Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 8-9
  • Kutoka Misri Hadi Nchi Ya Ahadi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoka Misri Hadi Nchi Ya Ahadi
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • B3 Safari ya Kutoka Misri
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Israeli Na Mataifa Yaliyolizunguka
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Wayahudi Waathiriwa Na Utawala Wa Wagiriki Na Waroma
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Ukristo Waenea Katika Nchi Nyingine
    ‘Ona Nchi Nzuri’
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 8-9

Kutoka Misri Hadi Nchi Ya Ahadi

KILA mahali watu wanajua kuhusu safari ya Waisraeli ya kutoka Misri. Lakini Musa na watu wa Mungu wangetazamia nini baada ya kuvuka Bahari Nyekundu? Walielekea wapi, nao walifikaje kwenye Mto Yordani na kuingia Nchi ya Ahadi?

Njia Ambayo Waisraeli Walipitia

Lengo lao lilikuwa kufika nchi ya Kanaani. Hata hivyo, Musa hakufuata njia fupi zaidi, yaani umbali wa kilometa 400 hivi kupitia pwani yenye mchanga, njia ambayo ingewaelekeza moja kwa moja hadi Ufilisti, eneo la adui. Wala hawakuvuka eneo kubwa la Rasi ya Sinai lililokuwa uwanda wenye changarawe na mawe ya chokaa, na uliokuwa pia na ukame na joto kali. Badala yake, Musa aliwaongoza watu kuelekea kusini hadi kwenye pwani tambarare. Kwanza walipiga kambi huko Mara ambapo Yehova alifanya maji machungu yawe matamu.a Baada ya kuondoka Elimu, watu walilalamika kuhusu chakula; Mungu akawapa kware, kisha mana. Walipofika Refidimu, watu walilalamika tena kuhusu maji, wakawashinda Waamaleki waliowashambulia, naye baba-mkwe wa Musa akamhimiza atafute msaada kutoka kwa wanaume wanaostahili.—Kut, sura 15-18.

Kisha Musa akawaongoza Waisraeli hadi milima iliyokuwa kusini kabisa, na wakapiga kambi kwenye Mlima Sinai. Wakiwa huko, watu wa Mungu walipewa Sheria, wakajenga tabenakulo, na kutoa dhabihu. Katika mwaka wa pili, walielekea kaskazini kupitia ‘nyika kuu na yenye kutia woga’ hadi Kadeshi (Kadesh-barnea), safari ambayo huenda ilichukua muda wa siku 11. (Kum 1:1, 2, 19; 8:15) Watu hao walitangatanga nyikani kwa miaka 38 kwa sababu ya woga uliowapata baada ya kupokea habari mbaya zilizoletwa na wale wapelelezi kumi. (Hes 13:1–14:34) Walipiga kambi katika sehemu mbalimbali kama vile Abrona na Esion-geberi, kisha wakarudi tena Kadeshi.—Hes 33:33-36.

Walipokaribia Nchi ya Ahadi, Waisraeli hawakuelekea moja kwa moja kaskazini. Walizunguka kandokando ya eneo la kati la Edomu na kupanda juu kupitia “barabara ya mfalme,” au Barabara Kuu ya Mfalme. (Hes 21:22; Kum 2:1-8) Haikuwa rahisi kwa taifa zima lenye watoto, wanyama, na mahema kupitia njia hiyo. Iliwabidi kuteremka kwa kufuata njia iliyojipinda-pinda na kupanda tena makorongo yenye miinuko mikali, yaani, Zeredi na Arnoni (yenye kina cha meta 520 hivi).—Kum 2:13, 14, 24.

Hatimaye, Waisraeli walifika Mlima Nebo. Miriamu alikufa huko Kadeshi, naye Haruni akafa kwenye Mlima Hori. Musa naye alikufa mahali ambapo angeweza kuona nchi aliyotamani kuingia. (Kum 32:48-52; 34:1-5) Yoshua alipewa jukumu la kuwaongoza Waisraeli hadi nchi hiyo, na hivyo kumaliza safari iliyoanza miaka 40 mapema.—Yos 1:1-4.

[Maelezo ya Chini]

a Haijulikani kambi nyingi zilikuwa mahali gani hususa.

[Sanduku katika ukurasa wa 8]

VITABU VYA BIBLIA TANGU WAKATI HUO:

Mwanzo

Kutoka

Mambo ya Walawi

Hesabu

Kumbukumbu la Torati

Ayubu

Zaburi (sehemu)

[Ramani katika ukurasa wa 9]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Njia Ambayo Waisraeli Walipitia

Njia ya Wafanyabiashara

A7 MISRI

A5 Ramesesi?

B5 Sukothi?

C5 Ethamu?

C5 Pihahirothi

D6 Mara

D6 Elimu

E6 NYIKA YA SINI

E7 Dofka

F8 Refidimu

F8 Ml. Sinai (Horebu)

F8 NYIKA YA SINAI

F7 Kibroth-hataava

G7 Haserothi

G6 Rimon-peresi

G5 Risa

G3 Kadeshi

G3 Bene-yaakani

G5 Hor-hagidgadi

H5 Yotbata

H5 Abrona

H6 Esion-geberi

G3 Kadeshi

G3 NYIKA YA ZINI

H3 Ml. Hori

H3 Salmona

I3 Punoni

I3 Iye-abarimu

I2 MOABU

I1 Diboni

I1 Almon-diblathaimu

H1 Yeriko

[Mahali pengine]

A3 GOSHENI

A4 Oni

A5 Memfisi (Nofu)

B3 Soani

B3 Tahpanhesi

C5 Migdoli

D3 SHURI

D5 NYIKA YA ETHAMU

F5 NYIKA YA PARANI

G1 UFILISTI

G1 Ashdodi

G2 Gaza

G2 Beer-sheba

G3 Asimoni

G3 NEGEBU

H1 Yerusalemu

H1 Hebroni (Kiriath-arba)

H2 Aradi (Mkanaani)

H4 SEIRI

H4 EDOMU

I7 MIDIANI

Barabara Kuu

Njia ya kuelekea Nchi ya Wafilisti

Njia ya kuelekea Shuri

I4 Barabara ya Mfalme

Njia ya Wafanyabiashara

Njia ya El Haji

[Milima]

F8 Ml. Sinai (Horebu)

H3 Ml. Hori

I1 Ml. Nebo

[Bahari]

E2 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)

D7/G7 Bahari Nyekundu

I1 Bahari ya Chumvi

[Mito na Kijito]

A6 Mto Nile

F3 B.M. la Misri

I2 Arnoni

I3 Seredi

[Picha katika ukurasa wa 8]

Misafara ya wafanyabiashara walivuka Rasi ya Sinai

[Picha katika ukurasa wa 8]

Waisraeli walipiga kambi mbele ya Mlima Sinai

[Picha katika ukurasa wa 9]

Maji yalipatikana kwenye chemchemi zilizokuwa Kadeshi au karibu na eneo hilo

[Picha katika ukurasa wa 9]

Iliwabidi Waisraeli wote wavuke bonde la mto la Arnoni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki