Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 6 uku. 9
  • Ayubu Adumisha Utimilifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ayubu Adumisha Utimilifu
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Ayubu Alilitukuza Jina la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Ukamilifu wa Ayubu—Ni Nani Anayeweza Kuuiga?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Ukamilifu wa Ayubu—Kwa Sababu Gani Unastaajabisha Sana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • “Sitaukana Utimilifu Wangu!”
    Igeni Imani Yao
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 6 uku. 9
Ayubu akiwa na majipu mwili mzima

SEHEMU YA 6

Ayubu Adumisha Utimilifu

Shetani atilia shaka utimilifu wa Ayubu mbele za Mungu, lakini Ayubu abaki mwaminifu kwa Yehova

JE, MWANADAMU yeyote angeweza kuendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu ikiwa angejaribiwa vya kutosha na iwapo ingeonekana kana kwamba kuendelea kwake kumtii Mungu hakuna faida yoyote? Swali hilo lilitokezwa—na kujibiwa—katika kisa cha mtu anayeitwa Ayubu.

Waisraeli walipokuwa wangali Misri, Ayubu, mtu wa jamaa ya Abrahamu, alikuwa akiishi katika eneo ambalo leo ni Uarabuni. Wakati huohuo, malaika mbinguni walikusanyika mbele za Mungu, na yule mwasi, Shetani, alikuwa katikati yao. Katika mkutano huo huko mbinguni, Yehova alimsifu mtumishi wake mwaminifu Ayubu. Alisema kwamba hakuna mwanadamu mwingine yeyote aliye na utimilifu kama wa Ayubu. Lakini Shetani alisisitiza kwamba Ayubu anamtumikia Mungu kwa sababu Mungu anambariki na kumlinda. Shetani alidai kwamba ikiwa Ayubu angenyang’anywa kila kitu alichokuwa nacho, angemlaani Mungu.

Malaika wakiwa mbinguni wamekusanyika mbele za Mungu na Shetani akiwa miongoni mwao

Kwanza, Mungu alimruhusu Shetani amnyang’anye Ayubu mali yake na watoto wake, kisha aingilie afya yake. Kwa kuwa Ayubu hakujua Shetani anahusika, hakuelewa ni kwa nini Mungu anaruhusu apatwe na mambo yote hayo. Hata hivyo, Ayubu hakumkana Mungu kamwe.

Marafiki watatu bandia walimjia Ayubu. Walisema mengi wakijaribu kumsadikisha eti Mungu anamhukumu kwa sababu ya dhambi alizofanya kisiri. Hata walidai kwamba Mungu hapendezwi na watumishi wake wala hana imani nao. Ayubu alikataa maoni yao yenye kosa. Akiwa na uhakika, Ayubu alitangaza kwamba atadumisha utimilifu wake mpaka kifo!

Hata hivyo, Ayubu alikosea kwa kutaka sana kuonyesha kwamba hana kosa lolote. Kijana anayeitwa Elihu, ambaye alikuwa akisikiliza mjadala wote huo, akaanza kuzungumza. Elihu alimkaripia Ayubu kwa kutotambua kwamba kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova Mungu ni muhimu kuliko kutetewa kwa mwanadamu yeyote. Pia aliwakaripia vikali rafiki watatu bandia wa Ayubu.

Kisha Yehova Mungu akazungumza na Ayubu, akirekebisha maoni yake. Akitaja uumbaji mbalimbali wa ajabu, Yehova alimsaidia Ayubu kuona jinsi mwanadamu alivyo duni kwa kulinganishwa na ukuu wa Mungu. Ayubu alikubali nidhamu hiyo kutoka kwa Mungu. Kwa kuwa Yehova ni “mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema,” alimponya Ayubu, akampa maradufu mali aliyokuwa nayo, na kumbariki kwa wana wengine kumi. (Yakobo 5:11) Kwa kudumisha utimilifu wake kwa Yehova chini ya jaribu kali, Ayubu alitoa jibu tosha kwa dai la Shetani kwamba wanadamu hawawezi kuwa waaminifu kwa Mungu wakijaribiwa.

—Inatoka kwenye Kitabu cha Ayubu.

  • Shetani alidai nini kuhusu Ayubu?

  • Utimilifu wa Ayubu kwa Yehova ulitimiza nini?

MASUALA MUHIMU

Shetani alidai kwamba Ayubu, mtu asiye na lawama na mwenye kumwogopa Mungu kuliko watu wote waliokuwa duniani wakati huo, anamtumikia Yehova Mungu kwa sababu za kibinafsi. Dai hilo la Shetani lilidokeza pia kwamba viumbe wengine wote wenye akili wanamtumikia Yehova kwa sababu za kibinafsi. Suala hilo ni sehemu ya suala kuu zaidi ambalo Shetani alizusha katika shamba la Edeni, yaani, haki na kustahili kwa enzi kuu ya Yehova. Kitabu cha Ayubu kinaonyesha kwamba viumbe wa Mungu wanaweza kuchangia kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova kwa kudumisha utimilifu wao Kwake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki