Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 33
  • Kutimiza Unabii wa Isaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutimiza Unabii wa Isaya
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • Kutimiza Unabii wa Isaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Atimiza Unabii wa Isaya
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Je, Ungeuzima Utambi Ufukao Moshi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • “Mteule Wangu, Ambaye Nafsi Yangu Imependezwa Naye”!
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 33

Sura 33

Kutimiza Unabii wa Isaya

BAADA ya Yesu kupata habari kwamba Mafarisayo na wafuasi wa chama cha Herode wanapanga kumwua, yeye na wanafunzi wake waondoka kwenda kwenye Bahari ya Galilaya. Huko umati mkubwa wa watu kutoka sehemu zote za Palestina, na hata kutoka nje ya mipaka yake, wammiminikia. Yeye aponya wengi na matokeo ni kwamba wote wenye magonjwa ya kuhuzunisha sana wasogelea wamguse.

Kwa sababu umati wa watu ni mkubwa sana, Yesu awaambia wanafunzi wake wamwekee mashua pale aendelea kuitumia. Kwa kuiendesha atoke ufuoni, anaweza kuuzuia umati wa watu hao wasimsonge. Anaweza kuwafundisha akiwa mashuani au kusafiri kwenye eneo jingine kandokando ya ufuo wa bahari ili kuwasaidia watu kule.

Mwanafunzi Mathayo aandika kwamba utendaji wa Yesu unatimiza “neno lililonenwa na nabii Isaya.” Halafu Mathayo anukuu maneno ya unabii ambao Yesu anatimiza:

“Tazama, mtumishi wangu niliyemteua; mpendwa wangu, moyo wangu uliyependezwa naye; nitatia roho yangu juu yake, naye atawatangazia Mataifa hukumu. Hatateta wala hatapaza sauti yake; wala mtu hatasikia sauti yake njiani. Mwanzi uliopondeka hatauvunja, wala utambi utokao moshi hatauzima, hata ailetapo hukumu ikashinda. Na jina lake Mataifa watalitumainia.”

Bila shaka, Yesu ndiye mtumishi mpendwa ambaye Mungu anakubali. Na Yesu anafahamisha wazi ni nini haki ya kweli, ambayo mapokeo ya dini bandia yanaifunika isionekane. Mafarisayo hawataki hata kwenda kusaidia mgonjwa siku ya Sabato kwa sababu wanatumia sheria ya Mungu kwa njia isiyo haki! Kwa kufahamisha wazi haki ya Mungu ni nini, Yesu anawaondolea watu mzigo wa mapokeo yasiyo ya haki, na kwa sababu hiyo, viongozi wa kidini wanajaribu kumwua.

Inamaanisha nini kwamba ‘hatateta, wala hatapaaza sauti yake ili asikiwe katika njia pana’? Wakati anapoponya watu, Yesu ‘awakataza sana wasimdhihirishe.’ Yeye hataki kujitangaza kwa makelele mengi katika barabara wala hataki habari zilizopotoshwa zipitishwe kwa msisimuko kutoka kinywa kimoja mpaka kinywa kingine.

Pia, Yesu awapelekea ujumbe wenye faraja wale ambao kwa njia ya mfano ni kama mwanzi uliopondwa, walioinama na kugongwa katika sehemu ya chini ya nyayo. Wao ni kama utambi utokao moshi, ambao mwali wao wa mwisho u karibu kuzimika. Yesu hauvunji mwanzi uliopondeka wala hauzimi utambi utokao moshi. Bali kwa wororo na upendo, awainua wapole kwa ustadi. Kwa kweli, Yesu ndiye ambaye mataifa waweza kutumainia! Mathayo 12:15-21; Marko 3:7-12; Isaya 42:1-4.

▪ Yesu anafahamishaje wazi maana ya haki, bila kuteta wala kupaaza sauti katika njia pana?

▪ Ni nani walio kama mwanzi uliopondeka na utambi, na Yesu anawatendeaje?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki