Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gl kur. 16-17
  • Israeli Katika Siku Za Daudi Na Sulemani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Israeli Katika Siku Za Daudi Na Sulemani
  • ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Yehova Alipowasimamisha Waamuzi’
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Nchi Ya Ahadi
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Israeli Na Mataifa Yaliyolizunguka
    ‘Ona Nchi Nzuri’
  • Yesu “Katika Nchi Ya Wayahudi”
    ‘Ona Nchi Nzuri’
Pata Habari Zaidi
‘Ona Nchi Nzuri’
gl kur. 16-17

Israeli Katika Siku Za Daudi Na Sulemani

MUNGU aliahidi kuupatia uzao wa Abramu nchi ‘iliyotoka mto wa Misri mpaka mto Efrati.’ (Mwa 15:18; Kut 23:31; Kum 1:7, 8; 11:24) Baada ya Yoshua kuingia Kanaani, ilichukua muda wa karne nne hivi kwa Nchi ya Ahadi kufikia mipaka hiyo.

Mfalme Daudi aliwashinda Waaramu waliotawala ufalme wa Soba ambao ulienea hadi Mto Efrati kaskazini mwa Siria.a Daudi alipowashinda Wafilisti, alipanua miliki yake upande wa kusini hadi kufikia mpaka wa Misri.—2Sa 8:3; 1Nya 18:1-3; 20:4-8; 2Nya 9:26.

Mipaka (Wakati wa Sulemani)
Daudi na Sulemani (barabara)

Naye Sulemani alitawala “kutoka ule Mto [Efrati] hadi kwenye nchi ya Wafilisti na hadi kwenye mpaka wa Misri.” Utawala wake ulifananisha utawala wenye amani wa Mesiya. (1Fa 4:21-25; 8:65; 1Nya 13:5; Zb 72:8; Zek 9:10) Hata hivyo, inasemekana kwamba eneo lililokaliwa na Waisraeli ‘lilianzia Dani mpaka Beer-sheba.’—2Sa 3:10; 2Nya 30:5.

Mfalme Sulemani alikosa kumtii Mungu alipojirundikia farasi na magari ya vita. (Kum 17:16; 2Nya 9:25) Angeweza kuendesha farasi na magari hayo kwenye mfumo wa barabara uliokuwako. (Yos 2:22; 1Fa 11:29; Isa 7:3; Mt 8:28) Ni barabara chache sana tunazoelezewa mahali zilipopitia. Kwa mfano, tunaelezwa kuhusu “njia kuu inayopanda kutoka Betheli kwenda Shekemu na kuelekea upande wa kusini wa Lebona.”—Amu 5:6; 21:19.

Kitabu The Roads and Highways of Ancient Israel kinasema: ‘Ni vigumu kuchunguza mfumo wa barabara uliokuwako katika Israeli la kale, kwa kuwa barabara zilizokuwako wakati wa Agano la Kale hazikuwekwa lami hivyo hazingedumu.’ Hata hivyo, sura ya nchi na magofu ya majiji yaliyofukuliwa yanaonyesha mahali barabara nyingi zilipopitia.

Mara nyingi barabara ziliwasaidia wanajeshi kuamua mahali ambapo wangeelekea. (1Sa 13:17, 18; 2Fa 3:5-8) Ili kushambulia Israeli, Wafilisti walipiga mwendo kutoka Ekroni na Gathi hadi kwenye eneo lililokuwa “kati ya Soko na Azeka.” Jeshi la Sauli lilikutana nao huko “katika nchi tambarare ya chini ya Ela.” Baada ya Daudi kumuua Goliathi, Wafilisti walikimbia na kurudi Gathi na Ekroni, naye Daudi akakwea Yerusalemu.—1Sa 17:1-54.

Lakishi (D10), Azeka (D9), na Beth-shemeshi (D9) zilikuwa kwenye njia iliyopitia Shefela kuelekea vilima vya Yudea. Kwa hiyo majiji hayo yalikuwa muhimu sana katika kuzuia maadui wasipitie njia ya Via Maris na kufika katikati mwa nchi ya Israeli.—1Sa 6:9, 12; 2Fa 18:13-17.

[Maelezo ya Chini]

a Eneo la wana wa Rubeni lilifika kwenye Jangwa la Siria, na mpaka wake wa mashariki ulifika Mto Efrati.—1Nya 5:9, 10.

[Sanduku katika ukurasa wa 16]

VITABU VYA BIBLIA TANGU WAKATI HUO:

Samweli wa 1 na 2

Zaburi (sehemu)

Methali (sehemu)

Wimbo wa Sulemani

Mhubiri

[Ramani katika ukurasa wa 17]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

Maeneo Na Barabara Wakati Wa Ufalme Ulioungana

Mipaka (Wakati wa Sulimani)

Tifsa

Hamathi

Tadmori

Berothai (Kuni?)

Sidoni

Damasko

Tiro

Dani

Yerusalemu

Gaza

Aroeri

Beer-sheba

Tamari

Esion-geberi

Elathi (Elothi)

[Mito na Vijito]

Efrati

B.M. la Misri

Daudi na Sulemani (barabara)

B10 Gaza

C8 Yopa

C9 Ashdodi

C10 Ashkeloni

C11 Siklagi

C12 NYIKA YA PARANI

D5 Dori

D6 Heferi

D8 Afeki

D8 Rama

D9 Shaalbimu

D9 Gezeri

D9 Makazi

D9 Ekroni

D9 Beth-shemeshi

D9 Gathi

D9 Azeka

D10 Soko

D10 Adulamu

D10 Keila

D10 Lakishi

D11 Yatiri

D12 Beer-sheba

E2 Tiro

E4 Kabuli

E5 Yokneamu (Yokmeamu?)

E5 Megido

E6 Taanaki

E6 Arubothi

E7 Pirathoni

E8 Lebona

E8 Sereda

E8 Betheli

E9 Beth-horoni ya Chini

E9 Beth-horoni ya Juu

E9 Geba

E9 Gibeoni

E9 Gibea

E9 Kiriath-yearimu

E9 Nobu

E9 Baal-perasimu

E9 Yerusalemu

E9 Bethlehemu

E10 Tekoa

E10 Hebroni

E11 Zifu

E11 Horeshi?

E11 Karmeli

E11 Maoni

E11 Eshtemoa

F5 En-dori

F5 Shunemu

F5 Yezreeli

F6 Beth-sheani

F7 Tirsa

F7 Shekemu

F8 Sarethani

F8 Shilo

F8 Ofra?

F9 Yeriko

F11 En-gedi

G2 Abel-beth-maaka

G2 Dani

G3 Hasori

G3 MAAKA

G5 Lo-debari (Debiri)

G5 Rogelimu

G6 Abel-mehola

G7 Sukothi

G7 Mahanaimu

H1 SIRIA

H4 GESHURI

H6 Ramoth-gileadi

H8 Raba

H9 Medeba

H11 Aroeri

H12 MOABU

I4 Helamu?

I9 AMONI

[Babara kuu]

C10 Via Maris

H6 Barabara ya Mfalme

[Milima]

F5 Ml. Gilboa

[Bahari]

C8 Bahari ya Mediterania (Bahari Kuu)

F10 Bahari ya Chumvi

G4 Bahari ya Galilaya

[Chemchemi au kisima]

E9 En-rogeli

[Picha katika ukurasa wa 16]

Kulia: Bonde la Ela, vilima vya Yuda vikiwa upande wa mashariki

Chini: Barabara zilirahisisha usafiri katika Nchi ya Ahadi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki