Wimbo Na. 39
Amani Tuliyo Nayo
Makala Iliyochapishwa
1. Tumusifu Yehova,
Mwenye amani,
Atakomesha vita,
Kuwe amani.
Mukuu wa amani,
Ni Kristo Yesu.
Kutakuwa amani,
Atawalapo.
2. Tumeacha kinyongo,
Pia uchungu.
Mapanga na mikuki,
Tumebadili.
Ili kuwe amani,
Tutasamehe,
Na kuishi pamoja,
Kama “kondoo.”
3. Na tuwe na amani,
Sifa ya roho.
Twaonyesha hekima,
Kutoka juu.
Wengine wataona,
Tuna amani.
Hadi Ufalme uje,
Amani tele.
(Ona pia Zab. 46:9; Isa. 2:4; Yak. 3:17, 18.)