Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 25 uku. 29
  • Mashauri Kuhusu Imani, Mwenendo, na Upendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashauri Kuhusu Imani, Mwenendo, na Upendo
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • “Mwishindanie Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • “Wapendwa, . . . Jidumisheni Katika Upendo wa Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Waliandika Habari Zinazomhusu Yesu
    Wafundishe Watoto Wako
  • Mambo Makuu Katika Barua za Yohana na ya Yuda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 25 uku. 29
Mwandishi wa Biblia akiandika barua

Sehemu ya 25

Mashauri Kuhusu Imani, Mwenendo, na Upendo

Yakobo, Petro, Yohana, na Yuda, waandika barua za kuwatia moyo waamini wenzao

YAKOBO na Yuda walikuwa ndugu wa kambo wa Yesu. Petro na Yohana walikuwa mitume wa Yesu. Wanaume hao wanne waliandika jumla ya barua saba katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Kila moja ya barua hizo ina jina la mwandikaji. Mashauri yaliyoongozwa na roho yaliyo katika barua hizo yalikusudiwa kuwasaidia Wakristo kudumisha utimilifu kwa Yehova na kuendelea kuutazamia Ufalme wake.

Wakristo wanapaswa kuwa na imani. Haitoshi tu kudai kwamba mtu ana imani. Imani ya kweli huambatana na matendo. Yakobo aliandika: “Imani bila matendo imekufa.” (Yakobo 2:26) Mtu anapotenda kwa imani akiwa katika majaribu, anasitawisha sifa ya uvumilivu. Ili kufanikiwa, Mkristo anahitaji kumwomba Mungu ampe hekima, akiwa na imani kwamba Mungu atampa. Uvumilivu humfanya mtu akubaliwe na Mungu. (Yakobo 1:2-6, 12) Mwabudu wa Mungu akidumisha utimilifu kwa imani, Yehova Mungu atajibu sala yake. Yakobo asema: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8.

Mkristo anapaswa kuwa na imani yenye nguvu inayoweza kumsaidia kushinda vishawishi na kuepuka upotovu wa maadili. Kwa sababu ya upotovu wa maadili uliokuwa umeenea, Yuda aliwahimiza waamini wenzake ‘wafanye pigano kali kwa ajili ya imani.’—Yuda 3.

Dumisha mwenendo safi. Yehova hutaka waabudu wake wawe watakatifu au safi katika kila njia. Petro aandika: “Ninyi wenyewe pia iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote, kwa sababu imeandikwa: ‘Muwe watakatifu, kwa sababu mimi [Yehova] ni mtakatifu.’” (1 Petro 1:15, 16) Wakristo wamewekewa mfano wa kuiga. Petro asema: “Kristo aliteseka kwa ajili yenu, akiwaachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake kwa ukaribu.” (1 Petro 2:21) Ijapokuwa huenda Wakristo wakateseka kwa sababu wanaishi kulingana na viwango vya Mungu, wanadumisha “dhamiri njema.” (1 Petro 3:16, 17) Petro anawahimiza Wakristo wawe na mwenendo na matendo matakatifu ya ujitoaji-kimungu huku wakiingojea siku ya hukumu ya Mungu na dunia mpya iliyoahidiwa ambamo “uadilifu utakaa.”—2 Petro 3:11-13.

“Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.”—Yakobo 4:8

Wakristo wanapaswa kuwa na upendo. Yohana aliandika: “Mungu ni upendo.” Mtume huyo anasema kwamba Mungu alionyesha upendo wake mkuu kwa kumtuma Yesu awe ‘dhabihu kwa ajili ya dhambi zetu.’ Kwa hiyo basi, Wakristo wanapaswa kufanya nini? Yohana anajibu: “Wapendwa, ikiwa Mungu alitupenda hivi, basi sisi wenyewe tuko chini ya wajibu wa kupendana.” (1 Yohana 4:8-11) Njia moja ya kuonyesha upendo kama huo ni kwa kuwaonyesha ukarimu waamini wenzetu.—3 Yohana 5-8.

Hata hivyo, waabudu wa Yehova wanaweza kuonyesha jinsi gani kwamba wanampenda? Yohana anajibu: “Kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si mzigo mzito.” (1 Yohana 5:3; 2 Yohana 6) Wale wanaomtii Mungu kwa njia hiyo wanahakikishiwa kwamba Mungu ataendelea kuwapenda huku ‘wakitazamia uzima wa milele.’—Yuda 21.

—Inatoka kwenye Yakobo; 1 Petro; 2 Petro; 1 Yohana; 2 Yohana; 3 Yohana; Yuda.

  • Wakristo wanaweza kuonyesha imani kwa njia gani?

  • Mungu anataka waabudu wake wawe na mwenendo wa aina gani?

  • Mtu anaweza kuonyesha jinsi gani kwamba anampenda Mungu kikweli?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki