Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • si kur. 259-260
  • Kitabu cha Biblia Namba 63—2 Yohana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu cha Biblia Namba 63—2 Yohana
  • “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • YALIYOMO KATIKA WA YOHANA PILI
  • KWA NINI NI CHENYE MAFAA
  • Kataa Uasi wa Imani, Ambatana na Ile Kweli!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kitabu cha Biblia Namba 62—1 Yohana
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Kitabu cha Biblia Namba 64—3 Yohana
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
“Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
si kur. 259-260

Kitabu cha Biblia Namba 63—2 Yohana

Mwandikaji: Mtume Yohana

Mahali Kilipoandikiwa: Efeso, au karibu

Uandikaji Ulikamilishwa: c. (karibu 98) W.K.

1. Huenda Yohana wa Pili ikawa iliandikwa kwa nani?

BARUA ya pili ya Yohana ni fupi—ingeweza kuwa iliandikwa juu ya karatasi moja ya mafunjo—lakini imejaa maana. Imeelekezwa kwa “mama [bibi, NW] mteule na watoto wake.” Kwa kuwa “Kyria” (neno la Kigiriki la kusema “bibi”) lilikuwako wakati huo likiwa jina la matumizi ya kipekee wakati huo, wanachuo fulani wa Biblia wahisi kwamba ni mtu mwenye jina hilo aliyekuwa akiambiwa maneno hayo. Kwa upande mwingine, wengine hufikiri kwamba Yohana alikuwa akiandikia kundi fulani la Kikristo, akilirejezea kuwa “mama mteule.” Huenda hilo likawa lilifanywa ili kuvuruga wanyanyasaji. Ikiwa hivyo, salamu za “ndugu” (dada, NW) atajwaye katika mstari wa mwisho zingekuwa ni za washiriki wa kundi jingine. Hivyo basi barua hii ya pili haikukusudiwa iwe ya kuhusisha ujumla wa watu kama ile ya kwanza, kwa maana yaonekana wazi iliandikwa ama kwa mtu mmoja ama kwa kundi moja hasa.—Mst. 1.

2. (a) Ni uthibitisho gani uonyeshao kwamba mtume Yohana ndiye mwandikaji wa Yohana wa Pili? (b) Ni nini kionyeshacho kwamba barua hii iliandikwa katika au karibu na Efeso, 98 W.K. hivi, na ni nini huunga mkono uasilia wayo?

2 Hakuna sababu ya kutia shaka kwamba Yohana aliiandika barua hii. Mwandikaji ajiita “mzee.” Kwa uhakika hilo lapatana na Yohana si kwa sababu ya umri wake wa uzee tu bali pia kwa sababu, akiwa mmoja wa zile “nguzo” (Gal. 2:9) na mtume wa mwisho mwenye kubaki hai, yeye kwa kweli alikuwa “mzee” kikweli katika kundi la Kikristo. Alijulikana sana, na haingetakiwa kufanya utambulisho zaidi kwa ajili ya wasomaji wake. Pia uandikaji wake waonyeshwa na ufanani katika mtindo wa barua ya kwanza na Gospeli ya Yohana. Kama barua ya kwanza, barua ya pili yaonekana kuwa iliandikwa katika au karibu na Efeso, 98 W.K. hivi. Kwa habari ya Yohana wa Pili na wa Tatu, Cyclopedia ya McClintock na Strong yaeleza hivi: “Kutokana na ufanani wazo wa ujumla, twaweza kutunga fikira ya kwamba nyaraka hizo mbili ziliandikwa kutoka Efeso muda mfupi baada ya Waraka wa Kwanza. Zote mbili zatumika kwa visa kimoja kimoja vya mwenendo ambavyo kanuni zavyo zilikuwa zimeonyeshwa kikamili katika Waraka wa Kwanza.”a Katika kuunga mkono uasilia wayo, barua hii yanukuliwa na Irenaeus, wa karne ya pili, nayo ilikubaliwa na Clement wa Aleksandria, wa kipindi icho hicho.b Pia, barua za Yohana zimeorodheshwa katika Muratorian Fragment.

3. Kwa nini Yohana aliandika barua hii?

3 Kama ilivyokuwa kweli juu ya Yohana wa Kwanza, sababu ya barua hii ni ule ushambulizi wenye kufanywa na walimu bandia juu ya imani ya Kikristo. Yohana ataka kuonya wasomaji wake juu ya watu hao ili waweze kuwatambua na kukaa mbali nao, huku wakiendelea kutembea katika ile kweli, katika kupendana.

YALIYOMO KATIKA WA YOHANA PILI

4. Kwa nini Yohana aonya waziwazi juu ya kupendana, na ni lazima wale wajisukumao mbele zaidi ya fundisho la Kristo watendeweje?

4 Pendaneni; kataeni waasi-imani (Mist. 1-13). Baada ya kueleza upendo wake katika ile kweli kwa yule ‘mama mteule na watoto wake,’ Yohana ashangilia kwamba amepata baadhi yao wakitembea katika ile kweli, kama ilivyoamriwa na Baba. Aomba kwamba waonyeshane upendo kwa kuendelea kutembea kulingana na amri za Mungu. Kwa maana wadanganyaji na wapinga Kristo wameenda wakaingia katika ulimwengu, ambao hawamwungami Yesu Kristo kuwa anakuja katika mwili. Yeye ajisukumaye mbele zaidi ya fundisho la Kristo hana Mungu, bali yeye abakiye katika fundisho hili “ana Baba na Mwana pia.” Yeyote asiyeleta fundisho hili hapasi kupokewa katika nyumba zao, wala hapaswi hata kusalimiwa. Yohana ana mengi ya kuwaandikia, lakini badala ya kufanya hivyo atumainia kuja na kusema nao uso kwa uso, ili shangwe yao ipate ‘kuwa imetimizwa.’—Mist. 9, 12.

KWA NINI NI CHENYE MAFAA

5. (a) Ni hali gani iliyotokea katika siku ya Yohana ambayo imetokea pia katika nyakati za ki-siku-hizi? (b) Kama Yohana, sisi leo twaweza kuonyeshaje uthamini kwa ajili ya mwungamano wa kundi?

5 Yaonekana kwamba katika siku ya Yohana, kama vile ilivyo katika nyakati za ki-siku-hizi, kulikuwako watu fulani wasiotosheka kukaa na yale mafundisho yaliyo wazi na rahisi ya Kristo. Walitaka kitu fulani zaidi, kitu fulani ambacho kingetekenya ubinafsi wao, kitu fulani ambacho kingewakweza na kuwatia katika cheo kimoja na wanafalsafa wa kilimwengu, nao walikuwa na nia ya kuchafua na kugawanya kundi la Kikristo ili watimize makusudi yao ya ubinafsi. Yohana aliuthamini upatano wa kundi ambao hukaa katika upendo na katika fundisho lifaalo kwa mwungano pamoja na Baba na Mwana. Sisi twapaswa kuuthamini hivyo hivyo mwungamano wa kundi leo, hata kukataa kushirikiana au kuwapa salamu wale waasio imani na kufuata fundisho jingine zaidi ya lile lililopokewa kupitia Maandiko yaliyopuliziwa na Mungu. Kwa kuendelea kutembea kulingana na amri za Mungu, na katika kipimo kamili cha shangwe ipatikanayo katika ushirika wa kweli wa Kikristo, twaweza kuwa na uhakikishio wa kwamba “neema, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.” (Mst. 3) Kwa uhakika barua ya pili ya Yohana yakazia kubarikiwa kwa umoja huo wa Kikristo.

[Maelezo ya Chini]

a Chapa-mrudio ya 1981, Buku 4, ukurasa 955.

b New Bible Dictionary, hariri la pili, 1986, lililohaririwa na J. D. Douglas, ukurasa 605.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki