SEHEMU YA 14
Unawezaje Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova?
Amua kuwa upande wa Mungu. 1 Petro 5:6-9
Epuka desturi zozote zinazopingana na Biblia. Unahitaji ujasiri ili kufanya hivyo.
Usijiingize katika siasa za mataifa; mataifa hayo hayaungi mkono Yehova na Ufalme wake.
Fanya uamuzi mzuri—msikilize Mungu. Mathayo 7:24, 25
Shirikiana na Mashahidi wa Yehova; nao watakusaidia kumkaribia Mungu.
Endelea kujifunza kumhusu Mungu na ujitahidi kutii amri zake.
Imani yako itakapokuwa yenye nguvu zaidi, ujiweke wakfu kwa Yehova na ubatizwe.—Mathayo 28:19.
Msikilize Mungu. Soma Biblia, na uwaombe Mashahidi wa Yehova wakusaidie kuielewa. Kisha, ufanye mambo unayojifunza. Ukifanya hivyo, utaishi milele.—Zaburi 37:29.