Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 18
  • Tunawasaidiaje Ndugu Zetu Wakati wa Taabu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunawasaidiaje Ndugu Zetu Wakati wa Taabu?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mashahidi wa Yehova Hutoa Misaada Wakati wa Misiba?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Kazi ya Kutoa Msaada
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Jinsi ya Kusaidia Baada ya Janga
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2023
  • Tunaweza Kusaidiaje?
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 18

SOMO LA 18

Tunawasaidiaje Ndugu Zetu Wakati wa Taabu?

Mashahidi wa Yehova wakitoa msaada baada ya janga katika Jamhuri ya Dominika

Jamhuri ya Dominika

Wajitoleaji wakijenga upya Jumba la Ufalme nchini Japani

Japani

Shahidi wa Yehova akimfariji mtu baada ya janga nchini Haiti

Haiti

Janga linapotokea, mara moja Mashahidi wa Yehova hupanga kuwasaidia ndugu zao ambao wanahitaji msaada. Jitihada hizo huonyesha upendo wa kweli tulio nao. (Yohana 13:34, 35; 1 Yohana 3:17, 18) Tunatoa msaada katika njia zipi?

Tunatoa msaada wa kifedha. Njaa kali ilipotokea Yudea, Wakristo wa karne ya kwanza huko Antiokia waliwatumia ndugu zao wa kiroho msaada wa kifedha. (Matendo 11:27-30) Vivyo hivyo, tunaposikia kwamba ndugu zetu katika sehemu nyingine za dunia wanakabili hali ngumu, tunatuma fedha kupitia kutaniko letu ili kuwasaidia.—2 Wakorintho 8:13-15.

Tunatoa huduma zinazohitajika. Wazee wanaotumikia katika eneo lililokumbwa na janga hujitahidi kuwasiliana na kila mshiriki wa kutaniko na kuhakikisha wote wako salama. Halmashauri ya kutoa misaada inaweza kuratibu kugawanywa kwa chakula, maji safi ya kunywa, nguo, makao, na matibabu. Mashahidi wengi wenye ujuzi hujitolea kusafiri kwa gharama zao wenyewe ili kushiriki katika kazi hiyo ya kutoa misaada au kurekebisha nyumba na Majumba ya Ufalme yaliyoharibiwa. Umoja tunaofurahia tukiwa tengenezo na uzoefu ambao tumepata kwa kufanya kazi pamoja, hutuwezesha kupanga mambo haraka uhitaji unapotokea. Ijapokuwa sisi huwasaidia “wale ambao ni ndugu zetu katika imani,” tunawasaidia wengine pia iwezekanapo, haidhuru dini yao.—Wagalatia 6:10.

Tunatoa msaada wa kiroho na faraja. Waliokumbwa na janga mara nyingi huhitaji faraja. Katika nyakati hizo, tunatiwa nguvu na Yehova, “Mungu wa faraja yote.” (2 Wakorintho 1:3, 4) Tunafurahia kuzungumza pamoja na wale walio katika hali hizo kuhusu ahadi za Biblia zinazowahakikishia kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utakomesha majanga yote yanayosababisha uchungu na kuteseka.—Ufunuo 21:4.

  • Kwa nini Mashahidi huitikia haraka majanga yanapotokea?

  • Ni ujumbe gani wa kiroho wenye kufariji tunaoweza kuzungumzia na watu waliokabili hali ngumu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki