Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 2/1 kur. 9-14
  • Kujitiisho wa Kimungu—Kwa Nini na kwa Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujitiisho wa Kimungu—Kwa Nini na kwa Nani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu kwa Nini Twawiwa na Yehova Mungu Ujitiisho
  • Yesu Kristo, Kielelezo Kikamilifu cha Ujitiisho wa Kimungu
  • Vielelezo vya Kale vya Ujitiisho wa Kimungu
  • Kielelezo cha Paulo cha Ujitiisho
  • Kile Ambacho Ujitiisho wa Kimungu Wataka Kwetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • ‘Tiini’ kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa Kitheokrasi
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Ujitiisho wa Mke—Wamaanisha Nini?
    Amkeni!—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 2/1 kur. 9-14

Kujitiisho wa Kimungu—Kwa Nini na kwa Nani?

“Ee BWANA [Yehova, NW] najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.”—YEREMIA 10:23.

1. Ni namna gani za kujitegemea ambazo zimethaminiwa sana?

Miongoni mwa hati mashuhuri zaidi za kibinadamu ni lile Julisho la Kujitegemea, ambalo kupitia hilo koloni za Uingereza katika Amerika Kaskazini katika karne ya 18 zilijulisha kutotegemea kwazo nchi iliyokuwa ikizitawala, Uingereza. Walitaka uhuru, na kutotegemea udhibiti wa kigeni na uhuru viliambatana pamoja. Kujitegemea kisiasa na kiuchumi kwaweza kuwa na faida kubwa. Katika nyakati za hivi karibuni mabara mengine ya Ulaya ya Mashariki yamesonga kuelekea kujitegemea kisiasa. Hata hivyo, Ni lazima ikubaliwe kwamba katika mabara hayo kujitegemea huko kumeleta matatizo mengi mazito.

2, 3. (a) Ni namna gani ya kujitegemea isiyotamanika? (b) Ukweli huo ulikaziwaje mwanzoni?

2 Ingawa huenda namna-namna za kujitegemea zikawa zenye kutamanika kama nini, kuna namna moja ya kujitegemea isiyotamanika. Hiyo ni ipi? Kutomtegemea Mfanyi wa mwanadamu, Yehova Mungu. Hiyo si baraka bali ni laana. Kwa nini? Kwa sababu mwanadamu hakukusudiwa kamwe atende bila kumtegemea Mfanyi wake, kama vile maneno ya nabii Yeremia yaliyonukuliwa juu yanavyoonyesha vizuri. Yaani, mwanadamu alikusudiwa ajitiishe kwa Mfanyi wake. Kujitiisha kwa Muumba wetu kunamaanisha kumtii.

3 Uhakika huo ulikaziwa watu wa kwanza kwa amri ya Yehova kama ilivyorekodiwa kwenye Mwanzo 2:16, 17: “Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” Kukataa kujitiisha kwa Mfanyi wake kulimletea Adamu na wazao wake wote dhambi, kuteseka, na kifo.—Mwanzo 3:19; Warumi 5:12.

4, 5. (a) Ni nini kimetokea kwa sababu ya wanadamu kukataa kujitiisha kwa Mungu? (b) Ni amri gani ya kiadili isiyoepukika?

4 Kukataa kwa wanadamu kujitiisha kwa Mungu si jambo la hekima na pia si sawa kiadili. Katika ulimwengu hilo limetokeza mweneo mkubwa wa ukosefu wa kufuata sheria, uhalifu, jeuri, na ukosefu wa adili katika ngono pamoja na matunda yao ya magonjwa yenye kupitishwa kingono. Isitoshe, je, si kweli kwamba pigo la leo la uhalifu wa vijana husababishwa hasa na kukataa kwa vijana kujitiisha kwa Yehova, na pia kwa wazazi wao na kwa sheria za nchi? Roho hiyo ya kujitegemea inaonwa katika njia ya ajabu-ajabu na ya ovyoovyo ambayo watu huvalia na katika lugha chafu wanayotumia.

5 Lakini hakuna yeyote awezaye kuponyoka ile sheria ya kiadili ya Muumba isiyoepukika: “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu.”—Wagalatia 6:6, 7.

6, 7. Ni nini shina lenye kusababisha kukataa kujitiisha, kama ionwavyo kwa vielelezo gani?

6 Ni nini shina lenye kusababisha kukataa huko kote kujitiisha? Kwa usahili, ni ubinafsi na kiburi. Ndiyo sababu Hawa, mwanamke wa kwanza, alijiachilia adanganywe na nyoka na kushiriki lile tunda lililokataliwa. Kama angalikuwa mwenye kiasi na mnyenyekevu, kile kishawishi cha kuwa kama Mungu—kujiamulia mwenyewe yaliyo mema na mabaya—kusingalimvutia. Na kama asingalikuwa na ubinafsi, asingalitaka kitu kilichokuwa kimekatazwa kwa wazi na Mfanyi wake, Yehova Mungu.—Mwanzo 2:16, 17.

7 Muda mfupi baada ya Adamu na Hawa kuanguka, kiburi na ubinafsi vilimsababisha Kaini amwue kimakusudi ndugu yake Habili. Pia, ubinafsi uliwasababisha malaika fulani watende kwa kujitegemea, wakiacha mahali pao pa awali na kujivika miili ili kufurahia anasa za mwili. Kiburi na ubinafsi vilimchochea Nimrodi na zimekuwa sifa zenye kutokeza za watawala wengi wa kilimwengu tangu wakati wake.—Mwanazo 3:6, 7; 4:6-8; 1 Yohana 3:12; Yuda 6.

Sababu kwa Nini Twawiwa na Yehova Mungu Ujitiisho

8-11. Ni sababu zipi nne zenye nguvu za kuzoea kwetu ujitiisho wa kimungu?

8 Kwa nini twawiwa na Mfanyi wetu, Yehova Mungu ujitiisho? Kwanza kabisa ni kwa sababu yeye ni Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote Mzima. Mamlaka yote ni haki yake. Yeye ndiye Hakimu, Mpaji-sheria, na Mfalme wetu. (Isaya 33:22) Imeandikwa vema juu yake kwamba: “Hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”—Waebrania 4:13.

9 Isitoshe, kwa kuwa Mfanyi wetu ni mweza yote, hakuna awezaye kumpinga kwa mafanikio; hakuna awezaye kupuuza wajibu wake wa kujitiisha kwake Yeye. Hatimaye, wale wanaokataa wataharibiwa kama vile Farao wa zamani na kama vile Shetani Ibilisi atakavyoharibiwa kwa wakati wa Mungu.—Zaburi 136:1, 11-15; Ufunuo 11:17; 20:10, 14.

10 Ujitiisho ni wajibu wa viumbe vyote wenye akili kwa sababu wako kwa kusudi la kutumikia Mfanyi wao. Ufunuo 4:11 hujulisha hivi: “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea utukufu na heshima na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.” Yeye ndiye Mfinyanzi-Vyombo Mkuu, na yeye hufanya vyombo vya kibinadamu vitumikie kusudi lake.—Isaya 29:16; 64:8.

11 Hatupaswi kupuuza ukweli wa kwamba Mfanyi wetu ni mwenye hekima yote, kwa hiyo yeye ajua yaliyo bora zaidi kwetu. (Warumi 11:33) Sheria zake ni za ‘faida yetu.’ (Kumbukumbu la Torati 10:12, 13, NW) Zaidi ya yote, “Mungu ni upendo,” kwa hiyo yeye ataka tu yaliyo bora zaidi kwetu. Tuna sababu nyingi kama nini za kujitiisha kwa Mfanyi wetu, Yehova Mungu!—1 Yohana 4:8.

Yesu Kristo, Kielelezo Kikamilifu cha Ujitiisho wa Kimungu

12, 13. (a) Yesu Kristo alidhihirishaje ujitiisho wa kimungu? (b) Ni maneno gani ya Yesu yanayoonyesha mtazamo wake wenye unyenyekeo?

12 Pasipo na shaka yoyote Mwana wa Yehova, Yesu Kristo, atutolea kielelezo kikamilifu cha ujitiisho wa kimungu. Mtume Paulo aeleza hilo kwenye Wafilipi 2:6-8: “[Ingawa Yesu Kristo] alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba [mti wa mateso, NW].” Alipokuwa duniani, Yesu alisema tena na tena kwamba hakufanya chochote uanzishi wake mwenyewe; hakutenda kwa kujitegemea, bali sikuzote alidumisha ujitiisho kwa Baba yake wa kimbingu.

13 Twasoma hivi kwenye Yohana 5:19, 30: “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo atendayo Mwana vile vile. Mimi siwezi kufanya neno mwenyewe; kama nisikiavyo ndivyo nihukumuvyo; na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu siyatafuti mapenzi yangu mimi, bali mapenzi yake aliyenipeleka.” Vilevile, alisali hivi tena na tena usiku wa kusalitiwa kwake: “Si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.”—Mathayo 26:39, 42, 44; ona pia Yohana 7:28; 8:28, 42.

Vielelezo vya Kale vya Ujitiisho wa Kimungu

14. Noa alionyesha ujitiisho wa kimungu katika njia zipi?

14 Miongoni mwa vielelezo vya mapema vya kibinadamu vya ujitiisho wa kimungu alikuwa Noa. Alionyesha ujitiisho wake katika njia tatu. Kwanza, kwa kuwa mwanamume mwadilifu, bila hitilafu miongoni mwa marika wake, akitembea pamoja na Mungu wa kweli. (Mwanzo 6:9) Pili, kwa kujenga safina. “Sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu hivyo ndivyo alivyofanya.” (Mwanzo 6:22) Tatu, kwa kuvumisha onyo la kuja kwa Gharika akiwa “mhubiri wa uadilifu.”—2 Petro 2:5, NW.

15, 16. (a) Abrahamu aliweka kielelezo gani kizuri katika ujitiisho wa kimungu? (b) Sara alionyeshaje ujitiisho?

15 Abrahamu alikuwa kielelezo kingine chenye kutokeza cha ujitiisho wa kimungu. Alidhihirisha ujitiisho kwa kutii amri hii ya Mungu: “Toka wewe katika nchi yako.” (Mwanzo 12:1) Hilo lilimaanisha kuacha mazingira yake yenye ustarehe katika Uru (ambalo halikuwa jiji duni, kama ionyeshwavyo na mavumbuzi ya kiakiolojia) azurure huku na huku akiwa mhamiaji katika bara la kigeni kwa muda wa miaka mia moja. Abrahamu alionyesha ujitiisho wa kimungu hasa kwa kukabiliana na ule mtihani mkubwa wa kuwa na nia ya kumtoa mwana wake Isaka.—Mwanzo 22:1-12.

16 Sara mke wa Abrahamu, atutolea kielelezo kingine kizuri cha ujitiisho wa kimungu. Kuzurura huku na huku katika bara la kigeni kwa hakika kulileta hali nyingi zisizofaa, lakini hatusomi popote juu ya yeye akilalamika. Aliweka kielelezo kizuri cha ujitiisho wa kimungu katika zile pindi mbili ambazo Abrahamu alimjulisha kuwa dada yake mbele ya watawala wapagani. Nyakati zote mbili alishirikiana, hata ingawa alikuwa karibu awe mshiriki wa masuria wao kwa sababu ya hilo. Ikithibitisha ujitiisho wake wa kimungu ni njia yake ya kumwita mume wake, Abrahamu, “Bwana” moyoni mwake, akionyesha kwamba ujitiisho huo ulikuwa mtazamo wa kweli wa moyo wake.—Mwanzo 12:11-20; 18:12; 20:2-18; 1 Petro 3:6.

17. Kwa nini inaweza kusemwa kwamba Isaka alionyesha ujitiisho wa kimungu?

17 Acheni tusipuuze kielelezo cha ujitiisho wa kimungu kilichotolewa na mwana wa Abrahamu Isaka. Mapokeo ya Kiyahudi huonyesha kwamba Isaka alikuwa karibu mwenye miaka 25 wakati Yehova alipomwamuru baba yake Abrahamu, amtoe kuwa dhabihu. Kama Isaka angalitaka, angalimpinga baba yake kwa urahisi, aliyekuwa na umri wa miaka mia moja zaidi ya yeye. Lakini sivyo. Ingawa Isaka alitaka kujua juu ya kutokuwako kwa mnyama kwa ajili ya dhabihu, alijitiisha kinyenyekevu kwa baba yake alipomweka juu ya madhabahu na kisha kumfunga mikono na miguu ili kuzuia au kudhibiti maitikio yoyote yasiyokusudiwa ambayo huenda ikawa yangetokea ikiwa kisu cha kuchinjia kingetumiwa.—Mwanzo 22:7-9.

18. Musa alionyeshaje kielelezo kizuri cha ujitiisho wa kimungu?

18 Miaka kadhaa baadaye, Musa alituwekea kielelezo kizuri katika ujitiisho wa kimungu. Kwa kweli hilo laonyeshwa na kusimuliwa kwake kuwa “mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.” (Hesabu 12:3) Kutimiza kwake amri za Yehova kwa utii kwa muda wa miaka 40 jangwani, hata ingawa alikuwa na uangalizi wa watu waasi waliohesabika kuwa milioni mbili au tatu, kulithibitisha zaidi ujitiisho wake wa kimungu. Hivyo rekodi yasema kwamba “Musa akafanya hayo yote; kama yote BWANA [Yehova, NW] aliyoagiza ndivyo alivyofanya.”—Kutoka 40:16.

19. Ayubu alionyesha ujitiisho wake kwa Yehova kwa maneno gani?

19 Ayubu ni mtu mwingine mwenye kutokeza aliyetuwekea kielelezo bora sana katika ujitiisho wa kimungu. Baada ya Yehova kumruhusu Shetani afagilie mbali mali zote za Ayubu, awaue watoto wake, na kisha kumpiga kwa “majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa,” mke wa Ayubu alimwambia hivi: “Je! wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? umkufuru Mungu, ukafe.” Hata hivyo, Ayubu alionyesha ujitiisho wake wa kimungu kwa kumwambia hivi: “Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya?” (Ayubu 2:7-10) Yakionyesha mtazamo uo huo wa akili ni maneno yake yaliyorekodiwa kwenye Ayubu 13:15: “Ajaponiua, nitamngojea vivyo.” Ingawa kwa kweli, Ayubu alihangaikia sana juu ya kujitetea kwake mwenyewe, hatupaswi kupuuza kwamba hatimaye Yehova alimwambia hivi mmoja wa wale waliokuwa eti wafariji wake: “Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.” Bila shaka, Ayubu anatutolea kielelezo kizuri cha unyenyekeo wa kimungu.—Ayubu 42:7.

20. Daudi alionyesha ujitiisho wa kimungu katika njia zipi?

20 Kutaja kielelezo kinginecho kimoja tu kutoka kwa Maandiko ya Kiebrania, ni Daudi. Wakati Mfalme Sauli alipomwinda Daudi kana kwamba alikuwa ni mnyama, Daudi alikuwa na nafasi mbili za kumaliza taabu zake kwa kumchinja Sauli. Hata hivyo, ujitiisho wa kimungu wa Daudi ulimzuia asifanye hivyo. Maneno yake yamerekodiwa kwenye 1 Samweli 24:6: “Hasha! nisimtendee bwana wangu masihi wa BWANA [Yehova, NW], neno hili, kuunyosha mkono wangu juu yake, kwa maana yeye ni masihi wa Bwana.” (Ona pia 1 Samweli 26:9-11.) Yeye vilevile alionyesha ujitiisho wake wa kimungu kwa kukubali karipio alipofanya makosa au kutenda dhambi.—2 Samweli 12:13; 24:17; 1 Mambo ya Nyakati 15:13.

Kielelezo cha Paulo cha Ujitiisho

21-23. Mtume Paulo alionyesha ujitiisho wa kimungu katika visa gani mbalimbali?

21 Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, tuna kielelezo chenye kutokeza cha ujitiisho wa kimungu cha mtume Paulo. Alimwiga Bwana Mkubwa wake, Yesu Kristo, katika hilo kama alivyomwiga katika sehemu nyinginezo za huduma yake ya kimitume. (1 Wakorintho 11:1) Ingawa Yehova Mungu alimtumia kwa njia kubwa zaidi ya yeyote kati ya wale mitume wengine, Paulo hakutenda kamwe kwa kujitegemea. Luka atuambia kwamba wakati swali lilipotokea kuhusu kama waongofu wasio Wayahudi walihitaji kutahiriwa, “ndugu [wa Antiokia] wakaamuru kwamba Paulo na Barnaba na wengine miongoni mwao wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee kwa habari ya swali hilo.”—Matendo 15:2.

22 Kwa habari ya utendaji wa Paulo wa umishonari, tunaambiwa hivi kwenye Wagalatia 2:9: “Walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo, na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara.” Kuliko kutenda kwa kujitegemea, Paulo alitafuta mwelekezo.

23 Vivyo hivyo, Paulo alipokuwa Yerusalemu, kwa mara ya mwisho alikubali lile shauri alilopewa na wazee huko kuhusu kwenda kwenye hekalu na kufuata utaratibu wa Sheria ili wote waweze kuona kwamba hakuwa mwasi-imani kwa habari ya Sheria ya Musa. Kwa kuwa kufanya kwake hivyo kulionekana kuwa kulikuwa na matokeo mabaya kikundi chenye ghasia kikichochewa dhidi yake, je, ujitiisho wake kwa wazee hao kulikuwa kosa? Hasha, kama ionyeshwavyo kutokana na yale tunayosoma kwenye Matendo 23:11: “Usiku ule Bwana akasimama karibu naye, akasema, Uwe na moyo mkuu; kwa sababu, kama ulivyonishuhudia habari zangu Yerusalemu, imekupasa kunishuhudia vivyo hivyo Rumi nako.”

24. Ni sehemu zipi zaidi za ujitiisho zitakazozungumzwa katika makala ifuatayo?

24 Kwa kweli, Maandiko hutupa sisi sababu zenye nguvu za sisi kujitiisha na vielelezo vyenye kutokeza vya wale waliodhihirisha ujitiisho huo. Katika makala ifuatayo, tutachunguza hali mbalimbali ambamo twaweza kujitiisha kwa Yehova Mungu, misaada ya kufanya hivyo kwetu, na thawabu zinazotokea.

Ungejibuje?

◻ Ni namna gani ya kujitegemea isiyotamanika?

◻ Ni nini shina lenye kusababisha kukataa kujitiisha?

◻ Twawiwa na Yehova ujitiisho kwa sababu zipi?

◻ Maandiko hutoa vielelezo gani vizuri vya ujitiisho wa kimungu?

[Picha katika ukurasa wa 10]

Nimrodi, mtawala wa kwanza wa baada ya furiko

kuasi ujitiisho wa kimungu

[Picha katika ukurasa wa 13]

Noa, kielelezo kisicho na hitilafu cha ujitiisho wa kimungu.—Mwanzo 6:14, 22

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki