Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jy sura 18 uku. 46-uku. 47 fu. 6
  • Yesu Aongezeka Naye Yohana Apungua

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Aongezeka Naye Yohana Apungua
  • Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Habari Zinazolingana
  • Yohana Apungua, Yesu Azidi
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Yohana Anapungua, Yesu Anazidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Yohana Anataka Kusikia Kutoka kwa Yesu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Yohana Mbatizaji—Mfano Mzuri wa Kudumisha Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 18 uku. 46-uku. 47 fu. 6
Yohana Mbatizaji akizungumza na wanafunzi wake

SURA YA 18

Yesu Aongezeka Naye Yohana Apungua

MATHAYO 4:12 MARKO 6:17-20 LUKA 3:19, 20 YOHANA 3:22–4:3

  • WANAFUNZI WA YESU WABATIZA WATU

  • YOHANA MBATIZAJI AFUNGWA GEREZANI

Baada ya kusherehekea Pasaka katika majira ya kuchipua ya mwaka wa 30 W.K., Yesu na wanafunzi wake wanaondoka Yerusalemu. Hata hivyo, hawarudi moja kwa moja nyumbani kwao huko Galilaya. Wanaenda katika eneo la Yudea, ambako wanabatiza watu wengi. Yohana Mbatizaji amekuwa akifanya kazi kama hiyo kwa karibu mwaka mmoja, na baadhi ya wanafunzi wake bado wako pamoja naye, labda katika bonde la Mto Yordani.

Yesu hambatizi mtu yeyote—wanafunzi wake wanabatiza watu chini ya mwelekezo wake. Katika kipindi hiki cha huduma ya Yesu, Yesu na Yohana wanawafundisha Wayahudi ambao wanatubu dhambi walizotenda dhidi ya agano la Sheria ya Mungu.—Matendo 19:4.

Lakini wanafunzi wa Yohana wanaona wivu, wanamlalamikia kumhusu Yesu: “Mtu [Yesu] aliyekuwa pamoja nawe . . . anabatiza na watu wote wanaenda kwake.” (Yohana 3:26) Lakini Yohana hana wivu. Anashangilia mafanikio ya Yesu na anataka wanafunzi wake washangilie pia. Yohana anawakumbusha: “Ninyi wenyewe mlishuhudia kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, bali, nimetumwa nimtangulie.’” Anatoa mfano kuhusu jambo hilo ili wote waelewe: “Yule aliye na bibi harusi ndiye bwana harusi. Hata hivyo, rafiki ya bwana harusi, anaposimama na kumsikia, anashangilia sana kwa sababu ya sauti ya bwana harusi. Kwa hiyo shangwe yangu imekamilishwa.”—Yohana 3:28, 29.

Kama rafiki ya bwana harusi, Yohana alishangilia miezi kadhaa iliyopita alipowatambulisha wanafunzi wake kwa Yesu. Baadhi yao walimfuata Yesu na baada ya muda wangetiwa mafuta kwa roho takatifu. Yohana anataka pia wanafunzi wake wa sasa wamfuate Yesu. Kwa kweli, kusudi la Yohana ni kutayarisha njia kwa ajili ya huduma ya Yesu. Yohana anaeleza hivi: “Huyo lazima aendelee kuongezeka, lakini mimi lazima niendelee kupungua.”—Yohana 3:30.

Yohana mwingine, ambaye hapo awali alianza kumfuata Yesu, baadaye aliandika hivi kuhusu alikotoka Yesu na jukumu lake muhimu katika kuwaokoa wanadamu: “Yule anayetoka juu yuko juu ya watu wote. . . . Baba anampenda Mwana naye amekabidhi vitu vyote mkononi mwake. Yule anayemwamini Mwana ana uzima wa milele; yule asiyemtii Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu hukaa juu yake.” (Yohana 3:31, 35, 36) Huo ni ukweli muhimu ambao watu wanapaswa kujua!

Yohana Mbatizaji afungwa gerezani

Muda mfupi baada ya Yohana Mbatizaji kusema kwamba jukumu na kazi yake lazima ipungue, anakamatwa na Mfalme Herode. Herode amemchukua Herodia, mke wa Filipo ndugu yake wa kambo, na kumwoa. Yohana anapofunua hadharani kitendo hicho cha uzinzi, Herode anaagiza Yohana afungwe gerezani. Anaposikia kwamba Yohana amekamatwa, Yesu anaondoka Yudea pamoja na wanafunzi wake na ‘kwenda Galilaya.’—Mathayo 4:12; Marko 1:14.

  • Ni nini maana ya ubatizo unaofanywa na Yohana? Ni nini maana ya ubatizo unaofanywa chini ya mwelekezo wa Yesu kabla hajafufuliwa?

  • Yohana anaonyeshaje kwamba wanafunzi wake hawapaswi kuonea wivu kazi ya Yesu?

  • Kwa nini Yohana anafungwa gerezani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki