Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • T-26 kur. 1-2
  • Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?
  • Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Uisome Biblia?
  • Msaada wa Kuielewa Biblia
  • Je, U Tayari Kutumia Wakati Kila Juma Kuielewa Biblia?
  • Unaalikwa Kujifunza
  • Msaada wa Kuielewa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Mpango wa Kujifunza Biblia kwa Ajili ya Watu Wote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Biblia na Wewe
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Lishike kwa Mkazo Neno la Mungu
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
Pata Habari Zaidi
Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?
T-26 kur. 1-2

Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?

Kwa Nini Uisome Biblia?

BIBLIA ni tofauti na kitabu kingine chochote kwa sababu ina mafundisho yenye upendo kutoka kwa Mungu. (1 Wathesalonike 2:13) Iwapo unatumia yale ambayo Biblia hufundisha, utanufaika sana. Utampenda Mungu zaidi na utakuwa na ukaribu naye, ambaye ni Mpaji wa “kila zawadi njema na kila upaji mkamilifu.” (Yakobo 1:17) Utapata kujua jinsi ya kumfikia kwa sala. Wakati wa matatizo, unaweza kupata msaada wa Mungu. Ukiishi kupatana na viwango ambavyo vimeelezwa katika Biblia, Mungu atakupa uhai wa milele.—Waroma 6:23.

Biblia ina kweli zinazoweza kutuelimisha. Wale wanaopata ujuzi wa Biblia wanaacha imani zisizo za kweli ambazo zinashikiliwa na watu wengi sana. Kwa mfano, kujua ukweli kuhusu kinachotupata tunapokufa hutuondolea hofu kwamba wafu wanaweza kutudhuru au kwamba watu wetu wa ukoo na marafiki waliokufa wanateseka. (Ezekieli 18:4) Mafundisho ya Biblia juu ya ufufuo hufariji wale waliofiwa na wapendwa wao. (Yohana 11:25) Kujua ukweli juu ya malaika waovu hutufanya tuwe macho kuhusiana na hatari za kuwasiliana na roho na hutusaidia kuelewa ni kwa nini kuna matatizo mengi sana duniani.

Kanuni za Mungu zinazopatikana katika Biblia hutuonyesha jinsi ya kuishi maisha yenye kutunufaisha kimwili. Kwa mfano, kuwa na ‘kiasi katika mazoea’ hutusaidia kuwa na afya njema. (1 Timotheo 3:2) Kwa ‘kujisafisha wenyewe kila unajisi wa mwili na wa roho,’ tunaepuka kudhuru afya yetu. (2 Wakorintho 7:1) Pia, kutumia ushauri wa Mungu unaopatikana katika Biblia hutusaidia tuwe wenye furaha katika ndoa na wenye kujiheshimu.—1 Wakorintho 6:18.

Ukitumia Neno la Mungu, utakuwa mtu mwenye furaha zaidi. Ujuzi wa Biblia hutusaidia kupata amani ya akili na uradhi na hutupa tumaini. Hutusaidia kusitawisha sifa zenye kuvutia kama huruma, upendo, shangwe, amani, fadhili, na imani. (Wagalatia 5:22, 23; Waefeso 4:24, 32) Sifa hizo hutusaidia tuwe waume au wake wazuri, baba au mama wazuri, wana au binti wazuri.

Je, umewahi kufikiria yale yatakayotokea wakati ujao? Unabii wa Biblia hutusaidia kujua tunaishi katika kipindi muhimu katika historia ya wanadamu. Unabii huo unaeleza sio tu hali ya ulimwengu leo bali pia unaonyesha kwamba hivi karibuni Mungu atageuza dunia iwe paradiso.—Ufunuo 21:3, 4.

Msaada wa Kuielewa Biblia

Labda umejaribu kusoma Biblia lakini ukaona kwamba ni vigumu kuielewa. Labda hujui ni wapi katika Biblia unapoweza kupata majibu ya maswali yako. Ikiwa ndivyo, basi si wewe peke yako uliye na tatizo hilo. Sote tunahitaji kusaidiwa ili kuelewa Neno la Mungu. Mashahidi wa Yehova katika nchi zipatazo 235, hutoa mafundisho ya Biblia bila malipo kwa watu wengi. Watafurahia kukusaidia pia.

Kwa kawaida inakuwa vizuri kuisoma Biblia hatua kwa hatua, ukianza na mafundisho ya msingi. (Waebrania 6:1) Unapoendelea kujifunza, utakuwa na uwezo wa kula “chakula kigumu”—yaani, kweli nzito zaidi. (Waebrania 5:14) Biblia ndiyo chanzo cha kweli hizo. Vichapo vinavyotegemea Biblia, kama vile broshua Mungu Anataka Tufanye Nini?, vitakusaidia kuelewa Maandiko yanayozungumzia habari mbalimbali.

Je, U Tayari Kutumia Wakati Kila Juma Kuielewa Biblia?

Kwa kawaida, funzo la Biblia linaweza kupangwa wakati na mahali panapokufaa. Wengi hujifunzia nyumbani kwao wenyewe. Wengine hata hujifunza kupitia simu. Funzo hilo sio kama mafunzo ya darasani yenye watu wengi, bali ni mpango wa kibinafsi unaorekebishwa ufaane na hali zako, kutia ndani kiwango cha ujuzi na elimu yako. Hakuna mitihani, na hutaaibishwa. Maswali yako ya Biblia yatajibiwa, na utajifunza jinsi ya kumkaribia Mungu.

Huhitaji kulipia funzo hilo la Biblia. (Mathayo 10:8) Hilo hutolewa bila malipo kwa watu wa dini zote na hata wale wasio na dini lakini wanaopendezwa kikweli na kujua Neno la Mungu zaidi.

Ni nani wawezao kushiriki mazungumzo hayo? Familia yako yote na yeyote kati ya marafiki wako ambaye utapenda kualika. Mazungumzo hayo yanaweza kufanywa nawe peke yako ikiwa unataka hivyo.

Wengi hutenga muda wa saa moja kila juma ili kujifunza Biblia. Ikiwa unaweza kupata muda mwingi zaidi au hata ikiwa muda unaoweza kupata kila juma ni mfupi, Mashahidi watakuwa tayari kukusaidia.

Unaalikwa Kujifunza

Tunakuomba uwasiliane na Mashahidi wa Yehova. Njia moja ya kufanya hivyo ni kuandika barua ukitumia anwani iliyo hapa chini. Mipango itafanywa ili mtu fulani aongoze funzo la Biblia la nyumbani pamoja nawe.

□ Nitumieni nakala ya broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Onyesha lugha unayotaka

□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.

Isipokuwa imeonyeshwa vingine, manukuu ya Maandiko ya Kiebrania ni kutoka katika Union Version ya Kiswahili chapa ya 1994, na manukuu ya Maandiko ya Kigiriki ni kutoka katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki