Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 23 uku. 60-uku. 61 fu. 4
  • Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Anatoa Sheria Zake 35
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Sinai Mlima wa Musa na wa Rehema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Walivunja Ahadi Yao
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 23 uku. 60-uku. 61 fu. 4
Waisraeli wamesimama kwenye sehemu ya chini ya Mlima Sinai

SOMO LA 23

Waisraeli Wamtolea Yehova Ahadi

Miezi miwili hivi baada ya Waisraeli kutoka Misri, walifika kwenye Mlima Sinai na kupiga kambi. Yehova akamwita Musa, naye akapanda juu mlimani, kisha Yehova akamwambia hivi: ‘Mimi niliwaokoa Waisraeli. Ikiwa watanitii na kushika sheria zangu, watakuwa watu wangu wa pekee.’ Musa akashuka kutoka mlimani na kuwaambia Waisraeli maneno ambayo Yehova alikuwa amesema. Waliitikiaje? Walisema hivi: ‘Tutafanya mambo yote ambayo Yehova anatuambia tufanye.’

Musa akapanda tena juu mlimani. Akiwa huko, Yehova akamwambia: ‘Baada ya siku tatu, nitazungumza nawe. Waonye watu wasijaribu kupanda juu kwenye Mlima Sinai.’ Musa akateremka kutoka mlimani na kuwaambia Waisraeli wajitayarishe kusikiliza kile ambacho Yehova atasema.

Waisraeli wanaona radi na wingu zito juu ya Mlima Sinai

Siku tatu baadaye, Waisraeli waliona radi na wingu zito kwenye mlima. Pia, walisikia sauti kubwa sana ya mingurumo na pembe. Kisha Yehova akashuka kwenye mlima katika moto. Waisraeli wakaogopa sana na kutetemeka. Mlima wote ulitetemeka sana na kufunikwa na moshi. Sauti ya pembe ikazidi kuwa kubwa. Kisha Mungu akasema: ‘Mimi ni Yehova. Msiabudu miungu mingine.’

Musa akapanda tena juu mlimani, na Yehova akampa sheria ambazo zilionyesha jinsi watu walivyopaswa kumwabudu na jinsi walivyopaswa kujiendesha. Musa akaandika sheria hizo kisha akawasomea Waisraeli. Wakaahidi hivi: ‘Tutafanya mambo yote ambayo Yehova ametuambia tufanye.’ Naam, Waisraeli walimtolea Mungu ahadi. Je, wangeitimiza?

“Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.”​—Mathayo 22:37

Maswali: Ni nini kilichotendeka kwenye Mlima Sinai? Waisraeli waliahidi kufanya nini?

Kutoka 19:1–20:21; 24:1-8; Kumbukumbu la Torati 7:6-9; Nehemia 9:13, 14

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki