Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w81 6/1 kur. 20-21
  • Alipokuwa Mtoto Aliteswa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alipokuwa Mtoto Aliteswa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Habari Zinazolingana
  • Hatimaye Wapata Mtoto!
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Mungu Anajaribu Imani ya Ibrahimu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Unaweza Kuiga Imani ya Abrahamu na Sara!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
w81 6/1 kur. 20-21

Neno la Mungu Li Hai

Alipokuwa Mtoto Aliteswa

UKIWA kijana, huenda ukawa unaona vigumu leo kuwa Mkristo wa kweli. Huenda ukawa unadhihakiwa kwa sababu ya kukataa kuvuta tumbako au kutumia dawa za kulevya. Au huenda ukateswa kwa sababu ya kukataa kushiriki sherehe zinazopingana na kanuni za Biblia. Jambo hilo linakumbusha namna alivyoteswa Isaka, mwana kijana wa Ibrahimu na mkewe mpendwa Sara.

Kwa Isaka taabu yake ilifikia upeo wake wakati wa karamu aliyofanya Ibrahimu katika siku ya Isaka kuachishwa kunyonya. Wakati huo, Isaka alikuwa na umri wapata miaka mitano. Siku zile akina mama waliwanyonyesha watoto wao kwa muda mrefu. Wakati wa karamu hiyo, Ishmaeli, mwana tineja (miaka 13-19) alianza kumdhihaki na kumchekelea nduguye mdogo. Hayo hayakuwa mabishano ya watoto tu. Biblia inasema kwamba kwa kweli Ishamaeli “alianza kumtesa” Isaka.—Gal. 4:29, NW.

Sara aliona yaliyokuwa yakitukia, naye hakuyafurahia hata kidogo. Kwa wazi kuteswa kwa Isaka kulihusiana na ulizo la kwamba ni nani ambaye angerithi aliyokuwa amejipatia Ibrahimu. Kwa hiyo Sara alimwendea Ibrahimu na kumwambia: ‘Mwambie Hajiri na mwanawe waondoke. Hatashiriki urithi wa mwanangu lsaka.’

Jambo hilo likamwudhi Ibrahimu. Yeye hakutaka kumfukuza Ishmaeli, kwa kuwa yeye pia alikuwa mwanawe. Lakini Mungu alimwamibia Ibrahimu amsikilize mkewe Sara. Kwa hiyo Ibrahimu akawapa Hajiri na mwanawe vitu walivyohitaji kwa safari yao akawaacha waende zao.​—Mwa. 21:8-14.

Mtu anayeteswa aweza kupata kitia-moyo kutokana na habari hiyo ya Biblia juu ya Isaka. Sababu gani? Kwa sababu, baada ya wakati kupita, kudhihakiwa na Ishmaeli kulikomeshwa. Yehova Mungu alihakikisha kwamba Ibrahimu alichukua hatua ya kuondoa chanzo cha taabu katika nyumba yake. Vivyo hivyo leo, Mungu hataruhusu uteseke kuliko vile unavyoweza kuvumilia. Yeye atakupa nguvu ili uweze kuvumilia, au atahakikisha kwamba mwishowe chanzo cha tatizo hilo kimeondolewa.​—1 Kor. 10:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki