Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fg somo la 14 maswali 1-4
  • Kwa Nini Mungu Ana Kikundi au Tengenezo la Watu Wanaomwabudu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Mungu Ana Kikundi au Tengenezo la Watu Wanaomwabudu?
  • Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Mungu Amewapanga Watu Wake kwa Utaratibu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tumefanywa Tengenezo Tumtumikie Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Tengenezo la Mungu Linaloonekana
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Je, Mungu Ana Watu Wanaomtumikia kwa Utaratibu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
fg somo la 14 maswali 1-4

SOMO LA 14

Kwa Nini Mungu Ana Kikundi au Tengenezo la Watu Wanaomwabudu?

1. Kwa nini Mungu alianzisha taifa la Israeli?

1. Watu wa Mungu katika Israeli ya kale; 2. Wakristo wa Karne ya kwanza wakifanya kazi ya kuhubiri kwa utaratibu

Mungu aliwafanya wazao wa Abrahamu kuwa taifa naye akawapa sheria. Aliliita taifa hilo “Israeli” na kulipatia jukumu la kuendeleza ibada ya kweli na kulitunza neno lake. (Zaburi 147:19, 20) Kwa hiyo, kupitia taifa la Israeli, watu wa mataifa mengine wangefaidika.​—Soma Mwanzo 22:18.

Mungu aliwachagua Waisraeli wawe mashahidi wake. Historia yao ya kale inathibitisha jinsi ambavyo watu hufaidika wanapotii sheria za Mungu. (Kumbukumbu la Torati 4:6) Kwa hiyo, kupitia taifa la Israeli, watu wa mataifa mengine wangeweza kumjua Mungu wa kweli.​—Soma Isaya 43:10, 12.

2. Kwa nini Wakristo wa kweli wanamwabudu Mungu wakiwa kikundi?

Baada ya muda, Waisraeli walipoteza kibali cha Mungu, hivyo Yehova akachagua kutaniko la Kikristo lichukue mahali pa taifa hilo. (Mathayo 21:43; 23:37, 38) Leo, Wakristo wa kweli ndio wanaotumikia wakiwa mashahidi wa Yehova.​—Soma Matendo 15:14, 17.

Yesu aliwazoeza wafuasi wake wakiwa kikundi ili watekeleze kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kutoka katika mataifa yote. (Mathayo 10:7, 11; 24:14; 28:19, 20) Kazi hiyo inakaribia mwisho wake kwenye umalizio wa mfumo huu wa mambo. Kwa mara ya kwanza katika historia, Yehova ameunganisha mamilioni ya watu kutoka katika mataifa yote kwenye ibada ya kweli. (Ufunuo 7:9, 10) Wakristo wa kweli humwabudu Mungu wakiwa kikundi, au kutaniko, kwa kusudi la kutiana moyo na kusaidiana. Wanafurahia programu ileile ya mafundisho ya Biblia kwenye mikutano yao ulimwenguni pote.​—Soma Waebrania 10:24, 25.

3. Katika nyakati zetu, tengenezo la Mashahidi wa Yehova lilianzaje?

Picha za Mashahidi wa Yehova wakihubiri katika miaka ya 1900 na pia leo; machapisho ya kujifunzia Biblia katika lugha nyingi.

Katika miaka ya 1870, kikundi kidogo cha wanafunzi wa Biblia kilianza kuelewa kweli za Biblia ambazo hazikuwa zikijulikana kwa muda mrefu. Walijua kwamba Yesu alikuwa ameanzisha kutaniko la Kikristo kwa kusudi la kuhubiri. Hivyo, walianza kampeni ya kuhubiri kuhusu Ufalme ulimwenguni pote. Katika mwaka wa 1931 walianza kutumia jina Mashahidi wa Yehova.​—Soma Matendo 1:8; 2:1, 4; 5:42.

4. Mashahidi wa Yehova wanasimamiwaje?

Katika karne ya kwanza, makutaniko ya Kikristo katika maeneo mengi yalipata mwongozo kutoka kwa baraza linaloongoza ambalo lilimtambua Yesu kuwa Kichwa cha kutaniko. (Matendo 16:4, 5) Vivyo hivyo leo, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote hupata mwongozo kutoka kwa Baraza Linaloongoza lenye wazee wenye uzoefu. Baraza hilo linasimamia ofisi za tawi za Mashahidi wa Yehova ambazo zinafanya kazi ya kutafsiri, kuchapa, na kugawa vifaa vinavyotumiwa kwa ajili ya kujifunza Biblia katika lugha zaidi ya 600. Hivyo, Baraza Linaloongoza linaweza kuandaa kitia-moyo cha Kimaandiko na mwongozo kwa ajili ya makutaniko zaidi ya 100,000 ulimwenguni pote. Katika kila kutaniko, wanaume wanaostahili wanatumikia wakiwa wazee, au waangalizi. Wanaume hao wanalitunza kundi la Mungu kwa upendo.​—Soma 1 Petro 5:2, 3.

Mashahidi wa Yehova hufuata utaratibu wanapofanya kazi ya kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi. Kama walivyofanya mitume, Mashahidi wa Yehova wanahubiri nyumba kwa nyumba. (Matendo 20:20) Pia, hujitolea kujifunza Biblia kibinafsi na watu wanyoofu wanaoipenda kweli. Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova si kikundi au tengenezo tu. Sisi ni familia yenye Baba mwenye upendo. Sisi ni ndugu na dada tunaohangaikiana. (2 Wathesalonike 1:3) Kwa kuwa watu wa Yehova wanazingatia kumpendeza Mungu na kuwasaidia wengine, wao ni familia yenye furaha zaidi duniani.​—Soma Zaburi 33:12; Matendo 20:35.

Unaweza kupata habari zaidi katika sura ya 19 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki