Wimbo Na. 26
Tembea Pamoja na Mungu!
Makala Iliyochapishwa
(Mika 6:8)
1. Tembea pamoja naye;
Yehova kwa kiasi.
Nawe ushike ukamilifu;
Ili akupe nguvu.
Na ukitii kweli yake,
Usidanganyike;
Mungu na akuongoze,
Sawa na mutoto.
2. Tembea pamoja naye;
Na dhambi uepuke.
Nawe ufanye maendeleo,
Pata kibali chake.
Yote yaliyo safi, mema,
Tafakari hayo.
Na ili uvumilie,
Tumaini Mungu.
3. Tembea pamoja naye;
Nawe utajifunza,
Ujitoaji, na kuridhika,
Sifa zenye faida.
Utembee naye kwa shangwe.
Imba sifa zake.
Kufanya kazi ya Mungu,
Hutupa furaha.
(Ona pia Mwa. 5:24; 6:9; Flp. 4:8; 1 Tim. 6:6-8.)