Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 22
  • Ni Kazi Gani Zinazofanywa Katika Ofisi ya Tawi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Kazi Gani Zinazofanywa Katika Ofisi ya Tawi?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Barua Kutoka Ofisi ya Tawi
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Ya Kwanza Miaka 100 Iliyopita
    Amkeni!—2000
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Jinsi Ambavyo Baraza Linaloongoza Limepangwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 22

SOMO LA 22

Ni Kazi Gani Zinazofanywa Katika Ofisi ya Tawi?

Kikundi cha wanaume wakipanga kazi katika ofisi ya tawi kwenye visiwa vya Solomon

Visiwa vya Solomon

Shahidi wa Yehova akifanya kazi katika ofisi ya tawi nchini Kanada

Kanada

Magari ya kusafirisha machapisho

Afrika Kusini

Wanabetheli wanafanya kazi katika idara mbalimbali zinazosimamia kazi ya kuhubiri katika nchi moja au kadhaa. Huenda baadhi yao wanafanya kazi katika idara ya kutafsiri, kuchapisha magazeti, kutengeneza vitabu, sauti au video, au idara nyingine zinazoshughulikia mambo yanayohusu eneo linalosimamiwa na ofisi ya tawi.

Halmashauri ya Tawi husimamia utendaji. Baraza Linaloongoza limeikabidhi Halmashauri ya Tawi jukumu la kusimamia utendaji wa ofisi ya tawi. Kwa kawaida halmashauri hiyo huwa na wazee watatu au zaidi wanaostahili. Halmashauri ya tawi hulijulisha Baraza Linaloongoza maendeleo ya utendaji mbalimbali katika eneo lililo chini ya usimamizi wake na pia kuhusu matatizo yoyote yanayoweza kutokea. Ripoti hizo hulisaidia Baraza Linaloongoza kuamua habari zinazohitaji kuandikwa katika machapisho na zinazohitaji kuzungumziwa katika mikutano na makusanyiko. Wawakilishi wa Baraza Linaloongoza hutumwa kwa ukawaida kwenye ofisi za tawi ili kuzipatia mwongozo Halmashauri za Tawi kuhusu jinsi ya kufanya kazi zao. (Methali 11:14) Programu ya pekee inayotia ndani hotuba ambayo hutolewa na mwakilishi wa makao makuu huandaliwa ili kuwatia moyo wale wanaoishi katika eneo lililo chini ya usimamizi wa ofisi ya tawi.

Makutaniko yanapata utegemezo. Ndugu waliowekwa katika ofisi ya tawi huidhinisha kuanzishwa kwa makutaniko mapya. Akina ndugu hutoa mwongozo kuhusu utendaji wa mapainia, wamishonari, na waangalizi wa mzunguko ambao wanatumikia katika eneo lililo chini ya ofisi ya tawi. Wanapanga makusanyiko, wanaratibu ujenzi wa Majumba ya Ufalme, na kuhakikisha kwamba machapisho yamefika kwenye makutaniko. Kazi zote zinazofanywa katika ofisi ya tawi huchangia umoja na upatano katika kutimiza kazi ya kuhubiri.—1 Wakorintho 14:33, 40.

  • Halmashauri za Tawi hulisaidiaje Baraza Linaloongoza?

  • Ni majukumu gani yanayotimizwa katika ofisi ya tawi?

PATA KUJUA MENGI ZAIDI

Wageni wanakaribishwa kutembelea ofisi yoyote ya tawi, kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa. Wewe pia unakaribishwa. Unapotembelea ofisi ya tawi, valia kama unavyovalia unapohudhuria mikutano yetu. Imani yako itaimarishwa unapotembelea Betheli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki