WIMBO NA. 113
Amani Tuliyo Nayo
Makala Iliyochapishwa
1. Tumsifu Yehova,
Mwenye amani,
Atakomesha vita,
Kuwe amani.
Mkuu wa amani,
Ni Kristo Yesu.
Kutakuwa amani,
Atawalapo.
2. Tumeacha ghadhabu,
Na chuki pia.
Mapanga na mikuki,
Tumebadili.
Ili kuwe amani,
Tutasamehe,
Na kuishi pamoja,
Kama “kondoo.”
3. Amani ya Yehova,
Baraka kwetu.
Tutii maagizo,
Toka moyoni.
Wengine na waone,
Tuna amani.
Hadi Ufalme uje,
Kuwe amani.
(Ona pia Zab. 46:9; Isa. 2:4; Yak. 3:17, 18.)