Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • th somo la 14 uku. 17
  • Kukazia Mambo Makuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kukazia Mambo Makuu
  • Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Habari Zinazolingana
  • Kukazia Mambo Makuu
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutayarisha Muhtasari
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kufafanua Kichwa Kikuu
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Pitia Mambo Makuu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
Pata Habari Zaidi
Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
th somo la 14 uku. 17

SOMO LA 14

Kukazia Mambo Makuu

Andiko lililotajwa

Waebrania 8:1

MUHTASARI: Wasaidie wasikilizaji wafuatane na hotuba yako, na uweke wazi jinsi kila jambo kuu linavyohusiana na kichwa kikuu na jambo unalotaka kufundisha.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Uwe na lengo. Jiulize, je, hotuba hii imekusudiwa kuwashauri, kuwasadikisha, au kuwachochea wasikilizaji? Kisha uitoe kulingana na kusudi lake. Hakikisha kila jambo kuu linazungumziwa kwa njia itakayokusaidia kutimiza lengo lako.

    Dokezo linalofaa

    Jiulize hivi: ‘Huenda wasikilizaji wangu wakawa wanajiuliza au kupinga mambo gani kuhusu habari hii? Huenda wakauliza maswali hayo au kutokeza vipingamizi hivyo kwa mpangilio gani?’ Kisha panga habari yako kwa mpangilio huohuo ili wasikilizaji wako wafuatane nawe, waelewe, na kukubali habari unayowaeleza.

  • Kazia kichwa kikuu katika hotuba yako. Rejelea kichwa kikuu katika hotuba yako yote kwa kurudia maneno makuu ya kichwa hicho au kwa kutumia maneno yanayofanana na hayo.

  • Fanya mambo makuu yawe wazi na rahisi. Chagua mambo makuu yanayohusiana na kichwa kikuu tu na ambayo utaweza kuyatumia kufundisha kwa wakati uliopangiwa. Usiwe na mambo mengi makuu. Taja kila jambo kuu waziwazi. Baada ya kuzungumzia jambo moja tua kidogo kabla ya kuanza kuzungumzia jambo kuu linalofuata. Onyesha uhusiano uliopo kati ya jambo kuu ambalo umemaliza kuzungumzia na linalofuata.

    Dokezo linalofaa

    Unaweza kutaja mambo makuu katika utangulizi wako ili wasikilizaji wafuatane nawe au urudie kuyataja katika umalizio ili kuwasaidia kuyakumbuka.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki