Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • od sura 15 kur. 157-161
  • Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa Kitheokrasi
  • Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUNAPASWA KUJITIISHA KWA NANI?
  • ‘Tiini’ kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Kile Ambacho Ujitiisho wa Kimungu Wataka Kwetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kujitiisho wa Kimungu—Kwa Nini na kwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Inamaanisha Nini Kuwa Kichwa cha Familia?
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
od sura 15 kur. 157-161

SURA YA 15

Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa Kitheokrasi

NI LAZIMA tujitiishe kwa Mungu, Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, ili tuwe sehemu ya tengenezo linalofanya mapenzi ya Yehova. Tunatambua kwamba Mwana wake ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo na pia tunafuata kanuni ya ukichwa katika mambo mengine maishani. Kila mtu anayejitiisha katika mpango huo wa kitheokrasi hufaidika.

2 Wanadamu walijulishwa kwa mara ya kwanza kabisa kuhusu mpango wa kujitiisha chini ya mamlaka katika bustani ya Edeni. Mpango huo unafafanuliwa katika amri za Mungu zilizo kwenye Mwanzo 1:28 na 2:16, 17. Wanyama wangeongozwa na wanadamu, na Adamu na Hawa walipaswa kujitiisha kwa mapenzi na mamlaka ya Mungu. Kutii mamlaka ya Mungu kungeleta amani na utaratibu mzuri. Kanuni ya ukichwa inakaziwa tena katika 1 Wakorintho 11:3. Mtume Paulo aliandika hivi: “Nataka mjue kwamba kichwa cha kila mwanamume ni Kristo; nacho kichwa cha mwanamke ni mwanamume; nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.” Hilo linaonyesha kwamba kila mtu yuko chini ya ukichwa fulani katika mpango huo, isipokuwa Yehova.

3 Watu wengi leo hawaheshimu wala kutii kanuni ya ukichwa. Kwa nini? Tatizo lilianzia Edeni wazazi wa wanadamu walipochagua kimakusudi kutojitiisha chini ya ukichwa wa Mungu mwenye enzi kuu. (Mwa. 3:4, 5) Hata hivyo, hawakupata uhuru zaidi. Badala yake, walijitiisha chini ya kiumbe mwovu wa roho, Shetani Ibilisi. Uasi wa kwanza uliwatenganisha wanadamu na Mungu. (Kol. 1:21) Ndiyo sababu wanadamu wengi leo wako chini ya nguvu za yule mwovu.—1 Yoh. 5:19.

4 Tunapojifunza na kuishi kupatana na kweli ya Neno la Mungu, tunakataa kuongozwa na uvutano wa Shetani. Tukiwa Mashahidi waliojiweka wakfu na kubatizwa, tunamkubali Yehova kuwa Mtawala Mkuu wa maisha yetu. Tunakubaliana na Mfalme Daudi, aliyekiri kwamba Yehova ndiye “mkuu juu ya vyote.” (1 Nya. 29:11) Bila shaka tunakiri hivi kwa unyenyekevu: “Jueni kwamba Yehova ni Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, na sisi ni mali yake. Sisi ni watu wake na kondoo wa malisho yake.” (Zab. 100:3) Tunatambua kwamba Yehova ni mkuu na tunapaswa kujitiisha kwake kikamili kwa kuwa aliumba vitu vyote. (Ufu. 4:11) Tukiwa wahudumu wa Mungu wa kweli, tunamfuata Yesu Kristo, ambaye aliweka kielelezo kikamilifu cha kujitiisha kwa Mungu.

5 Yesu alijifunza nini kutokana na mateso yaliyompata alipokuwa duniani? Andiko la Waebrania 5:8 linajibu hivi: “Ingawa alikuwa mwana, alijifunza kutii kutokana na mateso yaliyompata.” Naam, Yesu aliendelea kujitiisha kwa ushikamanifu kwa Baba yake wa mbinguni hata alipokabili magumu. Zaidi ya hayo, Yesu hakufanya lolote kwa uamuzi wake mwenyewe. Hakusema mambo aliyotunga yeye mwenyewe; wala hakutafuta utukufu wake mwenyewe. (Yoh. 5:19, 30; 6:38; 7:16-18) Wakati wa huduma yake, alifurahia kufanya mapenzi ya Baba yake, hata ingawa alipingwa na kuteswa kwa kufanya hivyo. (Yoh. 15:20) Hata hivyo, Yesu alijitiisha kwa Mungu. Yesu “alijinyenyekeza” mpaka “kifo juu ya mti wa mateso.” Kujitiisha kwake kikamili kwa Yehova kulikuwa na faida nyingi. Kuliwaletea wanadamu wokovu wa milele, kulifanya apandishwe cheo, na kulimtukuza Baba yake.—Flp. 2:5-11; Ebr. 5:9.

TUNAPASWA KUJITIISHA KWA NANI?

6 Tunapojitiisha kwa Mungu kwa kufanya mapenzi yake, tunaepuka mahangaiko na mambo mengi yenye kuvunja moyo yanayowapata wale wanaokataa kujitiisha chini ya enzi kuu ya Yehova. Adui yetu, Ibilisi, hujaribu kila wakati kutumeza. Tutakombolewa kutoka kwa mwovu huyo ikiwa tutachukua msimamo dhidi yake na kujinyenyekeza mbele za Yehova kwa kujitiisha kwake kwa kupenda.—Mt. 6:10, 13; 1 Pet. 5:6-9.

7 Katika kutaniko la Kikristo, tunatambua ukichwa wa Kristo na mamlaka ambayo amempa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” Jambo hilo huathiri jinsi tunavyowaona na kuwatendea wengine kutanikoni. Kujitiisha kwa mpango wa Mungu kutanikoni kutatuchochea kutii Neno la Mungu katika sehemu zote za ibada yetu. Utii huo unatia ndani huduma yetu, kuhudhuria na kushiriki mikutano, uhusiano wetu na wazee, na kuunga mkono mipango ya kitengenezo.—Mt. 24:45-47; 28:19, 20; Ebr. 10:24, 25; 13:7, 17.

8 Kujitiisha kwa Mungu huchangia amani, usalama, na utaratibu mzuri wa kutaniko la Kikristo. Watu wanaojitiisha kwa Mungu huonyesha sifa bora za Yehova. (1 Kor. 14:33, 40) Mambo ambayo tumejionea katika tengenezo la Yehova yametuchochea tuhisi kama Mfalme Daudi. Baada ya kuona tofauti kati ya watumishi wa Yehova na waovu, Daudi aliimba hivi kwa shangwe: “Wenye furaha ni watu ambao Mungu wao ni Yehova!”—Zab. 144:15.

9 Katika mpango wa ndoa na familia, “kichwa cha mwanamke ni mwanamume.” Wakati huohuo, wanaume nao wanapaswa kujitiisha kwa Kristo, nacho Kichwa cha Kristo ni Mungu. (1 Kor. 11:3) Wake wanapaswa kujitiisha kwa waume zao, na watoto kwa wazazi wao. (Efe. 5:22-24; 6:1) Kila mmoja katika familia anapotii kanuni ya ukichwa, kunakuwa na amani.

10 Mume anapaswa kutumia ukichwa kwa upendo, na hivyo kumwiga Kristo. (Efe. 5:25-29) Akitumia vizuri na kutopuuza ukichwa wake, mke na watoto wake hufurahia kujitiisha. Jukumu la mke ni kuwa msaidizi au kikamilisho. (Mwa. 2:18) Anapomheshimu na kumuunga mkono mume wake bila kulalamika, anapata kibali cha mume wake na kumletea Mungu sifa. (1 Pet. 3:1-4) Waume na wake wanapotii shauri la Biblia kuhusu ukichwa, wanawawekea watoto wao mfano mzuri wa kujitiisha kwa Mungu.

Ujitiisho wa kitheokrasi hugusa kila sehemu ya maisha

11 Kujitiisha kwa Mungu huathiri pia mtazamo wetu kuelekea “mamlaka zilizo kubwa,” ambazo “zimewekwa na Mungu katika vyeo vyao vya kadiri.” (Rom. 13:1-7) Wakiwa raia wanaotii sheria, Wakristo hulipa kodi, wakimlipa “Kaisari vitu vya Kaisari, na Mungu vitu vya Mungu.” (Mt. 22:21) Pia, mipango ya kuhubiri eneo kikamili hupatana na sheria za kulinda taarifa zinazotumiwa. Tukijitiisha na kuheshimu mamlaka halali katika mambo yote ambayo hayapingani na sheria ya Yehova ya uadilifu, tutatumia vizuri nguvu zetu zote katika kazi ya kuhubiri.—Marko 13:10; Mdo. 5:29.

12 Ujitiisho wa kitheokrasi hugusa kila sehemu ya maisha. Kwa macho ya imani, tunatazamia kuiona siku ambayo wanadamu wote watajitiisha kwa Yehova Mungu. (1 Kor. 15:27, 28) Wale wanaokubali kwa shangwe enzi kuu ya Yehova watabarikiwa sana wanapoendelea kujitiisha kwake kwa umilele wote!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki