandikwa “jng,” na baadaye liache kabisa kutamkwa. Sasa, mtu wa miaka 1,000 tangu sasa angejuaje kutamka herufi “jng” akiziona zimeandikwa hivyo? Kwa kuwa hakusikia hapo kwanza matamko ya neno hilo wala hajui ni herufi gani za a, e,i,o, u zilizotumiwa, bila shaka hangejua. Iko hivyo na jina la Mungu. Haijulikani hasa namna lilivyotamkwa, ijapokuwa wanachuo fulani wanafikiri “Yahweh” ni matamshi sahihi. Walakini, “Yehova” ni namna ambayo imetumiwa kwa karne nyingi na inajulikana sana mahali pote.
24. (a) Ili tuwe wasiogeuka-geuka, sababu gani inafaa tutumie jina la Mungu? (b) Kwa sababu ya Matendo 15:14, sababu gani ni jambo la maana kutumia jina la Mungu?
24 Hata hivyo, je! tulitumie jina la Mungu, ijapokuwa labda hatutakuwa tukilitamka sawasawa kama mwanzoni? Tunatumia majina ya watu wengine katika Biblia, ijapokuwa hatuyatamki sawasawa na Kiebrania cha kwanza kabisa. Kwa mfano, jina la Yesu linatamkwa “Yesh’ua” katika Kiebrania. Vivyo hivyo, inafaa kutumia jina la Mungu, ambalo limefunuliwa katika Biblia, hata kama tunalitamka “Yahweh,” “Yehova,” ama katika njia nyingine ambayo watu wanazoea kutamka katika lugha yetu. Ubaya ni kukosa kutumia jina hilo. Kwa sababu gani? Kwa sababu wale wasiolitumia hawawezi kuwa kati ya wale ambao Mungu anachukua wawe “watu kwa ajili ya jina lake.” (Matendo 15:14, NW) Haitupasi tulijue tu jina la Mungu bali tulisifu mbele ya wengine, kama Yesu alivyofanya alipokuwa hapa duniani. —Mathayo 6:9; Yohana 17:6, 26.
Mungu wa Kusudi
25. (a) Ni mambo gani juu ya Mungu ambayo huenda yakawa magumu kwetu kufahamu? (b) Ni nini kilichomwongoza Yehova aanze kuumba vitu?
25 Ijapokuwa huenda ikawa vigumu kwa akili zetu kufahamu, Yehova hajapata kuwa na mwanzo na hatakuwa na mwisho hata kidogo. Yeye ni “Mfalme wa umilele.” (Zaburi 90:2; 1 Timotheo 1:17, NW) Kabla hajaanza kuumba vitu, Yehova alikuwa peke yake katika anga la ulimwengu mzima. Hata hivyo hangaliweza kuwa mpweke, kwa sababu yeye ni kamili ndani yake mwenyewe na hakosi lo lote. Ni upendo uliomwongoza aanze kuumba, kuwapa wengine uhai wafurahie vitu. Viumbe vya Mungu vya kwanza vilikuwa watu wa kiroho kama yeye. Yeye alikuwa na tengenezo kubwa la wana wa kimbinguni hata kabla ya dunia kutayarishwa kuwa makao ya wanadamu. Yehova alikusudia waone furaha kubwa katika maisha na katika utumishi ambao aliwapa.—Ayubu 38:4, 7.
26. Sababu gani tunaweza kuwa na hakika kwamba kusudi la Mungu kwa dunia litatimizwa?
26 Dunia ilipotayarishwa, Yehova aliweka watu wawili, Adamu na Hawa, katika sehemu ya dunia iliyokuwa tayari paradiso. Lilikuwa kusudi lake wawe na watoto ambao wangetii na kumwabudu yeye, na kupanua paradiso hiyo duniani pote. (Mwanzo 1:27, 28) Walakini, kama vile tulivyokwisha kujifunza, kusudi hilo la ajabu lilizuiwa. Adamu na Hawa walichagua kutokutii Mungu, na kusudi lake halijatimizwa. Lakini litatimizwa, kwa maana ingekuwa kama Yehova anakubali kushindwa ikiwa hatimizi yale anayokusudia. Na hilo hangeweza kufanya hata kidogo! “Nitatenda mapenzi yangu yote,” anatangaza. “Nimenena, nami nitatekeleza.”—Isaya 46:10, 11.
27. (a) Kwa nini Mungu atatutaka tutoe sababu ya matendo yetu? (b) Basi ni ulizo gani ambalo imetupasa tufikirie kwa uzito?
27 Je! unaona una sehemu yo yote katika kusudi la Mungu? Si kwa kufanya tu lo lote utakalo bila kufikiria yaliyo mapenzi ya Mungu. Hivyo ndivyo Shetani na Adamu na Hawa walifanya. Walijua mapenzi ya Mungu lakini hawakuyafanya. Mungu aliwataka watoe sababu ya matendo yao. Je! sisi pia tunatakwa kutoa sababu ya matendo yetu? Ndiyo, kwa sababu Mungu ndiye Chemchemi ya uzima wetu. Uzima wetu unategemea yeye. (Zaburi 36:9; Mathayo 5:45) Ni kwa kadiri gani, basi, sisi tunaishi kupatana na anayokusudia Mungu tufanye? Inatupasa tufikirie kwa uzito jambo hilo, kwa sababu nafasi yetu ya kupata uzima wa milele inalitegemea hilo.
Namna ya Kuabudu Yehova
28. Ni misaada gani ambayo watu fulani wametumia ili waabudu Mungu?
28 Namna tunavyoabudu Yehova ni jambo la maana. Imetupasa tuabudu katika njia anayoisema hata ikiwa tofauti na njia ile ambayo tumefundishwa. Kwa mfano, imekuwa desturi ya watu fulani kutumia mifano katika kuabudu kwao. Labda watasema hawauabudu mfano, bali kuuona na kuugusa kunawasaidia waabudu Mungu. Hata hivyo, je! Mungu anataka tumwabudu kwa kusaidiwa na mifano?
29. Biblia inaonyesha namna gani kwamba ni makosa kutumia mifano katika ibada?
29 Hataki hivyo. Na kwa sababu iyo hiyo Musa aliwaambia Waisraeli kwamba Mungu hakuwatokea katika umbo lo late linaloonekana. (Kumbukumbu la Torati 4:15-19) Kwa kweli, moja ya Amri Kumi inasema: “Hutajifanyia sanamu ya kuchongwa wala mfano wo wote wa cho chote . . . hutaviinamia wala kuvitumikia.” (Kutoka 20:4, 5, Jerusalem Bible ya Kikatoliki) Yehova peke yake ndiye amepaswa kuabudiwa. Biblia inaonyesha tena na tena namna lilivyo kosa kufanya mfano au kuinama mbele ya huo, au kuabudu ye yote au cho chote isipokuwa Yehova.—Isaya 44:14-20; 46:6, 7; Zaburi 115:4-8.
30. (a) Yesu na mitume wake walisema nini kinachoonyesha kwamba ni kosa kutumia mifano? (b) Kulingana na Kumbukumbu la Torati 7:25, mifano inapasa ifanywe nini?
30 Basi, kama ambavyo labda tumetazamia. Yesu hakutumia mifano hata kidogo katika kuabudu. “Mungu ni Roho,” akaeleza, “na wale wanaoabudu yeye lazima waabudu kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24, NW) Kwa kufuata shauri hilo, hakuna ye yote wa wafuasi wa kwanza wa Yesu aliyetumia mifano imsaidie katika ibada. Kwa kweli, Paulo mtume wake aliandika hivi: “Sisi tunatembea kwa imani, si kwa kuona.” (2 Wakorintho 5:7, NW) Naye mtume wake Yohana alionya hivi: “Jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Sababu gani usitazame uku na huku katika nyumba yako ujiulize karna unafuata au hufuati shauri hilo?—Kumbukumbu la Torati 7:25.
31. (a) Hata ikiwa labda hatufahamu sababu ya kutolewa kwa sheria fulani ya Mungu, ni nini kitakachotuongoza tuitii? (b) Imetupasa tujaribu kufanya nini, na ni mwito gani tunaopaswa kuukubali?
31 Kuabudu Yehova, Muumba, katika njia anayoelekeza kutatuletea furaha ya kweli kweli. (Yeremia 14:22) Biblia inaonyesha kwamba matakwa yake yanatolewa kwa faida yetu, ili tupate hali njema ya milele. Ni kweli kwamba huenda zikawako nyakati ambazo, kwa sababu ya uchache wa maarifa na ujuzi wetu, hatufahamu vizuri kabisa sababu gani sheria fulani inayotolewa na Mungu ni ya maana sana au inavyotuletea faida hasa. Hata hivyo, kuamini kwetu thabiti kwamba Mungu anajua mengi kushinda sisi kunafaa kutuongoze tumtii yeye kwa moyo wa kupenda. (Zaburi 19:7-11) Basi, na tufanye kila jitihada tujifunze yote tuwezayo juu ya Yehova, tukiukubali mwito wake huu: “Ee karibuni, na tuabudu na kuinama chini; na tupige magoti mbele za Yehova Mfanyi wetu. Maana yeye ni Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake na kondoo za mkono wake.”—Zaburi 95:6, 7, NW.
[Sanduku kwenye ukurasa wa 42]
Baadhi ya mahali ambapo jina la Mungu linaoneka katika Biblia Union Version ya Kiswahili panaonekana hapa
3Nami nilimtokea Ibrahimu na Isaka, na Yakobo, kama Mungu mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA, sikujulikana kwao.
18Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, Ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.
2 Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana BWANA YEHOVA nguvu zangu na wimbo wangu, naye amekuwa wokovu wangu.
4 Mtumainini BWANA sikuzote, Maana BWANA YEHOVA ni mwamba wa milele.
[Picha kwenye ukurasa wa 34, na 35]
Ikiwa nyumba ina mjenzi . . . ulimwengu mzima wa vitu vilivyo na maumbo ya ufundi zaidi una mjenzi pia.
[Picha kwenye ukurasa wa 39]
Kwa kuwa Yesu alisali kwa Mungu akiomba mapenzi ya Mungu, wala si yake, yatimizwe, hao wawili hawawezi kuwa ni nafsi moja.
[Picha kwenye ukurasa wa 40, na 41]
Ikiwa roho takatifu iliwajaa wanafunzi karibu 120, ingewezaje kuwa mtu (nafsi)?
[Piccha kwenye ukurasa wa 45]
Je! Inafaa kutumia mifano katika ibada?