Sura ya 3
Mungu ni Nani?
1. Kwa nini kuna mvurugo mwingi juu ya Mungu ni nani?
HAJA YA wanadamu kwa Mungu na msaada wake haikuwa kubwa sana kuliko sasa. Maisha zetu zinategemea juu ya kumjua yeye. Lakini, bila shaka, kuna mvurugo mwingi juu ya yeye ni nani, kwa maana leo, kama zamani, iko miungu mingi inayoabudiwa katika nchi mbalimbali. Lakini Biblia huonyesha waziwazi kwamba kuna Mungu mmoja tu wa kweli.—1 Wakorintho 8:5, 6.
2. (a) Je! “Mungu” ndilo jina peke yake la Mungu wa kweli? (b) Jina lake peke yake ni nini?
2 Ili ajitofautishe mwenyewe na miungu mingi ya uongo, Mungu wa kweli amejipa mwenyewe jina la peke yake. Hili humtenga na wengine wote. Labda wengine watauliza “Je! ‘Mungu’ si ndilo jina lake?” La, kwa maana “Mungu” ni jina la cheo tu, kama vile “Rais,” “Mfalme” na “Hakimu” yalivyo majina ya cheo. Jina la Mungu la peke yake limejulishwa kwetu katika Neno lake, Biblia, na jina hilo ni YEHOVA. Katika tafsiri nyingi za Biblia jina hili hupatikana katika Zaburi 83:18, mahali tusomapo hivi: “Wajue ya kuwa Wewe, uitwaye jina lako YEHOVA, ndiwe peke yako Uliye juu, juu ya nchi yote.” Na katika karibu tafsiri zote jina hili hupatikana katika Ufunuo 19:1-6 kama sehemu ya neno la “Haleluya.” Maana yake ni “msifuni Yah” (ni namna ya kifupi cha Yehova). Kitabu The Catholic Encyclopedia (1910, Vol. VIII, ukurasa wa 329) husema kwa habari ya Jina hili la Kimungu: “Yehova jina la pekee la Mungu katika Agano la Kale.” Walakini, The Jerusalem Bible, tafsiri ya karibuni ya Kikatoliki, kwa kawaida hutumia jina la “Yahweh,” kama zifanyavyo tafsiri fulani nyingine. Kwa nini iko hivyo?
3. (a) Jina la Mungu huonyeshwaje katika Maandiko ya Kiebrania? (b) Kwa nini haiwezekani kujua barabara jinsi jina la Mungu lilivyotamkwa katika Kiebrania katika nyakati za zamani?
3 Katika Kiebrania, lugha ambayo katika hiyo vi-tabu vya kwanza thelathini na tisa vya Biblia viliandikwa, jina la Mungu huonyeshwa kwa maelfu ya mara kwa herufi nne za Kiebrania, YHWH. Katika nyakati za zamani lugha ya Kiebrania iliandikwa bila vokali, msomaji akiwa akitoa vokali kadiri asomavyo maneno. Hivyo, tatizo ni la kwamba leo hatuna njia ya kujua barabara ni vokali zipi walizozitumia Waebrania zamani pamoja na konsonanti (herufi bubu) za YHWH. Wataalamu wengi wa chuo hufikiri jina lilitamkwa “Yahweh,” lakini namna ya “Yehova” imekuwa ikitumika kwa karne nyingi na yajulikana zaidi mahali pote.
4. (a) Mapadre ambao husema haitupasi kulitumia jina la Mungu kwa sababu hatujui tamko lake barabara hawapatani sawasawa jinsi gani? (b) Ni jambo gani la muhimu zaidi sana kuliko jinsi tulitamkavyo jina la Mungu? (c) Kwa nini ni muhimu kwetu kutumia jina la Mungu, kwa sababu ya Matendo 15:14?
4 Kwa sababu hatujui tamko barabara la jina la Mungu la peke yake, mapadre wengine husema lazima usilitumie hata kidogo, lakini badala yake useme tu “Mungu” au “Bwana.” Walakini, hawazidi kusema kwamba lazima usiyatumie majina ya “Yesu” na “Yeremia.” Lakini matamko haya ambayo hutumiwa na watu wote yako tofauti sana na matamko ya Kiebrania ya “Yesh’ua” na “Yirmeiah’.” Jambo la muhimu si tamko gani unalotumia kwa Jina la Kimungu, kwamba ni “Yahweh,” Yehova” a linginelo, ikiwa tamko linatumiwa na watu wote katika lugha yako. Kosa ni kushindwa kulitumia jina hilo. Kwa nini? Kwa sababu wale wasiolitumia hawangeweza kutambuliwa kama wamo miongoni mwa wale ambao Mungu huwachagua kuwa watu “kwa ajili ya jina lake.” (Matendo 15:14) Haitupasi kulijua jina la Mungu tu bali kuliheshimu na kulisifu mbele ya wengine, kama Mwana wa Mungu alivyofanya alipokuwa hapa duniani.—Mathayo 6:9; Yohana 17:6, 26.
SIFA ZA MUNGU NA KWA NINI IMETUPASA TUMWABUDU YEYE PEKE YAKE
5. Kwa nini hapana binadamu ambaye amewahi kumwona Mungu?
5 Biblia yenyewe hutuambia nini juu ya Mungu? Hutuambia kwamba “Mungu ni Roho.” (Yohana 4: 24) Roho haikufanyizwa kwa nyama na damu, wala kwa vitu vingine vya kimwili viwezavyo kuonekana au kugusika kwa milango ya maarifa ya kibinadamu. (1 Wakorintho 15:44, 50) Hivyo, macho ya kibinadamu hayajapata kumwona Mungu kamwe. (Yohana 1:18) Yeye yu mkuu zaidi kupita cho chote ambacho macho yetu huona. Fahari ya milima, mng’aro wa jua, na hata utukufu wa mbingu zenye nyota si kitu kama inalinganishwa na yeye.—Isaya 40:25, 26.
6. (a) Jinsi gani Biblia katika Ufunuo 15:3, 4 husimulia sifa za Mungu? (b) Je! Mungu alikuwa na mwanzo?
6 Si ajabu kwamba katika mbingu wimbo huimbwa hivi: “Kazi zako ni kuu na za ajabu, Ee Yehova Mungu, Mwenye Nguvu zote. Njia zako ni za haki na za kweli, Mfalme wa umilele. Ni nani ambaye kweli hatakuogopa wewe, Ee Yehova, na kulitukuza jina lako, kwa sababu wewe peke yako u mwaminifu?” (Ufunuo 15:3, 4, NW) Kama Muumba wa vitu vyote, Yehova Mungu, “Mfalme wa umilele,” alikuwako kabla ya wote wengine. Yeye ni wa “tangu milele hata milele,” maana yake ni kwamba yeye alikuwa hana mwanzo na hatakuwa na mwisho kamwe.—1 Timotheo 1:17; Zaburi 90:2.
7. (a) Kupatana na Ufunuo 4:11, kwa nini ni haki kwamba ibada yetu imwendee Yehova peke yake? (b) Mungu alitimiza kuumba kwa vitu vyote kwa njia ya gani?
7 Basi, jinsi ilivyo haki kwamba lazima ibada yetu imfikie yeye peke yake! Tuzitafakaripo kazi zake za kuumba, sisi pia twaweza kusema: “Umestahili wewe, [Yehova] wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.” (Ufunuo 4:11) Yeye alitimiza kuumba, si kwa vyombo kama vile wavitumiavyo wanadamu, bali kwa njia ya roho yake takatifu, ambayo ndiyo nguvu yake ya utendaji isi-yoonekana. (Mwanzo 1:2; Zaburi 104:30) Ni roho takatifu ile ile ambayo kwa hiyo baadaye aliandikisha Biblia ili tupate kujua mapenzi yake na makusudi yake kwa wanadamu duniani.—2 Petro 1:21.
8. (a) Kwa nini tuna wajibu kwa Mungu? (b) Basi, ni swali gani ambalo yatupasa tufikiri juu yake kwa uzito?
8 Kwa kuwa vitu vyote viliumbwa ‘kwa sababu ya mapenzi yake,’ lazima vyote vitumikie kusudi la Mungu. Yehova alimpasha habari mwanamume wa kwanza na mwanamke wa kwanza, Adamu na Hawa, juu ya kusudi lake kwao, na aliwajibisha wao kutenda kupatana nalo. Je! na sisi, pia, tuna wajibu kwa Mungu? Ndiyo, kwa sababu Mungu ndiye Chanzo cha uhai wetu. Hili ni kweli, si kwa sababu tumekuwa wazao wa wanadamu wawili wa kwanza tu ambao kwao Mungu alitoa uhai, bali pia kwa sababu uhai wetu wenye kuendelea kila siku hutegemea juu ya jua, mvua, hewa na chakula ambacho kutoka hicho Yehova huendelea kutuacha tufaidike. (Zaburi 36:9; Mathayo 5:45) Basi, ni kwa kiasi gani tunaishi maisha zetu kupatana na kusudi la Mungu kwetu? Yatupasa kufikiri kwa uzito juu ya hili, kwa sababu nafasi yetu ya uzima wa milele iko hatarini.
9. (a) Imetupasa tumwogope Mungu katika njia gani? (b) Kwa nini twaweza kufurahi kwamba Yehova ni mwenye nguvu zote?
9 Je! imetupasa kwa hakika tumwogope Mungu? Ndiyo, lakini kwa hofu kamili ya kuasi mapenzi yake, kwa sababu mapenzi yake ni ya haki. Hata katika mambo ya kawaida, je! hatuogopi kujihatirisha ambako kungeweza kuleta madhara au hasara ya uhai? Jinsi imetupasa zaidi sana tuogope kumkasirisha “Yehova Mungu, Mwenye Nguvu zote.” Lakini twaweza kufurahi kwamba yeye yu mwenye nguvu zote, kwa maana, “macho ya [Yehova] hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake.” (2 Mambo ya Nyakati 16:9; tazama pia Isaya 40:29-31.) Na tuwe hakika kwamba Yehova huutumia uwezo wake sikuzote kwa kusudi jema na kwa faida ya wale wapendao yaliyo haki. Kwa maana “Mungu ni upendo.”—1 Yohana 4:8.
10. Ni sifa gani za Yehova hutufanya sisi kufurahi kuwa na yeye kama Mungu wetu?
10 Kwa hiyo, Yehova, si Mungu mwenye kudhulumu. “Njia zake zote ni haki.” (Kumbukumbu la Torati 32:4) Kweli, yeye ni “Mungu mwenye kutaka ibada ya pekee,” lakini yeye pia ni “Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli.” (Kutoka 20:5, NW; 34:6) “Yeye anatujua umbo letu, na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.” (Zaburi 103:14) Twaweza kufurahi kweli kuwa na Mungu wa namna hiyo mwenye haki lakini mwenye huruma kama Hakimu wetu Mkuu, Mpaji wa sheria na Mfalme.—Isaya 33:22.
11. Hata ijapokuwa huenda tusielewe sababu kwa sheria fulani ya Mungu, jambo gani litatuongoza kuitii?
11 Kwa Yehova kuna “hekima na amri zina yeye; yeye anayo mashauri na fahamu.” (Ayubu 12:13) Ushuhuda wa hekima yake unaonekana katika kazi zake zote za kuumba, mbinguni na duniani pia. Basi, labda tuulize: “Kwa nini ye yote awe na shaka juu ya hekima ya Mungu?” Biblia huonyesha ya kwamba matakwa yake ni kwa faida yetu, kwa kukumbuka hali yetu njema ya milele. Ni kweli kwamba huenda zikawapo nyakati wakati sisi, kama wanadamu wenye maarifa ya kiasi na ujuzi, tusielewe kabisa kwa nini sheria fulani iliyosemwa na Mungu ni yenye muhimu sana, au jinsi ifanyavyo kazi kweli kwa faida yetu. Lakini imani yetu thabiti kwamba kwa wazi Mungu anajua zaidi sana kuliko sisi tujuavyo, kwamba ujuzi wake ni mkubwa zaidi kuliko ujuzi wetu, na ya kwamba jambo alifanyalo ni kwa faida yetu ya milele, itatuongoza sisi kumtii yeye kwa moyo wenye nia. —Zaburi 19:7-11; Mika 6:8.
JE! MUNGU NI “UTATU”?
12. (a) Imani za kanisa, kama vile Imani ya Athanasio, hufundisha nini juu ya Mungu? (b) Imetupasa kuuliza maswali gani juu ya fundisho hili?
12 Dini nyingi za Kristendomu hufundisha kwamba Mungu ni “Utatu,” ijapokuwa neno “Utatu” halionekani katika Biblia. Baraza ya Ulimwengu ya Makani-sa ilisema karibuni kwamba dini zote ambazo ni sehemu ya Baraza hiyo zimepaswa kufundisha imani ya kwamba kuna “Mungu mmoja, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,” yaani, watu watatu katika Mungu mmoja. Wale wafundishao fundisho hili la dini hukubali kwamba ni “fumbo.” Imani ya Athanasio, ya karne yapata ya nane ya Wakati wa Kawaida, husema kwamba Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wote watatu ni wa asili ile ile, wote watatu ni wa milele (na kwa hiyo walikuwa hawana mwanzo), na wote watatu ni wenye nguvu zote. Basi imani husomwa kwamba katika “Utatu hapana aliye kabla wala baada ya mwingine; hapana aliye mkubwa sana au mdogo kuliko mwingine.”a Je! jambo hilo ni la akili? Kwa muhimu zaidi, je! linapatana na Biblia?
13. Kupatana na New Catholic Encyclopedia, je! manabii wa Kiebrania na Wakristo wa kwanza waliamini katika “Utatu”?
13 Fundisho hili la dini halikujulikana kwa manabii wa Kiebrania na mitume wa Kikristo. New Catholic Encyclopedia (chapa ya mwaka wa 1967, Vol. ya XIV, ukur. 306) kinakubali kwamba “fundisho la dini la Utatu Mtakatifu halifundishwi katika Agano la Kale.” Kinakubali pia kwamba fundisho halina budi lilianza kutoka yapata mpaka mia tatu na hamsini baada ya kufa kwa Yesu Kristo. Hivyo Wakristo wa kwanza waliofundishwa na Yesu Kristo hawakuamini kwamba Mungu ni “Utatu.”
14. Yesu alionyeshaje kwamba yeye hakuwa sawa na Babaye?
14 Wakati Yesu alipokuwa duniani kwa hakika yeye hakuwa sawa na Babaye, kwa maana yeye alisema kulikuwako mambo fulani ambayo wala yeye wala malaika hawakujua ila kwamba Mungu peke yake ndiye aliyejua. (Marko 13:32) Tena, yeye aliomba kwa Babaye kwa msaada wakati alipokuwa akijaribiwa. (Luka 22:41, 42) Pia, yeye mwenyewe alisema: “Baba ni mkuu kuliko mimi.” (Yohana 14:28) Kwa sababu ya hii, Yesu alisema kwa habari ya Babaye kama “Mungu wangu” na kama “Mungu wa pekee wa kweli.”—Yohana 20:17; 17:3.
15. Twajuaje kwamba Yesu hakuwa sawa na Mungu hata baada alipofufuliwa kutoka kwa wafu?
15 Baada ya kufa kwa Yesu, Mungu alimfufua kwenye uzima tena na akampa utukufu ulio mkubwa sana kuliko ule aliokuwa nao kabla ya kuja duniani. Walakini, alikuwa angali si sawa na Babaye. Twajuaje? Kwa sababu baadaye Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu husema kwamba Mungu angali yu “kichwa cha Kristo.” (1 Wakorintho 11:3) Biblia husema pia kwamba yampasa Yesu atawale kama mfalme aliyewekwa na Mungu mpaka yeye ameweka adui wote chini ya miguu yake, na ya kwamba ndipo “Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.” (1 Wakorintho 15:28) Kwa wazi, hata tangu kufufuka kwake Yesu Kristo si sawa na Babaye.
16. (a) Je! usemi wa Yesu, “Mimi na Baba tu umoja,” hufundisha “Utatu”? (b) Yesu alimaanisha nini kwa usemi huo?
16 Lakini, je! pindi moja Yesu hakusema, “Mimi na Baba tu umoja”? (Yohana 10:30) Ndiyo, alisema. Walakini, usemi huo hauonyeshi hata kidogo “Utatu,” kwa kuwa yeye alisema tu habari ya watu wawili kama mmoja, si watatu. Kwa hakika Yesu alikuwa hapingi maandiko ambayo tumekwisha kuyasoma. Jambo ambalo alimaanisha kwa usemi huu yeye mwenyewe alieleza wazi baadaye wakati alipoomba kwa habari ya wafuasi wake kwamba “wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja.” (Yohana 17:22) Yesu na Babaye ni “umoja” kwa vile Yesu yu katika upatano kamili na Babaye. Naye aliomba kwamba wafuasi wake wote vilevile wawe katika upatano na Babaye, na Yesu na mmoja na mwenzake.
17. Kwa nini usemi katika Yohana 1:1 haufundishi “Utatu”?
17 Namna gani ule usemi katika Yohana 1:1, unaomtaja Yesu kama “Neno,” ukisema: “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”? Je! huu hauthibitishi “Utatu”? La. Kwanza, angalia, kwamba ni watu wawili tu wanaotajwa, sio watatu. Pia, katika sura ii hii, mstari wa 2 husema kwamba Neno “mwanzo alikuwako kwa (pamoja na) Mungu,” na mstari wa 18 husema kwamba “hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote,” lakini wanadamu wamemwona Yesu Kristo. Kwa sababu hizi, na katika upatano kamili na maandishi ya awali ya Kigiriki, tafsiri fulani za mstari wa 1 husomwa hivi: “Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa wa kimungu,” au alikuwa “mungu,” yaani, Neno alikuwa mwenye nguvu mfano wa mungu. (AT; NW) Hivyo sehemu hii ya Biblia inapatana na zote zinazobaki; haifundishi “Utatu.”b
18. Jinsi gani habari ya Biblia ya jambo lililotukia siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 C.E. huonyesha kwamba roho takatifu isingeweza kuwa mtu?
18 Kwa habari ya “Roho Mtakatifu,” aitwaye “Nafsi ya tatu katika Utatu,” tumekwisha kuona kwamba, si mtu, bali ni nguvu ya utendaji ya Mungu. (Waamuzi 14:6) Yohana Mbatizaji alisema kwamba Yesu angebatiza kwa roho takatifu hata kama Yohana alivyokuwa akibatiza na maji. Maji si mtu wala roho takatifu si mtu. (Mathayo 3:11) Jambo alilotabiri Yohana lilitimizwa wakati Mungu alimfanya Mwanawe Kristo Yesu kuimimina roho takatifu juu ya mitume na wanafunzi wakati wa siku ya Pentekoste mwaka wa 33 C.E., hata “wote wakajazwa na roho takatifu.” Je! ‘walijazwa’ na mtu? La, bali walijazwa na nguvu ya utendaji ya Mungu.—Matendo 2:4, 33, NW.
19. (a) Basi, “Utatu” ni fundisho la Biblia? (b) Ni katika nchi gani ya zamani ambamo wapagani waliamini katika zaidi kuliko utatu mmoja wa miungu?
19 Basi, mambo ya hakika huonyesha nini kwa habari ya “Utatu”? Wala neno wala wazo halimo katika Neno la Mungu, Biblia. Fundisho la dini halikutokana na Mungu. Lakini, utapendezwa kujua kwamba, kupatana na kitabu Babylonian Life and History (kilichoandikwa na Sir E. A. Wallis Budge, chapa ya mwaka wa 1925, kur. za 146, 147), katika Babeli wa zamani, wapagani waliamini katika jambo la namna hiyo; kwa kweli, wao waliabudu zaidi kuliko utatu mmoja wa miungu.
KUMWABUDU MUNGU “KATIKA ROHO NA KWELI”
20. Kupatana na Warumi 12:2, lazima tufanye nini ili kumpa Mungu ibada ya pekee?
20 Kumpenda na kumheshimu mtu, yampasa mmoja amjue yeye kama alivyo kwa kweli. Kumpa Mungu ibada ya pekee ambayo anastahili, lazima ujifunze Neno lake na “kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (Warumi 12:2) Jambo la muhimu si jinsi wanadamu watakavyo kumwabudu Mungu, bali jinsi Mungu atakavyo kuabudiwa.
21. Katika maneno ya Mwana wa Mungu mwenyewe, Mungu hutaka aabudiwe namna gani?
21 Kawaida za ibada ya kidini na “misaada kwa ibada” huenda zionekane zenye kupendeza machoni pa wale ambao huzitumia, lakini jinsi gani Mungu huzitazama? Bila shaka unataka kujua, kwa sababu unataka kuwa na kibali cha Mungu. Mwana wa Mungu mwenyewe hutuambia sisi kwamba “waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli.” (Yohana 4:23) Kwa mfano, je! matumizi ya sanamu, ni kuabudu “katika roho na kweli”? Je! inampendeza Mungu?
22. (a) Biblia, katika Kutoka 20:4, 5, husema nini juu ya sanamu za kidini? (b) Neno la Mungu husema nini kuonyesha kwamba matumizi ya sanamu kama “msaada” kwa ibada si sehemu ya ibada ya kweli?
22 Katika Kutoka 20:4, 5, katika mojawapo za Amri Kumi, Mungu mwenyewe husema: “Wewe hutajifanyia mwenyewe sanamu ya kuchonga au mfano wo wote wa kitu cho chote . . . wewe hutavipigia magoti wala kuvitumikia.” (The Catholic Jerusalem Bible) Watu fulani huona sanamu ya kidini kama “msaada” tu kwa kumwabudu Mungu kwa sababu wanaweza kuona na kuigusa sanamu. Lakini Mungu alimwongoza mtume Paulo kuandika: “Twaenenda kwa imani, si kwa kuona.” (2 Wakorintho 5:7) Mungu ni mwenye kusema kweli sana juu ya jambo. Yeye hutuambia kwamba matumizi ya sanamu si sehemu ya ibada ya kweli, bali kwamba sanamu za namna hiyo ni “uongo.” (Isaya 44:14-20; Zaburi 115:4-8) Hata ijapokuwa labda mtu atasema kwamba heshima inayopewa kwa sanamu ya kidini ni ndogo kuliko ile inayopewa kwa Mungu, Mungu mwenyewe husema kwamba yeye hatashiriki wo wote wa utukufu wake na sifa pamoja na sanamu za namna hiyo.—Isaya 42:8.
23. Tutazamapo huku na huku katika nyumba zetu, ni maneno gani ya mtume Yohana ambayo imetupasa tuyakumbuke?
23 Kwa upendo, mtume Yohana hutuonya sisi: “Jilindeni nafsi zenu na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Mbona usitazame huku na huku nyumbani mwako na kujiuliza mwenyewe kama unafanya hivi? (Kumbukumbu la Torati 7:25) Kwa kuleta maisha yako na ibada yako katika upatano na mapenzi ya upendo ya Yehova unaweza kupata baraka zake za milele.—1 Wakorintho 10:14.
24 Endelea kujifunza juu ya adhama ya Yehova na makusudi yake ya upendo, nawe utakua katika upendo kwake. Usiache kamwe siku ipite bila kumshukuru yeye kwa mambo mema ambayo unafurahia kwa sababu ya fadhili zake za upendo. Kwa kadiri unavyojifunza zaidi juu yake, kaza katika moyo wako muhimu wa uaminifu kwake kama Mungu mkuu wa ulimwengu wote. Kwa utii wa upendo kwake yeye, utajiweka mwenyewe katika njia iongozayo kwenye uzima wa milele.—Waefeso 4:23, 24; Zaburi 104:33-35.
[Maelezo ya Chini]
a Cyclopcedia of Biblical, Theological, and Ecclesiastical Literature, cha J. M’Clintock and J. Strong, Vol. II, ukur. 561.
b Karibu wenye kuamini katika utatu wameacha kutaja maneno ya “Baba, na, Neno, na Roho Mtakatifu: na watatu hawa ni umoja” yanayoonekana katika tafsiri fulani za Biblia katika 1 Yohana 5:7. Wataalamu wa maneno yenyewe hukubali kwamba maneno haya ni nyongeza ya uongo ya baadaye kwa maandishi ya awali yaliyoongozwa na roho ya Mungu.
24. Ikiwa kweli tunataka kukaribia karibu kwa Mungu, imetupasa tufanye nini?