Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 20 uku. 52-uku. 53 fu. 3
  • Mapigo Sita Yaliyofuata

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mapigo Sita Yaliyofuata
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mapigo Matatu ya Kwanza
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Musa na Haruni Wanamwona Farao
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Yehova Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 20 uku. 52-uku. 53 fu. 3
Makundi ya nzige

SOMO LA 20

Mapigo Sita Yaliyofuata

Musa na Haruni walienda kumwambia Farao ujumbe huu kutoka kwa Mungu: ‘Ikiwa hutawaruhusu watu wangu waende zao, nitatuma nzi juu ya nchi yako.’ Makundi makubwa ya nzi yakaanza kuvamia nyumba za Wamisri, matajiri kwa maskini. Nchi yote ikajaa nzi. Lakini katika eneo la Gosheni, ambako Waisraeli walikuwa wanaishi, hakukuwa na nzi. Pigo la nne na yale yaliyofuata yaliwapata Wamisri peke yao. Farao akamsihi hivi Musa: ‘Mwombe Yehova kwa niaba yangu aondoe nzi hao, kisha watu wako wanaweza kuondoka.’ Hata hivyo, Yehova alipowaondoa nzi, Farao alibadili mawazo yake. Unafikiri Farao angejifunza kutii?

Yehova alisema hivi: ‘Ikiwa Farao ataendelea kukataa kuwaruhusu watu wangu waende zao, mifugo ya Wamisri itapatwa na ugonjwa na kufa.’ Siku iliyofuata, mifugo ikaanza kufa. Lakini mifugo ya Waisraeli haikufa. Lakini bado Farao aliendelea kuwa na moyo mgumu na hakutaka kuwaruhusu waondoke.

Kisha Yehova akamwambia Musa arudi kwa Farao na kurusha majivu angani. Majivu hayo yakawa vumbi na kujaza nchi yote na kuwafunika Wamisri. Mavumbi hayo yakasababisha majipu juu ya Wamisri na wanyama wao wote. Ingawa hivyo, Farao alikataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke.

Mapigo ya Misri kuanzia pigo la 4 hadi la 6: nzi, mifugo inakufa, majipu

Yehova akamtuma tena Musa kwa Farao amwambie hivi: ‘Bado unakataa kuwaruhusu watu wangu waondoke? Kesho mvua kubwa sana ya mawe itanyesha juu ya nchi.’ Siku iliyofuata, Yehova akafanya mvua kubwa ya mawe inyeshe, pia kukawa na ngurumo, na moto. Wamisri hawakuwa wamewahi kuona mvua kubwa kama hiyo. Miti yote na mimea iliharibiwa isipokuwa katika eneo la Gosheni. Farao akasema: ‘Msihi Yehova ili mvua iache kunyesha! Kisha nitawaruhusu mwende.’ Hata hivyo, mara tu mvua ilipoacha kunyesha, Farao alibadili mawazo yake tena.

Kisha Musa akasema hivi: ‘Sasa nzige watakula mimea yote iliyobaki baada ya mvua ya mawe kunyesha.’ Makundi ya nzige wengi wakala kila kitu kilichobaki shambani na kwenye miti. Farao akamsihi Musa hivi: ‘Mwombe Yehova awaondoe nzige hawa.’ Lakini hata baada ya Yehova kuwaondoa nzige, bado Farao aliendelea kuwa na moyo mgumu.

Yehova akamwambia Musa hivi: ‘Nyoosha mkono wako kuelekea angani.’ Papo hapo, giza zito likatokea katika nchi yote. Kwa siku tatu, Wamisri hawakuweza kuona kitu chochote. Waisraeli tu ndio waliokuwa na mwangaza katika nyumba zao.

Mapigo ya Misri kuanzia pigo la 7 hadi la 9: mvua kubwa, nzige, giza

Farao akamwambia Musa: ‘Wewe na watu wako mnaweza kwenda. Lakini waacheni wanyama wenu.’ Musa akasema: ‘Lazima twende na wanyama ili tukamtolee Mungu wetu dhabihu.’ Farao alikasirika sana. Akamwambia hivi Musa kwa hasira: ‘Toka hapa! Nikikuona tena nitakuua!’

“Nanyi mtaona tena tofauti kati ya mtu mwadilifu na mtu mwovu, kati ya yule anayemtumikia Mungu na yule asiyemtumikia.”​—Malaki 3:18

Maswali: Yehova alileta mapigo gani baadaye? Mapigo hayo yalitofautianaje na yale matatu ya kwanza?

Kutoka 8:20–10:29

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki