Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 9 uku. 28-uku. 29 fu. 1
  • Hatimaye Wapata Mtoto!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hatimaye Wapata Mtoto!
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Alimwita “Binti ya Mfalme”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Unaweza Kuiga Imani ya Abrahamu na Sara!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • “Wewe Ni Mwanamke Mwenye Sura Nzuri”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Alipokuwa Mtoto Aliteswa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 9 uku. 28-uku. 29 fu. 1
Sara akiwa ndani ya hema anasikiliza malaika wanapozungumza na Abrahamu

SOMO LA 9

Hatimaye Wapata Mtoto!

Abrahamu na Sara walikuwa wameoana kwa miaka mingi. Waliacha nyumba yao nzuri huko Uru na sasa walikuwa wakiishi katika mahema. Lakini Sara hakuwa akilalamika kuhusu hali yao, kwa sababu alimtegemea Yehova.

Sara alitamani sana kupata mtoto hivi kwamba alimwambia Abrahamu hivi: ‘Ikiwa mtumishi wangu Hagari atapata mtoto na wewe, mtoto huyo atakuwa kama mwanangu.’ Baada ya muda, Hagari akajifungua mtoto aliyeitwa Ishmaeli.

Sara akiwa mjamzito

Miaka mingi baadaye, Abrahamu alipokuwa na umri wa miaka 99 na Sara alipokuwa na miaka 89, walitembelewa na wageni watatu. Abrahamu aliwakaribisha ili wapumzike chini ya kivuli cha mti na kula chakula. Je, unajua wageni hao walikuwa nani? Walikuwa malaika! Walimwambia Abrahamu hivi: ‘Mwaka ujao wakati kama huu, wewe na mke wako mtapata mtoto.’ Sara alikuwa akiwasikiliza katika hema lake. Alicheka na kuwaza hivi: ‘Je, kwa kweli ninaweza kuzaa mtoto nikiwa mzee?’

Mwaka uliofuata, Sara alijifungua mtoto wa kiume, kama ambavyo malaika wa Yehova aliahidi. Abrahamu alimwita mtoto huyo Isaka, jina linalomaanisha “Kicheko.”

Isaka alipokuwa na umri wa miaka mitano hivi, Sara alimwona Ishmaeli akimdhihaki Isaka. Kwa kuwa alitaka kumlinda mtoto wake, alienda kwa Abrahamu na kumwomba awafukuze Hagari na Ishmaeli. Mwanzoni, Abrahamu alikataa. Lakini Yehova alimwambia Abrahamu hivi: ‘Msikilize Sara. Nitamlinda Ishmaeli. Lakini nitatimiza ahadi yangu kupitia Isaka.’

Sara akiwa na Isaka wakati Hagari na Ishmaeli wakiondoka

“Kwa imani, Sara pia alipokea nguvu za kupata uzao, . . . kwa kuwa alimwona kuwa mwaminifu Yule aliyekuwa ameahidi.”​—Waebrania 11:11

Maswali: Sara alisikia malaika wakimwambia Abrahamu nini? Yehova alifanya nini ili kumlinda Isaka?

Mwanzo 16:1-4, 15, 16; 17:25-27; 18:1-15; 21:1-14; Waebrania 11:11

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki