Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • be funzo 28 uku. 179-uku. 180 fu. 8
  • Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi
  • Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Habari Zinazolingana
  • Kuzungumza kwa njia ya kawaida
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Ufasaha
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Sema Lililo “Jema kwa Ajili ya Kujenga”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
Pata Habari Zaidi
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
be funzo 28 uku. 179-uku. 180 fu. 8

SOMO LA 28

Kutoa Hotuba kwa Njia ya Maongezi

Unahitaji kufanya nini?

Unahitaji kutoa hotuba kama unavyozungumza kwa kawaida lakini kwa namna inayofaa wasikilizaji.

Kwa Nini Ni Muhimu?

Hotuba inayotolewa kwa njia inayofaa ya maongezi hustarehesha wasikilizaji na hufanya waweze kukubali mambo unayosema.

KWA kawaida watu hustarehe wanapozungumza na marafiki. Maneno yao yanatiririka tu. Watu wengine ni wachangamfu sana ilhali wengine huwa kimya. Hata hivyo, maongezi ya kawaida kama hayo huvutia.

Lakini unapokutana na mtu ambaye humjui si vizuri kuzungumza naye kana kwamba unamjua sana wala kuzungumza naye kwa njia inayokosa adabu. Katika jamii nyingi mazungumzo yote kati ya watu ambao hawajuani huanza kwa njia rasmi sana. Lakini baada ya salamu za heshima, kwa busara unaweza kuanza kuzungumza kwa njia ya kawaida ya maongezi.

Tahadhari pia unapotoa hotuba jukwaani. Kutoa hotuba kwa njia ya kizembe kutafanya mkutano wa Kikristo ukose heshima na watu wakose kuthamini mambo unayosema. Katika jamii fulani unapaswa kusema maneno fulani unapozungumza na mtu anayekuzidi umri, mwalimu, ofisa fulani, au mzazi. (Ebu ona maneno yanayotumiwa katika Matendo 7:2 na 13:16.) Maneno tofauti-tofauti hutumiwa kumwita mume au mke au rafiki unayempenda. Ingawa hatupaswi kuongea kwa njia rasmi sana jukwaani, tunapaswa kuongea kwa heshima.

Hata hivyo, kuna mambo ambayo yanaweza kumfanya mtu atoe hotuba bila kubadilikana. Mojawapo ya sababu hizo ni muundo wa sentensi. Tatizo huzuka msemaji anapojaribu kurudia maneno yaleyale kama yalivyoandikwa katika vichapo. Kwa kawaida watu huzungumza kwa njia tofauti na jinsi maneno yanavyoandikwa. Ni kweli kwamba kwa kawaida tunatayarisha hotuba kupitia habari iliyochapwa. Labda muhtasari uliochapwa ndio msingi wa hotuba. Lakini ikiwa unazungumza kana kwamba unasoma kichapo au ikiwa unasoma moja kwa moja muhtasari wa hotuba, inaelekea hutatoa hotuba kwa njia ya maongezi. Ili utoe hotuba kwa njia ya maongezi, tumia maneno yako mwenyewe na kuepuka sentensi ngumu-ngumu.

Jambo jingine ni kubadili-kubadili mwendo wako wa kuzungumza. Usemi baridi-baridi na ulio rasmi kupita kiasi husababishwa na maneno yanayofuatana kwa mwendo uleule mmoja usiobadilika. Katika mazungumzo ya kawaida, watu hubadili-badili mwendo na kutua-tua kwa njia tofauti-tofauti.

Bila shaka, unapohutubia watu wengi unapaswa kuhutubu kwa njia ya maongezi na kwa sauti ya juu, kwa mkazo, na kwa shauku ili waendelee kukusikiliza kwa makini.

Ili uzungumze kwa njia ya maongezi inayofaa utumishi, unahitaji kuwa na mazoea ya kuzungumza vizuri kila siku. Haimaanishi kwamba ni lazima uwe na elimu ya juu. Lakini ni vizuri uwe na mazoea mazuri ya usemi ambayo yatafanya wengine wakusikilize kwa heshima. Basi, ukiwa na mambo hayo akilini, ebu ona kama unahitaji kufanyia kazi sifa zifuatazo katika mazungumzo ya kawaida:

  1. Epuka lugha chafu au matusi kwa kupatana na shauri la Wakolosai 3:8. Kwa upande mwingine, si vibaya kutumia lugha inayotumiwa kwa kawaida inayopatana na lugha sanifu ingawa si rasmi.

  2. Jifunze kutumia maneno yanayoonyesha wazi jambo unalomaanisha.

  3. Uwe na mazoea ya kusema jambo unalotaka watu wakumbuke kwa njia inayoeleweka wazi na kwa maneno rahisi.

JINSI YA KUKUZA SIFA HII

  • Uwe na maoni mazuri juu ya wasikilizaji. Waone kama marafiki, lakini usiwazoee kupita kiasi. Waheshimu.

  • Zungumza bila kutazama sana maandishi. Usitumie miundo ileile ya maneno yaliyo katika kichapo. Jieleze kwa maneno yako mwenyewe. Tumia sentensi fupi-fupi, na ubadili-badili mwendo wako.

  • Kazia akili hamu yako ya kufundisha. Zungumza kwa hisia. Jambo muhimu ni ujumbe, wala si jinsi watu wanavyokuona.

  • Boresha mazungumzo yako ya kawaida. Tumia hatua kwa hatua madokezo yanayoonyeshwa katika ukurasa huu.

MAZOEZI: Chunguza mazoea yako ya kuzungumza. Fanyia kazi mambo matano ambayo yameorodheshwa hapo juu, ukishughulikia jambo moja kwa wakati mmoja siku kutwa. Ukifanya kosa lolote, angalau rudia tena wazo hilo akilini mwako kwa njia sahihi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki