Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 19 uku. 50-uku. 51 fu. 2
  • Mapigo Matatu ya Kwanza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapigo Matatu ya Kwanza
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Musa na Haruni Wanamwona Farao
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Mapigo Sita Yaliyofuata
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Yehova Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 19 uku. 50-uku. 51 fu. 2
Musa na Haruni wamesimama mbele ya Farao

SOMO LA 19

Mapigo Matatu ya Kwanza

Waisraeli walilazimishwa kufanya kazi ngumu wakiwa watumwa. Yehova aliwatuma Musa na Haruni wamwambie hivi Farao: ‘Waruhusu watu wangu waondoke ili wakaniabudu huko nyikani.’ Kwa kiburi, Farao akasema hivi: ‘Mimi sijali Yehova anasema nini, na sitawaruhusu Waisraeli waondoke.’ Kisha Farao akawalazimisha wafanye kazi ngumu hata zaidi. Yehova angemfundisha Farao somo. Unajua alifanya nini? Alileta Mapigo Kumi juu ya Misri. Yehova alimwambia hivi Musa: ‘Farao amekataa kunisikiliza. Kesho asubuhi atakuwa kwenye Mto Nile. Nenda ukamwambie, kwa kuwa amekataa kuwaruhusu watu wangu waondoke, maji yote ya Mto Nile yatageuka kuwa damu.’ Musa alitii na akaenda kwa Farao. Farao alimwona Haruni akipiga maji ya Mto Nile kwa fimbo yake, nayo yakageuka kuwa damu. Samaki wakafa, mto ukaanza kunuka, na hakukuwa na maji safi ya kunywa kutoka kwenye Mto Nile. Lakini bado Farao alikataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke.

Baada ya siku saba, Yehova alimtuma tena Musa kwa Farao akamwambie hivi: ‘Usipowaruhusu watu wangu waondoke, vyura watajaa katika nchi yote ya Misri.’ Haruni akainua fimbo yake na vyura wakaanza kujaa na kuifunika nchi. Kulikuwa na vyura katika nyumba za watu, vitandani, na kwenye vyombo. Vyura walikuwa kila mahali! Farao alimwambia Musa amwombe Yehova akomeshe pigo hilo. Akaahidi kwamba angewaruhusu Waisraeli waende. Kisha Yehova akakomesha pigo hilo, na Wamisri wakawakusanya vyura hao mafungu-mafungu. Nayo nchi ikaanza kunuka. Lakini kwa mara nyingine tena, Farao hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.

Baada ya hapo, Yehova akamwambia Musa hivi: ‘Mwambie Haruni apige mavumbi ya dunia kwa fimbo yake, nayo yatakuwa mbu, au wadudu wadogo wanaouma.’ Papo hapo, mbu wakajaa kila mahali. Baadhi ya watu wa Farao walimwambia hivi: ‘Pigo hili limetoka kwa Mungu.’ Lakini bado Farao hakuwaruhusu Waisraeli waondoke.

Mapigo matatu kati ya mapigo kumi nchini Misri: damu kwenye Mto Nile, vyura, na mbu

“Nitawafanya wajue nguvu zangu na uwezo wangu, nao watalazimika kujua kwamba jina langu ni Yehova.”​—Yeremia 16:21

Maswali: Taja mapigo matatu ya kwanza. Kwa nini Yehova alileta mapigo hayo?

Kutoka 5:1-18; 7:8–8:19; Nehemia 9:9,10

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki