Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 17
  • Waangalizi wa Mzunguko Wanatusaidiaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waangalizi wa Mzunguko Wanatusaidiaje?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Waangalizi Wasafirio—Wafanyi-Kazi-Wenzi Katika Ukweli
    Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote
  • Waangalizi Wasafirio—Zawadi Zikiwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Waangalizi Wanaochunga Kundi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Jinsi Ambavyo Waangalizi Wasafirio Hutumikia Wakiwa Wasimamizi-Nyumba Waaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 17

SOMO LA 17

Waangalizi wa Mzunguko Wanatusaidiaje?

Mwangalizi wa mzunguko na mke wake

Malawi

Mwangalizi wa mzunguko akiongoza mkutano wa utumishi wa shambani

Kikundi cha utumishi

Mwangalizi wa mzunguko akihubiri hadharani

Huduma ya shambani

Mwangalizi wa mzunguko akiwa kwenye kikao pamoja na wazee wa kutaniko

Mkutano wa wazee

Biblia huwataja mara kadhaa Barnaba na mtume Paulo. Wanaume hao walikuwa waangalizi wanaosafiri, wakiyatembelea makutaniko ya karne ya kwanza. Kwa nini? Walihangaikia kikweli hali ya ndugu zao wa kiroho. Paulo alisema kwamba alitaka ‘kurudi akawatembelee akina ndugu’ ili aone jinsi wanavyoendelea. Alikuwa tayari kusafiri mamia ya kilometa kwenda kuwaimarisha. (Matendo 15:36) Hiyo ndiyo tamaa ya waangalizi wa mzunguko leo.

Wanakuja kututia moyo. Kila mwangalizi wa mzunguko hutembelea makutaniko 20 hivi. Yeye hukaa katika kila kutaniko kwa muda wa juma moja, mara mbili kila mwaka. Tunaweza kufaidika sana kutokana na uzoefu wa ndugu hao na wake zao pia, ikiwa wameoa. Wanajitahidi kuwafahamu vizuri vijana kwa wazee, nao wana hamu ya kuandamana pamoja nasi katika huduma ya shambani na kwa wale tunaojifunza nao Biblia. Waangalizi hao huandamana pamoja na wazee kufanya ziara za uchungaji. Ili kutuimarisha, wao hutoa hotuba zenye kutia moyo katika mikutano na makusanyiko.—Matendo 15:35.

Wanapendezwa na wote kutanikoni. Waangalizi wa mzunguko wanapendezwa sana na hali ya kiroho ya makutaniko. Wao hufanya mkutano pamoja na wazee na watumishi wa huduma ili kuzungumzia maendeleo ambayo yamefanywa na kuwapa mapendekezo kuhusu jinsi ya kushughulikia majukumu yao. Wanawasaidia mapainia kupata mafanikio katika huduma yao, nao hufurahia kuwajua wapya na kusikia kuhusu maendeleo yao ya kiroho. Kila mmoja wa ndugu hao hujitoa kwa hiari akiwa “mfanyakazi mwenzi kwa ajili ya faida [yetu].” (2 Wakorintho 8:23) Tunapaswa kuiga imani yao na roho yao ya kujitoa kufanya mapenzi ya Mungu.—Waebrania 13:7.

  • Kwa nini waangalizi wa mzunguko hutembelea makutaniko?

  • Unaweza kufaidika jinsi gani kutokana na ziara zao?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Tia alama katika kalenda yako tarehe ya ziara ijayo ya mwangalizi wa mzunguko katika kutaniko lenu ili usikose kusikiliza hotuba zake kwenye Jumba la Ufalme. Ikiwa ungependa yeye au mke wake awepo wakati mnapojifunza Biblia juma hilo ili upate kumfahamu, mjulishe yule unayejifunza naye Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki