Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rk seh. ya 4 kur. 10-11
  • Mungu Ni Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Ni Nani?
  • Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Habari Zinazolingana
  • Namna Malaika Wanavyoweza Kukusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Malaika—Je! Wao Wanaathiri Maisha Yako Wewe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
rk seh. ya 4 kur. 10-11

Sehemu ya 4

Mungu Ni Nani?

WATU huabudu miungu mingi. Lakini Maandiko Matakatifu hufundisha kwamba kuna Mungu mmoja tu wa kweli. Hana kifani, ni mkuu sana, na ni wa milele. Aliumba kila kitu mbinguni na duniani, na akatupa uhai. Kwa hiyo, yeye peke yake ndiye anayestahili kuabudiwa.

Musa ameshika mabamba ya mawe yenye Amri Kumi

Sheria ilitolewa kupitia nabii Musa ikiwa “neno lililosemwa kupitia malaika”

Mungu ana jina moja tu la kibinafsi. Jina hilo ni YEHOVA. Mungu alimwambia Musa: “Hivi ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu.’ Hilo ndilo jina langu mpaka wakati usio na kipimo, na huo ndio ukumbusho wangu kwa kizazi baada ya kizazi.” (Kutoka 3:15) Jina Yehova linapatikana katika Maandiko Matakatifu mara 7,000 hivi. Kama andiko la Zaburi 83:18 linavyosema kumhusu Mungu, “wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Kitabu cha Kukunjwa cha Bahari ya Chumvi kikiwa na jina la Mungu likiwa limetiwa kivuli

Kitabu cha Kukunjwa cha kale cha Bahari ya Chumvi kilicho na maandishi yanayoonyesha jina la Mungu

Hakuna mtu ambaye amewahi kumwona Mungu. Mungu alimwambia Musa: “Huwezi kuuona uso wangu, kwa sababu hakuna mwanadamu anayeweza kuniona na bado aishi.” (Kutoka 33:20) Mungu anaishi mbinguni na hakuna mtu anayeweza kumwona. Ni kosa kutengeneza au kutumia sanamu, picha, au mfano wa Mungu katika sala. Yehova Mungu aliamuru hivi kupitia nabii Musa: “Usijifanyie sanamu ya kuchongwa wala umbo lililo kama kitu chochote kilicho juu mbinguni wala kilicho chini duniani wala kilicho ndani ya maji chini ya dunia. Usiviinamie wala kushawishiwa kuvitumikia, kwa sababu mimi Yehova Mungu wako ni Mungu anayetaka watu wajitoe kikamili.” (Kutoka 20:2-5) Baadaye, kupitia nabii Isaya, Mungu alisema: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu; nami sitampa mwingine yeyote utukufu wangu mwenyewe, wala sitazipa sanamu za kuchongwa sifa yangu.”—Isaya 42:8.

Watu fulani humwamini Mungu lakini huenda wakamwona kuwa asiyeweza kujulikana wala kufikiwa, wanayepaswa kumwogopa badala ya kumpenda. Una maoni gani? Je, Mungu anapendezwa na wewe? Unaweza kwa kweli kumjua, au hata kumkaribia? Acha tuone kile ambacho Maandiko yanasema kuhusu sifa za Mungu.

Ungejibu Namna Gani?

  • Kwa nini tumwabudu Mungu?

  • Jina la Mungu ni nani?

  • Kwa nini hatupaswi kutumia sanamu au mifano kumwabudu Mungu?

  • Mungu hutumia jinsi gani roho yake takatifu na malaika kutimiza mapenzi yake?

Roho Takatifu ya Mungu na Malaika Zake

Mungu hutimizaje mapenzi yake? Njia moja ni kupitia roho yake takatifu. Roho ya Mungu si kiumbe chenye uhai au malaika, bali ni nguvu zake za utendaji zisizoonekana, zisizo na mipaka ambazo anatumia kutimiza chochote atakacho. Mungu alitumia roho hiyo kuumba mbingu na dunia. “Mbingu zilifanywa kwa neno la Yehova, nayo majeshi yake yote yalifanywa kwa roho ya kinywa chake.” (Zaburi 33:6) Andiko la Mwanzo 1:2 linaeleza kwamba dunia ilipokuwa ingali imefunikwa na maji na Mungu alikuwa akiitayarisha ili wanadamu waishi ndani yake, “nguvu za utendaji za Mungu zilikuwa zikienda huku na huku juu ya uso wa maji.” Kisha Mungu akatumia roho yake takatifu kuumba vitu vyote vilivyo hai duniani.

Pia, Mungu hutumia malaika kutimiza mapenzi yake. Mungu aliwaumba waishi naye mbinguni. Malaika wana nguvu nyingi sana. Wao huwasilisha ujumbe wa Mungu na kufanya kazi nyingine muhimu. Kwa mfano, Maandiko yanataja Sheria iliyotolewa kupitia nabii Musa kuwa “neno lililosemwa kupitia malaika.” Malaika wa Mungu huwasaidia pia watumishi wake walio duniani. Maandiko yanawaita malaika wa Mungu “roho kwa ajili ya utumishi wa watu wote, waliotumwa kuhudumu kwa ajili ya wale watakaorithi wokovu.”—Waebrania 1:14; 2:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki