Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 12
  • Kazi Yetu ya Kuhubiri Ufalme Hufanywaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Yetu ya Kuhubiri Ufalme Hufanywaje?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanahubiri Nyumba kwa Nyumba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Lo Lote Ufanyalo—Hubiri!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 12

SOMO LA 12

Kazi Yetu ya Kuhubiri Ufalme Hufanywaje?

Mashahidi wa Yehova wakihubiri nyumba kwa nyumba

Hispania

Shahidi wa Yehova akihubiri katika bustani

Belarus

Shahidi wa Yehova akihubiri kupitia simu

Hong Kong

Mashahidi wa Yehova wakihubiri hadharani

Peru

Muda mfupi kabla ya kifo chake, Yesu alisema: “Habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:14) Lakini kazi hiyo ya kuhubiri ulimwenguni pote ingetimizwa jinsi gani? Ingetimizwa kwa kufuata kielelezo ambacho Yesu aliweka alipokuwa duniani.—Luka 8:1.

Tunajitahidi kuhubiri nyumba kwa nyumba. Yesu aliwazoeza wanafunzi wake kuhubiri habari njema nyumba kwa nyumba. (Mathayo 10:11-13; Matendo 5:42; 20:20) Wanafunzi hao walipewa maeneo hususa ya kuhubiri. (Mathayo 10:5, 6; 2 Wakorintho 10:13) Vivyo hivyo leo, kazi yetu ya kuhubiri inafanywa kwa utaratibu, na kila kutaniko huwa na eneo lake la kuhubiri. Utaratibu huo hutuwezesha kutimiza amri ya Yesu ya ‘kuwahubiria watu na kutoa ushahidi kamili.’—Matendo 10:42.

Tunajitahidi kuwafikia watu mahali popote walipo. Yesu alituwekea mfano kwa kuwahubiria watu katika maeneo mbalimbali yenye watu wengi kama vile kwenye ufuo wa bahari au kisimani. (Marko 4:1; Yohana 4:5-15) Sisi pia huzungumza na watu kuhusu Biblia popote walipo—iwe ni barabarani, katika maeneo ya biashara, kwenye mabustani, au kupitia simu. Pia, tunawahubiria majirani, wafanyakazi, wanafunzi, na watu wetu wa ukoo tunapopata fursa. Jitihada zote hizo zimefanya iwezekane kwa mamilioni ya watu ulimwenguni pote kusikia “habari njema za wokovu.”—Zaburi 96:2.

Je, kuna mtu yeyote ambaye ungependa kuzungumza naye kuhusu habari njema za Ufalme wa Mungu, na jinsi anavyoweza kufaidika wakati ujao? Zungumza naye mara tu upatapo fursa!

  • Ni “habari njema” zipi zinazohitaji kutangazwa?

  • Mashahidi wa Yehova wanaigaje mbinu ya Yesu ya kuhubiri?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Mwombe yule anayejifunza Biblia pamoja nawe akuonyeshe jinsi unavyoweza kuzungumza kwa busara pamoja na mtu unayemfahamu kuhusu jambo ambalo umejifunza katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki