Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rk seh. ya 11 kur. 26-27
  • Kuonyesha Imani ya Kweli Leo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuonyesha Imani ya Kweli Leo
  • Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tumia Nguvu kwa Njia Inayofaa
  • Dumisha Viwango vya Mungu vya Haki
  • Jifunze Hekima Kutoka kwa Mungu
  • Onyesha Upendo wa Kweli
  • Imani ya Kweli Ni Nini?
    Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Je, Kweli Una Imani Katika Habari Njema?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • “Imani Iliyotenganishwa na Matendo Imekufa Kama Mzoga”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Imani ya Kweli—Siri ya Kuwa na Maisha Yenye Furaha
rk seh. ya 11 kur. 26-27

Sehemu ya 11

Kuonyesha Imani ya Kweli Leo

WATU wengi leo hudai kwamba wana imani. Hata hivyo, Yesu alifundisha kwamba ni watu wachache tu ambao wangekuwa na imani ya kweli. Alisema: “Ingieni kupitia lango jembamba; kwa sababu barabara inayoongoza kwenye uharibifu ni pana na kubwa, na wengi ndio wanaoipitia; lakini lango ni jembamba na barabara inayoongoza kwenye uzima ina nafasi ndogo, na wachache ndio wanaoipata.”—Mathayo 7:13, 14.

Leo watu huonyesha kwamba wana imani ya kweli jinsi gani? “Kwa matunda yao mtawatambua,” Yesu akasema. “Kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini kila mti uliooza huzaa matunda yasiyofaa.” (Mathayo 7:16, 17) Hivyo basi, imani ya kweli huzaa “matunda mazuri.” Huwachochea watu kuwa na sifa zinazokubaliwa na Mungu. Jinsi gani?

Tumia Nguvu kwa Njia Inayofaa

Watu walio na imani ya kweli hutumia nguvu na mamlaka yao kumtukuza Mungu na kuwanufaisha wengine. Yesu alifundisha: “Yeyote yule anayetaka kuwa mkubwa katikati yenu lazima awe mhudumu wenu.” (Marko 10:43) Vivyo hivyo, wanaume wenye imani ya kweli si wakatili, wawe nyumbani au kwingineko. Wanawapenda wake zao, wanawaheshimu, na kushughulikia mahitaji yao kwa upendo. Maandiko yanasema: “Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.” (Wakolosai 3:19) “Waume, endeleeni kukaa nao vivyo hivyo kulingana na ujuzi, mkiwapa heshima kama chombo dhaifu zaidi, yaani, mwanamke, kwa kuwa ninyi pia ni warithi pamoja nao wa pendeleo lisilostahiliwa la uzima, kusudi sala zenu zisizuiwe.”—1 Petro 3:7.

Kwa upande mwingine, mke ambaye ana imani ya kweli “anapaswa kumheshimu sana mume wake.” (Waefeso 5:33) Wake wanapaswa ‘kuwapenda waume zao na kuwapenda watoto wao.’ (Tito 2:4) Akina baba na mama walio na imani ya kweli hutenga wakati kuwa pamoja na watoto wao na kuwafundisha sheria na kanuni za Mungu. Wanapokuwa nyumbani, kazini, na penginepo, wao huwatendea wengine kwa staha na heshima. Wanafuata shauri hili la Kimaandiko: “Katika kuonyeshana heshima iweni wa kwanza.”—Waroma 12:10.

Watumishi wa Mungu hutii amri hii ya Kimaandiko: “Usikubali rushwa.” (Kutoka 23:8) Hawatumii kamwe mamlaka yao ili kujinufaisha. Badala yake, wao hutafuta fursa za kuwasaidia wengine, hasa walio na uhitaji. Wanatii shauri hili: “Msisahau kutenda mema na kushiriki vitu pamoja na wengine, kwa maana Mungu hupendezwa vema na dhabihu za namna hiyo.” (Waebrania 13:16) Kwa hiyo, wanajionea ukweli wa maneno haya ya Yesu: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.

Dumisha Viwango vya Mungu vya Haki

Watu wenye imani hutii sheria za Mungu kwa hiari, na kwao “amri zake si mzigo mzito.” (1 Yohana 5:3) Wanajua kwamba “sheria ya Yehova ni kamilifu . . . Maagizo kutoka kwa Yehova ni manyoofu, huufanya moyo ushangilie; amri ya Yehova ni safi, huyafanya macho yang’ae.”—Zaburi 19:7, 8.

Imani ya kweli huwachochea pia kukataa kila aina ya ubaguzi. Hawapendelei watu wa jamii fulani, nchi fulani, au cheo fulani, badala yake, wanafuata mfano wa Mungu. “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”—Matendo 10:34, 35.

Imani ya kweli huwachochea watu “kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.” (Waebrania 13:18) Pia, mtu mwenye imani huepuka porojo na uchongezi wenye kuumiza. Kuhusu mtu anayekubaliwa na Mungu, mtunga-zaburi Daudi aliandika: “Hakuchongea kwa ulimi wake. Hakumfanyia mwenzake jambo lolote baya.”—Zaburi 15:3.

Jifunze Hekima Kutoka kwa Mungu

Wale walio na imani ya kweli hutegemeza mafundisho yao katika Maandiko Matakatifu. Wanaamini kwamba “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu.” (2 Timotheo 3:16) Katika mahusiano yao pamoja na wengine, wao huonyesha “hekima inayotoka juu,” ambayo ni “safi kiadili, kisha yenye kufanya amani, yenye usawaziko, tayari kutii, yenye kujaa rehema na matunda mema.” (Yakobo 3:17) Wanajiepusha na mapokeo yasiyofaa na kuwasiliana na pepo, nao ‘hujilinda na sanamu.’—1 Yohana 5:21.

Onyesha Upendo wa Kweli

Nabii Musa alisema: “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Kumbukumbu la Torati 6:5) Watu wenye imani huwa na upendo wa aina hiyo kumwelekea Mungu. Wanaliheshimu jina la Mungu, Yehova. Wao ‘humshukuru Yehova, na kuliitia jina lake’ kwa imani. (Zaburi 105:1) Watumishi wa Mungu hutii amri hii pia: “Nawe mpende mwenzako kama wewe mwenyewe.” (Mambo ya Walawi 19:18) Wao hukataa jeuri na hujaribu kuwa “wenye kufanya amani na watu wote.” (Waroma 12:18) Kwa njia ya mfano, ‘wamefua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.’ (Isaya 2:4) Kwa sababu hiyo, wana “upendo kati [yao] wenyewe” na wanafurahia undugu wa ulimwenguni pote. (Yohana 13:35) Je, unaweza kuwatambua watu wa aina hiyo leo?

Ungejibu Namna Gani?

  • Ni nini kinachowatambulisha watu wenye imani ya kweli?

  • Watu wenye imani huonyesha jinsi gani sifa za Mungu kuhusiana na nguvu? hekima? haki? upendo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki