Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 13 uku. 36-uku. 37 fu. 1
  • Yakobo na Esau Wafanya Amani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yakobo na Esau Wafanya Amani
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Unautazamia Urithi kwa Bidii?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Mapacha Waliokuwa Tofauti
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yakobo Alipewa Urithi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 13 uku. 36-uku. 37 fu. 1
Yakobo anainama na Esau anakimbia kumwelekea

SOMO LA 13

Yakobo na Esau Wafanya Amani

Yehova alimwahidi Yakobo kwamba atamlinda kama alivyofanya kwa Abrahamu na Isaka. Yakobo aliishi katika eneo lililoitwa Harani. Alioa, akapata watoto na kuwa tajiri sana.

Baadaye, Yehova alimwambia Yakobo hivi: ‘Rudi katika nchi ya baba zako.’ Hivyo, Yakobo na familia yake walianza safari ndefu ya kurudi Kanaani. Wakiwa njiani, watu fulani walimjia Yakobo na kumwambia: ‘Ndugu yako Esau yuko njiani anakuja, akiwa pamoja na wanaume 400!’ Yakobo aliogopa kwamba huenda Esau angemshambulia yeye na familia yake. Alisali hivi kwa Yehova: ‘ Tafadhali nilinde dhidi ya ndugu yangu.’ Siku iliyofuata, Yakobo alituma zawadi nyingi kwa Esau, yaani, kondoo, mbuzi, ng’ombe, ngamia na punda.

Usiku huo, Yakobo alipokuwa peke yake alimwona malaika! Malaika alianza kupigana naye. Walipigana mweleka hadi asubuhi. Ingawa Yakobo aliumizwa, hakuacha kupigana. Kisha malaika akamwambia: ‘Niache niende.’ Lakini Yakobo akamjibu: ‘Sitakuacha mpaka unibariki.’

Mwishowe malaika akambariki Yakobo. Sasa Yakobo alijua kwamba Yehova atamlinda ili Esau asimshambulie.

Asubuhi, Yakobo alimwona kwa mbali Esau akija na wanaume 400. Yakobo alimkaribia Esau ndugu yake na kuinama chini mara saba. Esau alimkimbilia Yakobo na kumkumbatia. Wakalia pamoja na kufanya amani. Unafikiri Yehova alihisije Yakobo alipofanya amani na ndugu yake?

Baadaye, Esau alirudi kwake, na Yakobo akaendelea na safari. Yakobo alikuwa na watoto wa kiume 12. Watoto hao ni Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Dani, Naftali, Gadi, Asheri, Isakari, Zabuloni, Yosefu, na Benjamini. Mmoja wa watoto hao, yaani, Yosefu—alitumiwa na Yehova kuwakomboa watu Wake. Je, unajua alifanya hivyo jinsi gani? Acheni tuone.

“Endeleeni kuwapenda adui zenu na kusali kwa ajili ya wale wanaowatesa ninyi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni.”​—Mathayo 5:44, 45

Maswali: Kwa nini Yakobo alibarikiwa? Yakobo alifanyaje amani na Esau?

Mwanzo 28:13-15; 31:3, 17, 18; 32:1-29; 33:1-18; 35:23-26

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki