Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 20-21
  • Yerusalemu Na Hekalu La Sulemani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yerusalemu Na Hekalu La Sulemani
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • Hekalu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 20-21

Yerusalemu Na Hekalu La Sulemani

Jiji la Daudi

LILIITWA “ukamilifu wa uzuri” na “mji wa Mfalme Mkuu.” (Zb 48:2; 50:2; Omb 2:15) Yerusalemu lilikuwa jiji kuu la taifa la Mungu. (Zb 76:2) Baada ya Daudi kuteka jiji hilo kutoka kwa Wayebusi na kulifanya kuwa jiji lake kuu, liliitwa “Jiji la Daudi,” au “Sayuni.”—2Sa 5:7.

Ingawa Yerusalemu halikuwa mahali muhimu kivita, lilikuwa mashuhuri kwa sababu Mungu aliweka jina lake hapo. (Kum 26:2) Lilikuwa kituo cha kidini na cha kuendesha shughuli za serikali.

Yerusalemu liko katika mwinuko wa meta 750 juu ya usawa wa bahari katika safu ya milima iliyo katikati mwa Yudea. Biblia inataja kwamba jiji hilo lilikuwa ‘limeinuka’ na waabudu ‘walipanda’ kuelekea huko. (Zb 48:2, Union Version; 122:3, 4) Jiji hilo la kale lilizungukwa na mabonde: Bonde la Hinomu upande wa magharibi na kusini, na bonde la mto la Kidroni upande wa mashariki. (2Fa 23:10; Yer 31:40) Bubujiko la maji la Gihonia katika Bonde la Kidroni na En-rogeli lililokuwa upande wa kusini, lilikuwa chemchemi muhimu ya maji safi kwa jiji hilo hasa wakati maadui waliposhambulia.—2Sa 17:17.

Yerusalemu/Hekalu la Sulemani

Kwenye mchoro ulio katika ukurasa wa 21, Jiji la Daudi limeonyeshwa kwa rangi nyekundu. Wakati wa utawala wa Daudi na Sulemani, upande wa kaskazini wa jiji hilo ulifikia Ofeli (rangi ya kijani-kibichi) na Mlima Moria (rangi ya buluu). (2Sa 5:7-9; 24:16-25) Sulemani alimjengea Yehova hekalu lenye fahari kwenye mlima huo. Hebu wazia umati wa waabudu wakielekea “mlima wa Yehova” kwa ajili ya sherehe za kila mwaka! (Zek 8:3) Barabara zinazoonyeshwa kwenye ukurasa wa 17 zilifanya iwe rahisi kwa watu kusafiri.

Hekalu la Sulemani lililopambwa kwa dhahabu na mawe yenye thamani lilikuwa mojawapo ya majengo yaliyogharimu pesa nyingi zaidi. Jambo la kutokeza ni kwamba Yehova ndiye aliyetoa ramani ya ujenzi wa hekalu hilo. Kama unavyoona katika picha, kulikuwa na nyua kubwa na majengo ya usimamizi karibu na hekalu hilo. Utanufaika sana kujifunza kindani sehemu mbalimbali za hekalu hilo.—1Fa 6:1–7:51; 1Nya 28:11-19; Ebr 9:23, 24.

[Maelezo ya Chini]

a Mfalme Hezekia aliziba bubujiko hilo la maji na kujenga mtaro hadi kwenye kidimbwi kilichokuwa upande wa magharibi.—2Nya 32:4, 30.

[Sanduku katika ukurasa wa 21]

Baada ya muda, mipaka ya Yerusalemu ilipanuka upande wa magharibi na kaskazini. Wafalme wa Yuda waliotawala baada ya Sulemani walijenga kuta na malango zaidi. Utafiti wa kiakiolojia unaoendelea huenda ukaonyesha waziwazi ukubwa wa baadhi ya kuta hizo na mahali hususa zilipokuwa. Jiji hilo liliharibiwa mwaka wa 607 K.W.K. na likabaki ukiwa kwa miaka 70. Miaka 80 hivi baada ya Wayahudi kurudi, Nehemia alianza kazi kubwa sana ya kujenga upya kuta za Yerusalemu.

[Mchoro/Picha katika ukurasa wa 21]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Yerusalemu/Wakati wa Sulimani

ENEO LA HEKALU KATIKA SIKU ZA SULEMANI

Sehemu za Hekalu

1. Patakatifu Zaidi

2. Patakatifu

3. Ukumbi

4. Boazi

5. Yakini

6. Madhabahu ya Shaba

7. Bahari ya Kuyeyushwa

8. Mabehewa

9. Vyumba vya Kando

10. Vyumba vya Kulia Chakula

11. Ua wa Ndani

ENEO LA HEKALU

Ml. Moria

Vyumba vya

Mabehewa Kulia Chakula

Vyumba vya Kando

Patakatifu Boazi

Zaidi Patakatifu Ukumbi Madhabahu Ua wa

Yakini ya Shaba Ndani

Mabehewa Bahari ya

Kuyeyushwa

Ofeli

Kiwanja cha Watu Wote?

Lango la Maji?

JIJI LA DAUDI

Ml. Sayuni

Jumba la Mfalme Daudi

Lango la Chemchemi

Ukuta wa Manase?

Mnara wa Hananeli

Mnara wa Mea

Lango la Kondoo

Lango la Mlinzi

Lango la Ukaguzi

Lango la Farasi

KIDRONI VALLEY

Ukuta wa Chini?

Gihoni

Mfereji wa maji uliojengwa baadaye

TYROPOEON VALLEY

Lango la Marundo ya Majivu (Potsherds) (Dung)

En-rogeli

Lango la Bonde

VALLEY OF HINOMU

Lango la Pembeni

Mnara wa Jiko la Kuokea

Ukuta Mpana

Lango la Efraimu

Kiwanja cha Watu Wote

Lango la Jiji la Kale

Ukuta wa Kaskazini Uliotangulia Kujengwa

ENEO LA PILI

Lango la Samaki

[Picha]

Ofeli

Nyumba ya Binti ya Farao

Jumba la Mfalme Sulemani

Nyumba ya Msitu wa Lebanoni

Ukumbi wa Nguzo

Ukumbi wa Kiti cha Ufalme

Ml. Moria

Ua Mkuu

Hekalu

[Picha katika ukurasa wa 20]

Sehemu ya mbele ya picha hii inaonyesha mahali “Jiji la Daudi” lilipokuwa. Hekalu lilikuwa katika eneo tambarare (nyuma)

[Picha katika ukurasa wa 20]

Mchoro wa kompyuta unaoonyesha “Jiji la Daudi” la kale na hekalu la Sulemani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki