Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 42 uku. 102-uku. 103 fu. 3
  • Yonathani Alikuwa jasiri na Mshikamanifu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yonathani Alikuwa jasiri na Mshikamanifu
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • “Wakashikamana na Kuwa Marafiki wa Karibu Sana”
    Igeni Imani Yao
  • Yonathani “Alifanya Kazi na Mungu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Yonathani—“Mwanamume Mmoja Katika Elfu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • “Hakuna Kitu Chochote Kinachoweza Kumzuia Yehova”
    Igeni Imani Yao
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 42 uku. 102-uku. 103 fu. 3
Yonathani na mtumishi wake aliyembebea silaha

SOMO LA 42

Yonathani Alikuwa Hodari na Mshikamanifu

Yonathani, mwana wa kwanza wa mfalme Sauli, alikuwa shujaa hodari wa vita. Daudi alisema kwamba Yonathani alikuwa na mbio kuliko tai na alikuwa na nguvu kuliko simba. Siku moja, Yonathani aliona wanajeshi Wafilisti 20 wakiwa juu ya mlima. Alimwambia hivi mtumishi aliyembebea silaha: ‘Tutawashambulia ikiwa tu Yehova atatupa ishara. Wafilisti wakituambia twende mahali walipo, hiyo itakuwa ishara kwamba tunapaswa kuwashambulia.’ Wafilisti wakapaaza sauti: ‘Njooni tupigane!’ Kwa hiyo, wanaume hao wawili wakapanda mlima huo na kuwashinda askari-jeshi hao.

Yonathani akimpa Daudi baadhi vitu vyake

Kwa kuwa Yonathani alikuwa mtoto wa kwanza wa Sauli, yeye ndiye aliyepaswa kuwa mfalme baada ya baba yake. Lakini Yonathani alijua kwamba Yehova alikuwa amemchagua Daudi kuwa mfalme wa Israeli anayefuata. Yonathani hakumwonea Daudi wivu. Yonathani na Daudi wakawa marafiki wa karibu. Waliahidi kulindana na kuteteana. Yonathani akampa Daudi koti, upanga, upinde, na mshipi wake kama ishara ya urafiki wao.

Daudi alipokuwa akimkimbia Sauli, Yonathani alimwendea na kumwambia hivi: ‘Usiogope, uwe jasiri. Yehova amekuchagua kuwa mfalme. Hata baba yangu anajua jambo hilo.’ Je, ungependa kuwa na rafiki mzuri kama Yonathani?

Zaidi ya mara moja, Yonathani alihatarisha maisha yake ili kumsaidia rafiki yake. Alijua kwamba Mfalme Sauli alitaka kumuua Daudi, kwa hiyo akamwambia baba yake hivi: ‘Ukimuua Daudi utakuwa ukifanya dhambi; hajafanya kosa lolote.’ Sauli alimkasirikia Yonathani. Miaka michache baadaye, Sauli na Yonathani wakafa vitani.

Baada ya Yonathani kufa, Daudi alimtafuta Mefiboshethi, mwana wa Yonathani. Daudi alipompata Mefiboshethi, alimwambia hivi: ‘Kwa sababu baba yako alikuwa rafiki yangu wa karibu, nitakutunza maisha yako yote. Utaishi katika nyumba yangu ya kifalme na utakula mezani pangu.’ Daudi hakumsahau kamwe rafiki yake Yonathani.

“Mpendane kama vile nilivyowapenda. Hakuna mtu aliye na upendo mkuu kuliko huu, kwamba mtu atoe uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”​—Yohana 15:12, 13

Maswali: Yonathani alionyeshaje kwamba alikuwa jasiri? Yonathani alionyeshaje kwamba alikuwa mshikamanifu?

1 Samweli 14:1-23; 18:1-4; 19:1-6; 20:32-42; 23:16-18; 31:1-7; 2 Samweli 1:23; 9:1-13

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki