Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gt sura 123
  • “Tazama, Mtu Huyu!”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Tazama, Mtu Huyu!”
  • Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Habari Zinazolingana
  • “Tazama, Mtu Huyu!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Pilato Asema: “Tazama! Mwanamume!
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Pontio Pilato Alikuwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kutoka kwa Pilato Mpaka kwa Herode na Kurudi Tena
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
gt sura 123

Sura 123

“Tazama, Mtu Huyu!”

KWA kuvutiwa na utulivu wa Yesu na akitambua kwamba hana kosa, Pilato afuatia njia nyingine ya kumwachilia. “Kwenu kuna desturi,” aambia umati wa watu wale, “ya mimi kuwafungulia mtu mmoja wakati wa Pasaka [Sikukuu ya Kupitwa, NW].”

Baraba, muuaji mwenye sifa mbaya, amefungwa pia akiwa mfungwa-gereza, hivyo basi Pilato auliza: “Mnataka niwafungulie yupi? yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo?”

Kwa kuvutwa na usadikisho wa makuhani wakuu ambao wamewachochea, watu waomba Baraba aachiliwe lakini Yesu auawe. Bila kukata tamaa, Pilato ajibu, akiuliza tena: “Mnataka niwafungulie yupi katika hawa wawili?”

“Baraba,” wapaaza sauti.

“Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo?” Pilato auliza kwa kufadhaika.

Kwa mngurumo mmoja wenye kishindo cha kuziba masikio, wajibu: “Asulibiwe [acha atundikwe, NW]”! “Msulibishe! Msulibishe [mtundike, NW]!”

Kwa kujua kwamba wadai kifo cha mtu asiye na hatia, Pilato asihi hivi: “Kwa sababu gani? huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi [kumwadhibu] nitamfungua.”

Japo majaribio yake, umati huo wenye hasira, kwa kuchochewa na viongozi wao wa kidini, waendelea kupiga kelele: “Asulibiwe [atundikwe, NW]”! Kwa kuchochewa sana na makuhani, umati wataka damu. Na ebu fikiri, siku tano tu kabla ya hapo, wengine wao labda walikuwa miongoni mwa wale waliokaribisha Yesu kuingia Yerusalemu akiwa Mfalme! Muda wote huu, wanafunzi wa Yesu, ikiwa wapo, wabaki kimya na bila kujitokeza wazi.

Pilato, akiona kwamba maneno yake ya kusihi hayafai kitu, bali kunatokea fujo, achukua maji na kunawa mikono mbele ya ule umati, na kusema: “Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe.” Hapo watu hao wajibu: “Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.”

Hivyo basi, kulingana na madai yao—naye akitaka kufurahisha umati huo kuliko kufanya analojua kuwa haki—Pilato awafungulia Baraba. Achukua Yesu na kuagiza avuliwe mavazi halafu apigwe mijeledi. Huku hakukuwa kupiga viboko vya kawaida. The Journal of the American Medical Association linaeleza zoea la Kiroma la kupiga mijeledi:

“Chombo cha kawaida kilikuwa kiboko kifupi (flagramu au flagelamu) chenye kamba kadhaa moja moja za ngozi-kavu au zilizosokotwa zikiwa na marefu mbalimbali, ambamo vipande vidogo vya chuma au vipande vyenye ncha kali vya mifupa ya kondoo vilifungwa kwa kuachana. . . . Askari Waroma walipopiga-piga mgongo wa mfungwa kwa nguvu kamili, vile vipande vya chuma vya mfiringo vingesababisha michubuo ya kina kirefu, na zile kamba za ngozi-kavu na mifupa ya kondoo zingekata ndani ya ngozi na sehemu zilizo chini ya ngozi ya mwili. Halafu, kupigwa mijeledi kulipoendelea, miraruko ya ngozi ingeingia chini ya nyuzi za mnofu chini kwenye mifupa ya mwili na kutokeza nyuzinyuzi zenye kuning’inia za mnofu wenye kutoka damu.”

Baada ya kupigwa huko kenye mateso makali, Yesu apelekwa ndani ya jumba la gavana, na kikundi kizima cha askari kinaitwa kikusanyike. Humo askari warundika matukano zaidi juu yake kwa kusokota taji la miiba na kulisukuma juu ya kichwa chake. Watia mwanzi katika mkono wake wa kulia, nao wamvika vazi la zambarau, namna inayovaliwa na watu wa kifalme. Halafu wamwambia hivi kwa dhihaka: “Salamu, Mfalme wa Wayahudi!” Pia, wamtemea mate na kumpiga kofi usoni. Wakichukua ule mwanzi imara kutoka mkononi mwake, wautumia kumpiga kichwani, hiyo ikizidi kuisukuma ndani ya ngozi ya kichwa chake ile miiba iliyochongoka ya “taji” lake lenye kumshushia heshima.

Fahari na imara ya kusifika ambayo Yesu anayo katika kuelekeana na kutendewa vibaya huko inavutia sana Pilato hivi kwamba inamsukuma kufanya jaribio jingine la kumwachilia. “Mtu huyu namleta nje kwenu, mpate kufahamu ya kuwa mimi sioni hatia yo yote kwake,” awaambia umati wa watu. Inawezekana kuwa awazia kwamba sura ya hali ya kuteswa-teswa kwa Yesu italainisha mioyo yao. Yesu anapokuwa amesimama mbele ya watu hao wenye fujo wasio na moyo wa huruma, akiwa amevaa taji la miimba na lile vazi la nje la zambarau na huku uso wake wenye kutoka damu ukiwa na maumivu, Pilato atangaza: “Tazama, mtu huyu!”

Ingawa amechubuliwa na kutwangwa, hapa amesimama mtu mwenye kutokeza zaidi katika historia yote, kwa kweli binadamu wa kutokeza zaidi aliyepata kuishi! Ndiyo, Yesu aonyesha fahari ya unyamavu na utulivu unaoonyesha ukuu ambao hata Pilato alazimika kuukubali wazi, kwa maana inaonekana maneno yake ni mchanganyiko wa heshima na huruma pia. Yohana 18:39–19:5; Mathayo 27:15-17, 20-30; Marko 15:6-19; Luka 23:18-25.

▪ Pilato ajaribu kwa njia gani kufanya Yesu aachiliwe?

▪ Pilato ajaribuje kujiondolea daraka?

▪ Ni nini kinachohusika katika kupigwa mijeledi?

▪ Yesu adhihakiwaje baada ya kupigwa mijeledi?

▪ Ni jaribio gani zaidi ambalo Pilato afanya ili kumwachilia Yesu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki