Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 86 uku. 200-uku. 201 fu. 1
  • Yesu Amfufua Lazaro

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Amfufua Lazaro
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mtu Aliyekuwa Maiti Siku Nne
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Kwa Nini Yesu Alikawia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Inakuwaje Tunapokufa?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Inakuwaje Wakati wa Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 86 uku. 200-uku. 201 fu. 1
Lazaro aliyefufuliwa akiwa pamoja na dada zake Maria na Martha

SOMO LA 86

Yesu Amfufua Lazaro

Yesu alikuwa na marafiki watatu wa karibu sana ambao waliishi Bethania. Marafiki hao walikuwa Lazaro na dada zake wawili, Maria na Martha. Siku moja, Yesu alipokuwa ng’ambo ya Yordani, Maria na Martha walimtumia ujumbe huu wa dharura: ‘Lazaro ni mgonjwa sana. Tafadhali, njoo upesi!’ Hata hivyo, Yesu hakwenda mara moja. Alisubiri kwa siku mbili zaidi, kisha, akawaambia wanafunzi wake: ‘Twendeni Bethania. Lazaro amelala, nami ninaenda kumwamsha.’ Mitume wakamwambia hivi: ‘Ikiwa Lazaro amelala, hiyo itamsaidia kupata nafuu.’ Kwa hiyo, Yesu akawaambia hivi waziwazi: ‘Lazaro amekufa.’

Yesu alipofika Bethania, siku nne zilikuwa zimepita tangu Lazaro alipozikwa. Umati mkubwa wa watu ulikuwa umekuja kuwafariji Martha na Maria. Baada ya Martha kusikia kwamba Yesu amekuja, alikimbia ili akampokee. Akamwambia hivi: “Bwana, kama ungekuwa hapa ndugu yangu hangekufa.” Yesu akamwambia: ‘Ndugu yako atafufuka. Martha, unaamini jambo hilo?’ Akajibu: ‘Ninaamini kwamba atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.’ Yesu akamwambia: “Mimi ndiye ufufuo na uzima.”

Kisha, Martha akaenda kwa Maria na kumwambia: ‘Yesu amekuja.’ Maria akatoka na kumkimbilia Yesu, nao umati ukamfuata. Alipofika, akaanguka miguuni pake huku akibubujikwa na machozi. Akamwambia Yesu: ‘Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yetu hangekufa.’ Yesu alipoona jinsi Maria alivyohuzunika, yeye pia akatokwa na machozi. Umati ulipomwona akilia, wakasema: ‘Ona, jinsi Yesu alivyompenda Lazaro.’ Lakini wengine wakawa wakiuliza: ‘Kwa nini hakuzuia rafiki yake asife?’ Yesu angefanya nini?

Yesu alienda kwenye kaburi ambalo lilikuwa limefunikwa kwa jiwe kubwa. Akawaamuru na kusema: “Liondoeni jiwe.” Martha akajibu: ‘Lakini siku nne zimepita! Mwili wake utakuwa unanuka.’ Hata hivyo, wakaliondoa jiwe, naye Yesu akasali na kusema: ‘Baba, ninakushukuru kwamba umenisikia. Ninajua kwamba sikuzote wewe hunisikia; lakini ninasema kwa sauti ili watu hawa waamini kwamba umenituma.’ Kisha, akaita kwa sauti kubwa: “Lazaro, njoo huku nje!” Jambo la kushangaza likatokea: Lazaro akatoka kaburini, akiwa bado amefungwa kwa vitambaa. Yesu akawaambia: ‘Mfungueni, mwacheni aende.’

Wengi walioshuhudia ufufuo huo wakaanza kumwamini Yesu. Lakini wengine wakaenda na kuwaambia Mafarisayo. Tangu siku hiyo, Mafarisayo wakapanga njama ya kumuua Lazaro na Yesu. Yuda Iskariote, mmoja wa wale mitume 12, akaenda kisiri kwa Mafarisayo na kuwauliza: ‘Mtanipa nini nikiwasaidia kumkamata Yesu?’ Wakakubaliana kumlipa vipande 30 vya fedha, hivyo, Yuda akawa akitafuta nafasi ya kumsaliti Yesu kwa Mafarisayo.

“Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu anayeokoa; Na Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu huokoa kutoka katika kifo.”​—Zaburi 68:20

Maswali: Simulia jinsi Lazaro alivyofufuliwa. Mafarisayo walipanga kufanya nini waliposikia habari kuhusu Lazaro?

Mathayo 26:14-16; Yohana 11:1-53; 12:10

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki