Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • be funzo 37 uku. 212-uku. 214 fu. 5
  • Kukazia Mambo Makuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukazia Mambo Makuu
  • Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Habari Zinazolingana
  • Kukazia Mambo Makuu
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kutayarisha Muhtasari
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Pitia Mambo Makuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
  • Kutumia Habari Ambazo Umepewa
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Pata Habari Zaidi
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
be funzo 37 uku. 212-uku. 214 fu. 5

SOMO LA 37

Kukazia Mambo Makuu

Unahitaji kufanya nini?

Panga hotuba yako na uitoe kwa kukazia vizuri mambo makuu.

Kwa Nini Ni Muhimu?

Kunasaidia kukumbuka mambo, na hivyo basi kuwawezesha watu kutafakari na kuona jinsi ya kuyatumia maishani.

MAMBO makuu ya hotuba ni yapi? Hayo si mambo yanayopendeza yanayotajwa kwa ufupi tu. Hayo ni mawazo muhimu ambayo yanafafanuliwa kwa urefu. Ni yale mawazo muhimu yanayokusaidia kutimiza kusudi lako.

Njia bora ya kukazia mambo makuu ni kuchagua habari na kuzipanga kwa hekima. Kwa kawaida unapofanya utafiti, unakusanya mambo mengi kuliko unayoweza kutumia. Unawezaje kujua mambo muhimu?

Kwanza, wafikirie wasikilizaji. Je, kwa ujumla hawafahamu habari unayozungumzia, au wanaifahamu sana? Je, wengi wao wanakubaliana na maoni ya Biblia kuihusu, au kuna wengine wanaotilia shaka? Wasikilizaji wanapata magumu gani katika maisha yao ya kawaida wanapojaribu kufuata kanuni za Biblia zinazohusu habari hiyo? Pili, hakikisha kwamba unafahamu kabisa kusudi la kutoa hotuba hiyo. Tumia njia hizo mbili kuchunguza habari hiyo na kubaki na mambo ambayo ni muhimu kabisa.

Kama umepewa muhtasari ambao una kichwa kikuu na mambo makuu, uufuate kwa makini. Lakini, hotuba yako itafaidi kwelikweli ukikumbuka mambo ambayo yametajwa hapo juu unapofafanua kila jambo kuu. Ikiwa hotuba hiyo haina muhtasari, ni juu yako kuchagua mambo makuu.

Ni rahisi kutoa hotuba ikiwa unakumbuka vizuri mambo makuu na umepanga vizuri habari chini ya mambo hayo. Hotuba hiyo inaweza kuwafaidi sana wasikilizaji.

Njia za Kupanga Hotuba. Kuna mbinu kadhaa unazoweza kutumia kupanga hotuba. Unapozidi kuzifahamu, utaona kwamba mbinu kadhaa zinaweza kutumika vizuri ikitegemea kusudi lako.

Mbinu inayotumika mara nyingi ni ile ya kugawanya hotuba kwa vichwa tofauti-tofauti. (Kila jambo kuu ni muhimu kwa sababu linafanya wasikilizaji waelewe zaidi hotuba hiyo au linakusaidia kutimiza kusudi lako.) Mbinu nyingine ni ile ya kuzungumzia matukio kulingana na jinsi yalivyofuatana. (Kwa mfano, matukio ya kabla ya Furiko yanaweza kufuatwa na matukio yaliyotangulia uharibifu wa Yerusalemu mwaka wa 70 W.K., nayo yanaweza kufuatwa na matukio ya siku zetu.) Mbinu ya tatu ni kutaja kisababishi cha jambo na matokeo yake. (Unaweza kuzungumzia kwanza kisababishi au matokeo. Kwa mfano, kwanza unaweza kutaja hali ya wakati huu, matokeo yake, kisha uonyeshe kisababishi.) Mbinu ya nne ni kulinganisha hali zinazotofautiana. (Unaweza kulinganisha baya na jema au mambo yanayofaa na yasiyofaa.) Nyakati nyingine unaweza kutumia zaidi ya mbinu moja katika hotuba.

Stefano alipowekewa mashtaka bandia mbele ya Sanhedrini ya Kiyahudi, alitoa hotuba yenye nguvu iliyoorodhesha matukio na jinsi yalivyofuatana. Unapoisoma hotuba hiyo katika Matendo 7:2-53, utaona kwamba alichagua kwa makini mambo aliyotaja. Kwanza, Stefano alihakikisha anasimulia historia ambayo wasikilizaji hawangeweza kukanusha. Kisha akataja kwamba ingawa Yosefu alikataliwa na ndugu zake, Mungu alimtumia kuandaa ukombozi. Kisha akaonyesha kwamba Wayahudi hawakumtii Musa ambaye Mungu alikuwa akimtumia. Alimalizia kwa kukazia kwamba roho ile iliyoonyeshwa na Wayahudi wa vizazi vilivyopita ilionyeshwa pia na wale waliofanya Yesu Kristo auawe.

Usitumie Mambo Makuu Mengi Mno. Ni mambo machache muhimu ambayo huhitajika kufafanua kichwa chochote kikuu. Kwa kawaida mambo hayo hayazidi matano. Ndivyo ilivyo iwe unazungumza kwa dakika 5, dakika 10, dakika 30, au kwa muda mrefu. Usijaribu kukazia mambo mengi mno. Wasikilizaji wanaweza kukumbuka mawazo machache tu katika hotuba moja. Na kadiri hotuba inavyokuwa ndefu ndivyo mambo makuu yanavyopasa kuwa wazi zaidi.

Hata iwe unatumia mambo mangapi makuu, hakikisha unafafanua kila jambo vizuri. Wape wasikilizaji muda wa kutosha wa kuchunguza kila jambo kuu ili walielewe vizuri.

Jaribu kutoa hotuba kwa njia rahisi. Nyakati nyingine kutoa hotuba kwa njia rahisi hakutegemei kiasi cha habari. Ikiwa umeweka pamoja mawazo yako katika vichwa vikuu vichache na unafafanua kila kichwa baada ya kingine, wasikilizaji watafuata hotuba hiyo kwa urahisi na kuikumbuka.

Kazia Mambo Makuu. Ukipanga vizuri hotuba, haitakuwa vigumu kukazia tena mambo makuu unapoitoa.

Njia kuu ya kukazia jambo ni kuonyesha uthibitisho wake, maandiko, na mambo mengine kwa njia ya kwamba mambo hayo yote yanakazia wazo kuu na kulidhihirisha. Mambo yote ya ziada yanapaswa kufanya jambo kuu liwe wazi, kulithibitisha, au kulidhihirisha. Usiongeze mambo mengine ambayo hayahusiki kwa sababu tu yanapendeza. Unapozungumzia mambo ya ziada, onyesha wazi jinsi yanavyohusiana na jambo kuu linalohusika. Usiache wasikilizaji wakisie-kisie uhusiano ulioko kati ya jambo kuu na mambo ya ziada. Unaweza kuonyesha uhusiano huo kwa kurudia mara kwa mara maneno makuu yanayoonyesha wazo kuu au yanayorudia jambo kuu.

Wasemaji wengine hukazia mambo makuu kwa kuyaorodhesha. Ingawa hiyo ni njia moja ya kukazia mambo makuu, haipasi kutumiwa badala ya ile njia ya kuchagua habari kwa makini na kuitoa kwa mfuatano mzuri.

Unaweza kutaja jambo kuu kwanza kabla ya kuzungumzia mambo yanayoliunga mkono. Hiyo itawasaidia wasikilizaji kufahamu faida ya mambo yanayofuata, na pia itakazia jambo kuu. Unaweza kukazia jambo kwa kulirudia baada ya kulifafanua kabisa.

Katika Huduma ya Shambani. Kanuni ambazo zimetajwa hapa hazihusu hotuba peke yake bali pia mazungumzo yetu katika huduma ya shambani. Unapofanya matayarisho, fikiria jambo lolote kuu ambalo watu wa eneo hilo wanafikiria. Chagua kichwa kikuu ambacho kitakuwezesha kuonyesha jinsi ambavyo tumaini la Biblia litakavyorekebisha hali hiyo. Unaweza kuchagua mambo makuu mawili ya kufafanua kichwa hicho. Chagua maandiko ambayo utatumia kutegemeza mambo hayo. Kisha panga jinsi utakavyoanzisha mazungumzo. Matayarisho kama hayo hukuwezesha kubadilikana kulingana na mazungumzo. Pia yatakusaidia kuwaambia watu jambo ambalo watakumbuka.

JINSI YA KUFAULU

  • Kabla ya kuchagua mambo makuu, fikiria mambo ambayo wasikilizaji wanajua kuhusu hotuba hiyo na ufahamu kusudi la hotuba yako. Kumbuka mambo hayo unapopanga hotuba.

  • Onyesha wazi uhusiano uliopo kati ya uthibitisho, maandiko, habari za ziada na wazo kuu ambalo linategemezwa na mambo hayo.

  • Kazia kila jambo kuu. Unaweza kufanya hivyo kwa kuyaorodhesha, kwa kutaja kila jambo kuu kabla ya kulifafanua, au kwa kurudia jambo kuu baada ya kulifafanua.

MAZOEZI: Pitia Funzo la Mnara wa Mlinzi la juma hili. Jaribu kutambua mambo makuu kupitia vichwa vidogo vyenye maandishi mazito na maswali yaliyo katika sanduku. Unaweza kufaidika ukifanya hivyo kila juma.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki