Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • od kur. 185-192
  • Sehemu ya 1: Mafundisho ya Kikristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sehemu ya 1: Mafundisho ya Kikristo
  • Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ujumbe Ambao Ni Lazima Tuutangaze
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Siku za Ushetani Zimehesabiwa
    Amkeni!—1994
  • Sala
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
od kur. 185-192

MASWALI KWA AJILI YA WALE WANAOTAKA KUBATIZWA

Sehemu ya 1: Mafundisho ya Kikristo

Kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kumekusaidia kuijua kweli. Bila shaka, mambo uliyojifunza yamekusaidia kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu na kukupatia tumaini la baraka na uzima wa wakati ujao katika dunia paradiso chini ya Ufalme wa Mungu. Imani yako katika Neno la Mungu imeimarishwa, na tayari umepata baraka nyingi kwa kushirikiana na kutaniko la Kikristo. Umejionea jinsi Yehova anavyoshughulika na watu wake leo.—Zek. 8:23.

Unapojiandaa kwa ajili ya ubatizo, utafaidika kwa kupitia mafundisho ya msingi ya Kikristo pamoja na wazee wa kutaniko. (Ebr. 6:1-3) Yehova na aendelee kukubariki unapojitahidi kuendelea kumjua, na akupe thawabu aliyoahidi.—Yoh. 17:3.

1. Kwa nini unataka kubatizwa?

2. Yehova ni nani?

• “Yehova ndiye Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani. Hakuna mwingine.”—Kum. 4:39.

• “Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zab. 83:18.

3. Kwa nini ni muhimu utumie jina binafsi la Mungu?

• “Basi, salini hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.’”—Mt. 6:9.

• “Kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”—Rom. 10:13.

4. Biblia inatumia baadhi ya maneno gani kumfafanua Yehova?

• “Yehova, Muumba wa miisho ya dunia, ni Mungu kwa umilele wote.”—Isa. 40:28.

• “Baba yetu uliye mbinguni.”—Mt. 6:9.

• “Mungu ni upendo.”—1 Yoh. 4:8.

5. Unaweza kumpa nini Yehova Mungu?

• “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.”—Marko 12:30.

• “Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.”—Luka 4:8.

6. Kwa nini unataka kuwa mshikamanifu kwa Yehova?

• “Uwe na hekima, mwanangu, na kuufanya moyo wangu ushangilie, ili niweze kumjibu yule anayenidhihaki.”—Met. 27:11.

7. Unasali kwa nani, na kupitia kwa jina la nani?

• “Kwa kweli ninawaambia, mkimwomba Baba jambo lolote, atawapa katika jina langu [Yesu].”—Yoh. 16:23.

8. Unaweza kusali kuhusu mambo gani?

• “Basi, salini hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. Utupatie leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii; na utusamehe madeni yetu, kama vile tunavyowasamehe wadeni wetu. Na usituingize katika majaribu, bali utukomboe kutoka kwa yule mwovu.’”—Mt. 6:9-13.

• “Huu ndio uhakika tulio nao kwake, kwamba tukiomba chochote kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.”—1 Yoh. 5:14.

9. Ni nini kinachoweza kumfanya Yehova asisikilize sala ya mtu?

• “Watamlilia Yehova awasaidie, lakini hatawajibu . . . kwa sababu ya matendo yao maovu.”—Mika 3:4.

• “Macho ya Yehova yanawatazama waadilifu, na masikio yake yanasikiliza dua yao, lakini uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda maovu.”—1 Pet. 3:12.

10. Yesu Kristo ni nani?

• “Simoni Petro akajibu: ‘Wewe ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.’” —Mt. 16:16.

11. Kwa nini Yesu alikuja duniani?

• “Mwana wa binadamu [alikuja], si kuhudumiwa, bali kuhudumu na kutoa uhai wake uwe fidia badala ya wengi.”—Mt. 20:28.

• “Ni lazima pia nitangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu katika majiji mengine, kwa sababu nilitumwa [Yesu] kufanya hivyo.”—Luka 4:43.

12. Unaweza kuonyeshaje kwamba unashukuru kwa dhabihu ambayo Yesu alitoa?

• “Alikufa kwa ajili ya wote ili wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili ya yule aliyekufa kwa ajili yao na kufufuliwa.”—2 Kor. 5:15.

13. Yesu ana mamlaka gani?

• “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.”—Mt. 28:18.

• “Mungu alimpandisha kwenye cheo cha juu zaidi na kumpa kwa fadhili jina lililo juu kuliko kila jina lingine.”—Flp. 2:9.

14. Je, unaamini kwamba Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova ni “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” aliyewekwa rasmi na Yesu?

• “Kwa kweli ni nani mtumwa mwaminifu na mwenye busara ambaye bwana wake alimweka rasmi asimamie watumishi wake wa nyumbani na kuwapa chakula chao kwa wakati unaofaa?”—Mt. 24:45.

15. Je, roho takatifu ni mtu?

• “Malaika akamjibu: ‘Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika. Kwa hiyo yule atakayezaliwa ataitwa mtakatifu, Mwana wa Mungu.’”—Luka 1:35.

• “Kwa hiyo, ingawa ninyi ni waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!”—Luka 11:13.

16. Yehova ametumiaje roho yake takatifu?

• “Kwa neno la Yehova mbingu ziliumbwa, na kwa roho ya kinywa chake kila kitu kilichomo kiliumbwa.”—Zab. 33:6.

• “Roho takatifu itakapokuja juu yenu mtapokea nguvu, nanyi mtakuwa mashahidi wangu . . . mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”—Mdo. 1:8.

• “Hakuna unabii wa Andiko unaotokana na fasiri yoyote ya kibinafsi. Kwa maana unabii haukuletwa wakati wowote kwa mapenzi ya mwanadamu, bali wanadamu walisema yaliyotoka kwa Mungu kama walivyoongozwa na roho takatifu.”—2 Pet. 1:20, 21.

17. Ufalme wa Mungu ni nini?

• “Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa kamwe. Na ufalme huo hautakabidhiwa watu wengine wowote. Utazipondaponda na kuzikomesha falme hizi zote, nao pekee utasimama milele.”—Dan. 2:44.

18. Ufalme wa Mungu utakunufaishaje?

• “Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufu. 21:4.

19. Unajuaje kwamba Ufalme utaleta baraka zake hivi karibuni?

• “Wanafunzi wakamkaribia faraghani, wakamuuliza: ‘Tuambie, mambo haya yatatukia lini, na ni nini itakayokuwa ishara ya kuwapo kwako na ya umalizio wa mfumo wa mambo?’ Yesu akawajibu: ‘. . . Taifa litapigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme, kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali. Na hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.’”—Mt. 24:3, 4, 7, 14.

• “Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, wenye kujidai, wenye majivuno, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, waliojaa kiburi, wanaopenda raha badala ya kumpenda Mungu, wakionekana kama watu wanaomwogopa Mungu lakini wakizikana nguvu zake; nawe jiepushe nao.”—2 Tim. 3:1-5.

20. Unaonyeshaje kwamba Ufalme ni jambo la muhimu kwako?

• “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza Ufalme na uadilifu wake.”—Mt. 6:33.

• “Yesu akawaambia wanafunzi wake: ‘Mtu yeyote akitaka kunifuata, lazima ajikane mwenyewe, aubebe mti wake wa mateso na aendelee kunifuata.’”—Mt. 16:24.

21. Shetani na roho waovu ni nani?

• “Ninyi mmetoka kwa baba yenu Ibilisi . . . Alikuwa muuaji alipoanza.”—Yoh. 8:44.

• “Yule joka mkubwa akatupwa chini, yule nyoka wa zamani, anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa; akatupwa chini duniani, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye.”—Ufu. 12:9.

22. Ni mashtaka gani ambayo Shetani ametoa kumwelekea Yehova na watumishi wake?

• “Mwanamke akamjibu nyoka: ‘Tunaweza kula matunda ya miti ya bustani. Lakini Mungu amesema hivi kuhusu matunda ya mti ulio katikati ya bustani: “Msiyale, wala msiyaguse; la sivyo mtakufa.”’ Ndipo nyoka akamwambia mwanamke: ‘Hakika hamtakufa. Kwa maana Mungu anajua kwamba siku ileile mtakapokula matunda ya mti huo, macho yenu yatafunguliwa nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.’”—Mwa. 3:2-5.

• “Shetani akamjibu Yehova: ‘Ngozi kwa ngozi. Mtu atatoa kila kitu alicho nacho ili aokoe uhai wake.’”—Ayu. 2:4.

23. Unaweza kuthibitishaje kwamba mashtaka ya Shetani ni ya uwongo?

• ‘Mtumikie Mungu kwa moyo kamili.’—1 Nya. 28:9.

• “Mpaka nitakapokufa, sitaukana utimilifu wangu!”—Ayu. 27:5.

24. Kwa nini watu wanakufa?

• “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, basi kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.”—Rom. 5:12.

25. Watu waliokufa wako katika hali gani?

• “Walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini waliokufa hawajui jambo lolote kamwe.”—Mhu. 9:5.

26. Kuna tumaini gani kwa watu waliokufa?

• “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.”—Mdo. 24:15.

27. Ni watu wangapi wataenda mbinguni kutawala pamoja na Yesu?

• “Tazama! Mwanakondoo amesimama juu ya Mlima Sayuni, na pamoja naye 144,000 walioandikwa jina lake na jina la Baba yake kwenye mapaji ya nyuso zao.”—Ufu. 14:1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki