WIMBO NA. 86
Lazima Tufundishwe
Makala Iliyochapishwa
1. Njo’ni mjifunze kuhusu Yehova.
‘Njo’ni mnywe maji ya uzima.’
Mafunzo mema yake Yehova.
Wenye njaa wote watalishwa.
2. Na mikutano kamwe tusisahau,
Lazima tufundishwe na Mungu.
Hapa palipo roho ya Mungu,
Tunatembea katika nuru.
3. Nyimbo tuimbazo zatutia moyo!
Sauti tamu za ndugu zetu!
Tukutanike na watu Wake.
Sikuzote tusikosekane.
(Ona pia Ebr. 10:24, 25; Ufu. 22:17.)