Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 82 uku. 192-uku. 193 fu. 2
  • Yesu Anawafundisha Wanafunzi Wake Jinsi ya Kusali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Anawafundisha Wanafunzi Wake Jinsi ya Kusali
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Kuhusu Sala Ambazo Mungu Anasikiliza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Yesu Anatufundisha Kusali
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Je, Tunapaswa Kusali kwa Yesu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 82 uku. 192-uku. 193 fu. 2
Farisayo akisali hadharani na watu wakisimama ili kumwangalia

SOMO LA 82

Yesu Awafundisha Wanafunzi Wake Jinsi ya Kusali

Mafarisayo walifanya mambo mengi ili tu waonekane na watu. Kwa mfano, waliwatendea wengine kwa fadhili ili kujionyesha. Walisali kwenye maeneo yenye watu wengi ili kila mtu awaone. Pia, walikariri sala ndefu na kuzirudia-rudia walipokuwa wanasali kwenye masinagogi au kwenye njia panda ili wengine wawasikie. Kwa hiyo, watu walishangaa Yesu alipowaambia hivi: ‘Msisali kama Mafarisayo. Wao hufikiri kwamba Mungu atafurahishwa na maneno yao mengi, lakini sivyo ilivyo. Sala ni kati yako wewe na Yehova. Msiseme mambo yaleyale tena na tena. Yehova anataka umwambie jinsi unavyohisi kikweli.

Mvulana akiwa amepiga magoti ili kusali

‘Mnapaswa kusali hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.”’ Pia, Yesu aliwaambia kwamba wanapaswa kusali kuhusu mahitaji ya chakula cha siku hiyo, kuomba msamaha wa makosa yao, na kuhusu mambo mengine ya kibinafsi.

Yesu alisema hivi: ‘Msiache kamwe kusali. Endeleeni kumwomba Baba yenu, Yehova, mambo mazuri. Kila mzazi hupenda kumpa mtoto wake vitu vizuri. Ikiwa mtoto wako ataomba mkate, je, utampa jiwe? Akiomba samaki, je, utampa nyoka?’

Kisha, Yesu akafafanua somo la mfano huo: ‘Ikiwa ninyi mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, je, Baba yenu, Yehova, hatawapa ninyi roho takatifu? Mnachopaswa kufanya ni kuomba.’ Je, unafuata ushauri wa Yesu? Wewe huwa unasali kuhusu mambo gani?

“Endeleeni kuomba, nanyi mtapewa; endeleeni kutafuta, nanyi mtapata; endeleeni kupiga hodi, nanyi mtafunguliwa.”—Mathayo 7:7

Maswali: Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wasali jinsi gani? Je, unasali kuhusu mambo ambayo ni muhimu kwako?

Mathayo 6:2-18; 7:7-11; Luka 11:13

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki