Ishi Milele Katika Paradiso Duniani
Mungu awaahidi uhai wa milele wale ambao humheshimu. “Waadilifu wenyewe watamiliki dunia, nao watakaa milele juu yayo,” Neno lake latuhakikishia.—Zaburi 37:29, NW.
Hata hivyo, ili uhesabiwe miongoni mwa “waadilifu,” wewe wahitaji kufanya mengi zaidi ya kuwa na habari tu juu ya fundisho la Utatu. Wahitaji kufanya maendeleo katika maarifa juu ya Mungu. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia wewe, ikiwa hujaanza kupokea msaada huo. Andikia tu I.B.S.A. kwenye anwani ifaayo iliyoorodheshwa chini, ukiomba habari zaidi au kwamba mmoja wa Mashahidi wa Yehova aje nyumbani kwako ajifunze Biblia pamoja nawe kwa ukawaida bila malipo.