Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 21 uku. 54-uku. 55 fu. 2
  • Pigo la Kumi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pigo la Kumi
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Musa na Haruni Wanamwona Farao
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Mapigo Matatu ya Kwanza
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Yehova Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 21 uku. 54-uku. 55 fu. 2
Mwanamume Mwisraeli akipaka damu juu ya mlango wake

SOMO LA 21

Pigo la Kumi

Musa alimwahidi Farao kwamba hangeenda kumwona tena. Lakini kabla hajaondoka, alimwambia Farao hivi: ‘Katikati ya usiku, kila mzaliwa wa kwanza nchini Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao mpaka mzaliwa wa kwanza wa watumwa, atakufa.’

Yehova aliwaambia Waisraeli watayarishe mlo wa pekee. Alisema hivi: ‘Chinjeni kondoo dume au mbuzi wa mwaka mmoja, kisha mpake damu yake kwenye mlango wa nyumba zenu. Chomeni nyama hiyo na kuila pamoja na mkate usiotiwa chachu. Vaeni nguo na viatu na muwe tayari kuondoka. Nitawakomboa usiku wa leo.’ Hebu wazia jinsi Waisraeli walivyofurahi!

Katikati ya usiku, malaika wa Yehova alienda katika kila nyumba nchini Misri. Mzaliwa wa kwanza katika nyumba yoyote ambayo haikuwa imepakwa damu mlangoni, alikufa. Lakini malaika huyo alipita nyumba zilizokuwa zimepakwa damu. Kila mzaliwa wa kwanza alikufa katika familia zote nchini Misri, iwe ni za matajiri au maskini. Lakini hakuna mtoto hata mmoja wa Mwisraeli aliyekufa.

Hata mwana wa Farao mwenyewe alikufa. Farao hangeweza kuvumilia tena. Papo hapo akawaambia Musa na Haruni hivi: ‘Simameni. Ondokeni hapa. Nendeni mkamwabudu Mungu wenu. Chukueni wanyama wenu na mwende!’

Usiku huo, kukiwa na mwezi mpevu, Waisraeli waliondoka Misri wakiwa wamepangwa kulingana na familia na makabila yao. Kulikuwa na wanaume Waisraeli 600,000, pamoja na wanawake wengi na watoto. Pia, watu wengine wengi waliambatana nao ili wamwabudu Yehova. Hatimaye, Waisraeli walikuwa huru!

Ili kukumbuka jinsi ambavyo Yehova aliwakomboa, kila mwaka wangetayarisha mlo huo wa pekee. Mlo huo uliitwa Pasaka.

Waisraeli wakitoka Misri

“Kwa sababu hii nimekuacha ubaki: ili nionyeshe nguvu zangu kuhusiana na wewe na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”​—Waroma 9:17

Maswali: Pigo la kumi lilikuwa lipi? Waisraeli walipaswa kufanya nini ili kujilinda wakati wa pigo la mwisho?

Kutoka 11:1–12:42;13:3-10

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki