Wimbo Na. 51
Tunashikamana na Yehova
Makala Iliyochapishwa
1. Bwana mwenye enzi kuu Yehova Mungu,
Utawala wake wa haki sikuzote.
Maneno yake yote yatatimia.
Tunashikamana na Yehova Mungu;
Na kuukubali utawala wake.
2. Kiti chake cha enzi kimeimarishwa.
Pande zote amezingirwa utukufu.
Wapole awaalika waje kwake.
Tunashikamana na Yehova Mungu;
Ndiye astahiliye kuabudiwa.
3. Mbingu za mbingu hazimutoshi Yehova.
Hakuna awezaye kushindana Naye.
Yote atabiriyo, yatatimia.
Tunashikamana na Yehova Mungu;
Mapenzi yake na tuzidi kufanya.
(Ona pia Kum. 4:4; 30:20; 2 Fal. 18:6; Zab. 89:14.)